DC JOKATE: HATULAZIMISHI WATU KUFANYA USAFI, BALI LITAKUWA ZOEZI SHIRIKISHI
Mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa Jokate Mwegelo amezindua kampeni ya "Pendezesha,safisha Dar es salaam" yenye lengo la kusafisha mkoa wa Dar es salaam.
Akizungumza katika eneo la Zakhem Mbagala, ambapo kampeni hiyo imezinduliwa kiwilaya, Mhe. Jokate amesema hawatawalazimisha watu kufanya usafi,bali litakuwa zoezi shirikishi.
"Hii sio kampeni ya siku moja kama alivyoagiza Mhe.Mkuu wa Mkoa,tofauti kubwa ya sasa hatushurutishi watu kufanya usafi,bali tumetengeneza mazingira watu waone wajibu wao katika hili".Alisema Mkuu huyo wa wilaya
Ameendelea kusema kuwa suala la usafi linapaswa kuwa ni utamaduni wa kila Mwananchi, huku akionesha kufurahishwa na jinsi mazingira ya eneo la Mbagala yalivyo kwa sasa.
Uzinduzi huo wa kampeni ya usafi umehudhuriwa na mstahiki meya wa halmashauri ya manispaa ya Temeke Mhe.Abdallah Mtinika pamoja na Mkurugenzi wa manispaa hiyo Ndugu Elihuruma Mabelya.
@jokatemwegelo
#safishapendezeshadaressalaam
#safishapendezeshatemeke
#kaziiendelee🇹🇿
Mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa Jokate Mwegelo amezindua kampeni ya "Pendezesha,safisha Dar es salaam" yenye lengo la kusafisha mkoa wa Dar es salaam.
Akizungumza katika eneo la Zakhem Mbagala, ambapo kampeni hiyo imezinduliwa kiwilaya, Mhe. Jokate amesema hawatawalazimisha watu kufanya usafi,bali litakuwa zoezi shirikishi.
"Hii sio kampeni ya siku moja kama alivyoagiza Mhe.Mkuu wa Mkoa,tofauti kubwa ya sasa hatushurutishi watu kufanya usafi,bali tumetengeneza mazingira watu waone wajibu wao katika hili".Alisema Mkuu huyo wa wilaya
Ameendelea kusema kuwa suala la usafi linapaswa kuwa ni utamaduni wa kila Mwananchi, huku akionesha kufurahishwa na jinsi mazingira ya eneo la Mbagala yalivyo kwa sasa.
Uzinduzi huo wa kampeni ya usafi umehudhuriwa na mstahiki meya wa halmashauri ya manispaa ya Temeke Mhe.Abdallah Mtinika pamoja na Mkurugenzi wa manispaa hiyo Ndugu Elihuruma Mabelya.
@jokatemwegelo
#safishapendezeshadaressalaam
#safishapendezeshatemeke
#kaziiendelee🇹🇿