Dede 01
JF-Expert Member
- May 12, 2024
- 1,182
- 2,248
Habari wakuu!
Kutokana na migogoro ambayo haiishi hapa katika nchi zetu za Afrika hususani kusini mwa jangwa la Sahara napendekeza baadhi ya mambo ambayo yatadumisha amani yetu.
1.Viongozi wa Africa waungane na wamalize tofauti zao zisio na tija kama tunavyoona baina ya Kagame na Tshisekedi. Hii ndo njia pekee itakayolinda Afrika yetu dhidi ya mabepari.
2. Sisi kama waafrika tujenge silaha zetu wenyewe zinazoendana na teknolojia ya sasa tuachane na ma AK 47 na Mabazuka. Serikali yetu ikishirikiana na EAC au SADC ianzishe kiwanda cha kutengeneza vifaa vya kisasa kama missiles, hypersonic weapons, jets za kisasa na ikiwezekana hata nuclear weapons na submarines. Hii ndo njia utakayotusaidia kulinda mipaka yetu dhidi ya mabepari endapo WW3 ikitokea.
3. Nchi za Afrika zisaidiane katika masuala ya kiintellijensia, hii itasaidia kutuliza na kuzuia mashambulizi ya kigaidi yanayoweza kutokea barani kwetu.
4. Nchi za kiAfrika ziachane na habari za misaada mabepari wanatumia misaada hii kuchukua rasilimali zetu. Haiwezekani karne hii ya 21 bado tunaomba vyandarua na tunaagiza dawa kutoka nje.
5. Hii inaenda kwa viongozi moja kwa moja, waache tamaa waangalie maslahi ya wananchi wao.
Yangu ni hayo tu ila kiwanda cha silaha za kisasa hapa Afrika ni muhimu.
Kutokana na migogoro ambayo haiishi hapa katika nchi zetu za Afrika hususani kusini mwa jangwa la Sahara napendekeza baadhi ya mambo ambayo yatadumisha amani yetu.
1.Viongozi wa Africa waungane na wamalize tofauti zao zisio na tija kama tunavyoona baina ya Kagame na Tshisekedi. Hii ndo njia pekee itakayolinda Afrika yetu dhidi ya mabepari.
2. Sisi kama waafrika tujenge silaha zetu wenyewe zinazoendana na teknolojia ya sasa tuachane na ma AK 47 na Mabazuka. Serikali yetu ikishirikiana na EAC au SADC ianzishe kiwanda cha kutengeneza vifaa vya kisasa kama missiles, hypersonic weapons, jets za kisasa na ikiwezekana hata nuclear weapons na submarines. Hii ndo njia utakayotusaidia kulinda mipaka yetu dhidi ya mabepari endapo WW3 ikitokea.
3. Nchi za Afrika zisaidiane katika masuala ya kiintellijensia, hii itasaidia kutuliza na kuzuia mashambulizi ya kigaidi yanayoweza kutokea barani kwetu.
4. Nchi za kiAfrika ziachane na habari za misaada mabepari wanatumia misaada hii kuchukua rasilimali zetu. Haiwezekani karne hii ya 21 bado tunaomba vyandarua na tunaagiza dawa kutoka nje.
5. Hii inaenda kwa viongozi moja kwa moja, waache tamaa waangalie maslahi ya wananchi wao.
Yangu ni hayo tu ila kiwanda cha silaha za kisasa hapa Afrika ni muhimu.