Ni wazi ndugu yetu anatumia madawa ya kulevya tena kwa mda mrefu, ila tukikumbuka mchango wake katika tasnia ya burudani hususan muziki, Daz baba ana haki ya kukumbukwa kwani ame-inspire vijana mpaka wazee kugeuza mtizamo wao kuhusu muziki wa kizazi kipya.
Kumbuka kazi yao ya kundi; Wimbo 'barua', 'matatizo', 'nitafanya nini'. Ukija kazi zake binafsi; Wimbo 'wife', 'elimu dunia', 'umbo namba nane', 'nipe tano' pamoja na kazi nyingine alizoshirikishw kama ''wana mwita kaka pouwa'', Hakika alikonga nyoyo zetu kwa utunzi mzuri na sauti nzuri iliyofanya wengi tumjue. Kwanini sasa tusimsaidie ndugu yetu?
Wito wangu kwa Media, nyie mna nguvu na ushawishi wa kuaminika, naombeni tumsaidie Daz baba / Daz Mwalimu arudi katika hali yake.