Dawasa wanatupiga

Dawasa wanatupiga

Hamna cha leakage wala nini, nyumbani kwetu tulitafuta hiyo leakage hadi basi
Halafu leakage hata kama ingekuwa kubwa kiasi hicho,

Mfano kuna kipindi tumepima maji kabisa tuliyotmia kwa mwezi kwenye simtank

Tulitumia simtank 4 za ujazo wa lita 2000 ambazo ni lita 8000 sawa na unit 8, ila matumizi bili ikaja unit 37, na mita zinasoma tumetumia unit hizo kweli
Sasa unit 8 hadi 37, leakage kubwa kiasi hicho ingeonekana tu
Hewa kwenye bomba nayo inafanya mita ikimbie kuliko kawaida
 
Inawezekana meter ni mbobu kweli.

Ila kwa upande wangu iko hivi.....

Huwa naweka kumbukumbu za matumizi ya kila mwezi (unit).

Kwa mfano ..matumizi ya maji September ni unit 59.

Yaani last time meter ilisoma 1813, na hadi juzi walikuja kusoma meter na kukuta 1872.
Hapo unachukua Current reading - previous reading ( 1872-1813) = 59 Unit.
Huwa nathibitisha kama alichosoma mosoma mita ni sahihi.

Then najiandaa kulipa bill, na hapo nakaa nikijua pesa nitakayolipa.

Unit moja ni 1,680/=

Data zangu na data za Dawasa hazijawahi kukinzana.
Wewe hautofautiani namm
 
Tatizo wanashindana nani anakusanya hela nyingi kila wilaya ukikusanya kidogo unatumbuliwa hao mameneja wao.
 
Suluhisho ni kufunga maji yasipite kwny mita wakat umesafiri...kuna ila gate valve kabla maji hayajaingia kwny mita
 
Nimefanya tathimini nikagundua hizi mita za maji hapa Dar ni majanga sana. Yaani hata ukiwa umesafiri bili inakuja ileile na mita inatembea.

Kuna kitu hakipo sawa kwenye mita za maji jamaa wanatupiga. Wanatuumiza sana jamani was galleries tena ufanisi wa mita zao.
AUWSA wa Arusha ndiyo majambazi kabisa. Bill za maji ni kubwa kuliko uhalisia. Wanabambika tu bill hawa waungwana
 
Hamna cha leakage wala nini, nyumbani kwetu tulitafuta hiyo leakage hadi basi
Halafu leakage hata kama ingekuwa kubwa kiasi hicho,

Mfano kuna kipindi tumepima maji kabisa tuliyotmia kwa mwezi kwenye simtank

Tulitumia simtank 4 za ujazo wa lita 2000 ambazo ni lita 8000 sawa na unit 8, ila matumizi bili ikaja unit 37, na mita zinasoma tumetumia unit hizo kweli
Sasa unit 8 hadi 37, leakage kubwa kiasi hicho ingeonekana tu

ulipiga picha meter yako kuonyesha unit zake na ukafika dawasa kuwaonyesha bill section utofauti meter na bill au porojo tu
 
mimi mbona kila mwezi nalipa 7600/ sh lakini bahati mbaya msomaji mwezi wa 9 kasoma vibaya bill imekuja million 1 na laki 5 badala ya kulipa elfu 7. nimeenda dawasa na wamerekebesha bill
 
unajua mpka now sijaelewa lawama zenu zinaenda wapi hivi unashindwa kusoma mita yako na ukaend atoa malalamiko ukiona hawatekelezi si bora uchangie mita ya jirani ujue ukitumia unit kadhaa unamlipa n yy atalipa idarani kuliko kukaa kulaumu wakati njia zipo nyingi na ukitaka usisumbuke chimba maji yako mbona huduma ya uchimbaji skuhzi ni nafuu sana
 
nawaombeni woote mnao lalamika swali ni moja tu : JE MITA YAKO INASOMA UNIT NGAPI? JE INALINGANA NA BILL ILIYOKUJA. kama inalingana huna haja ya kulalamika dawasa wanaangalia unit ulizo tumia mfano mwezi wa 8 meter inasoma 000094 mwezi wa 9 wamekuja meter yako inasoma 000099 maana yake umetumia maji unit 5 kwa mwezi wa 9 sawa na sh 8,398.15/ kumbuka unit 1 sawa na sh 1679.63.
 
Inawezekana meter ni mbobu kweli.

Ila kwa upande wangu iko hivi.....

Huwa naweka kumbukumbu za matumizi ya kila mwezi (unit).

Kwa mfano ..matumizi ya maji September ni unit 59.

Yaani last time meter ilisoma 1813, na hadi juzi walikuja kusoma meter na kukuta 1872.
Hapo unachukua Current reading - previous reading ( 1872-1813) = 59 Unit.
Huwa nathibitisha kama alichosoma mosoma mita ni sahihi.

Then najiandaa kulipa bill, na hapo nakaa nikijua pesa nitakayolipa.

Unit moja ni 1,680/=

Data zangu na data za Dawasa hazijawahi kukinzana.

unit 1 ni sawa na sh 1679.63
 
Kama unajua unit moja ya maji ni kiasi gani, wewe angalia tu mita yako, hutaibiwa hata senti.
 
Kitu kingine ili ujue kama kwako kuna likeji ni kufunga mabomba yote,kisha kacheki Mita inazunguka,ikiwa inazunguka ujue kuna likeji na kama haizunguki ujue upo salama
 
hakuna anayekupiga, nyumba ina leakage bwashee

nilipanga sehemu miaka ya nyuma, nilikua nalipa 30k-40k ya Maji kwa mwezi

nakumbuka one day, bafuni, naona kwa mbaaaali kuna sehem maji yanachuruzika, kucheki vizuri ni leakage , tena ndani ya ukuta

nikanunua jaba nalijaza maji, then nafunga ile gate valve ya mita kule nje, guess what, bili ilikuja 6000-7000 kwa mwezi kwa miezi yote niliyokaa pale
 
Utakuja kukosa maji siku moja .....mtandao wa nchi hii ni wa grade III unakata muda wowote....waulize madereva wa serikali kuna muda wanalala kwenye ma-pump ya GIPSA.
Wanahujumu Kwa makusudi ili wawapige Muende kuongeza mafuta kwenye vituo vya mafuta binafsi.


Hii nchi watu wanafanya hujuma kwenye sehemu nyingi

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
unajua mpka now sijaelewa lawama zenu zinaenda wapi hivi unashindwa kusoma mita yako na ukaend atoa malalamiko ukiona hawatekelezi si bora uchangie mita ya jirani ujue ukitumia unit kadhaa unamlipa n yy atalipa idarani kuliko kukaa kulaumu wakati njia zipo nyingi na ukitaka usisumbuke chimba maji yako mbona huduma ya uchimbaji skuhzi ni nafuu sana
Kwahiyo MTU unabomba bafuni kwako tena chumbani uende kuchota maji Kwa jirani ya kuoga!


Una kichwa kibovu badala utatue tatizo unatafuta suppression

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom