Jamaa naona kaenda kuwaambia wapiga kura waliomnyima Ubunge kwamba hakuwa na shida ya pesa ila uwakilishi... Ila wachagga wabishi sana, huyu jamaa angekuwa anagombea Mtimbwilimbwi angepita kwa kishindo..
Yani kwakuwa ana gari au uwezo wa kifedha mkubwa basi asingepaswa kutoswa ubunge? Hii kanuni ya wapi au kigezo cha wapi hiki?
Mosha alichemka sana. Kwanza alishindwa kutambua kuwa chama alichopitia kugombea ubunge kinakubwa na changamoto kubwa sana moshi. Hata hivyo hii haikuwa sababu kubwa ya yeye kutoswa.
Ukweli ni kuwa namna alivoendesha kampeni zake ndiko kulikomfelisha wala sio jingine. Alifanya siasa za kizamni sana. Binafsi naamini.jamaa angekuwa ametulia,kujipanga vizuri na kuwa na watu makini huu mwaka angeng'oa jimbo la moshi. Kuna watu wengi pia walitamani kufanya mabadiliko ya uongozi moshi lakini walibadili muelekeo baada ya.kuona siasa za zisizo natija kutoka kwa timu ya mosha.
Nikupe mfano mdogo. Mosha alifanya mkutano KCMC maduka ya juu. Kabla ya yeye kufika wapambe wake walishafika na wakawa wanamwaga.sera. Mkutano unafanyika nchi(inch) chache kutoa barabara kuu na gari zinapita. Ikaja haice ya.KCMC -SIDO nyuma inabendera ya chadema wapambe wake wakaifuta kuichomoa.bendera na kuivunja huku haice unashusha abiria. Then ikapita gari nyingine na bendera ya chadema nyuma akipigwa fimbo pale nyumabkwenye bendera,kisa pikipiki pia ikafanyiwa hivyo hivyo. Kumbuka mkutano unafanyika pembeni tu ya barabara kwahiyo sio kuwawafuasi wa chadema waliufuta mkutano wa ccm
Cha ajabu aliyekuwa sijui nani wake wa kampeni badala ya kukemea kitendo hicho.akawa anakiunga mkono. Kwa mazingira hayo pamoja na sehemu zingine zenye.ma
tukio kama hayo kweli ulitaraji ashinde? Binafsi nadhani ningehuzunika sana kama jamaa angeshinda.