DC Pangani, Zainab Abdallah ana moyo wa pekee. Alimshauri mumewe kuongeza mke kutokana na yeye kuwa busy na majukumu

Kaongeza wawili mpaka sasa na mmoja anatarajia kujifungua soon.
 
Mimi nakwambia ile siku najua anaenda kwa bimdogo ningekua naumwa hadi yeye mwenyewe ataogopa kuondoka. Au la nampa mchezo usiku kucha akifika kwa mke mwenza hata kumshika chuchu hawezi kwa jinsi alivyochoka.
Sasa si unaweza kumtoa roho aise mkamkosa wote halafu mnakuaga mna wivu kweli mkiolewa mke mwenza
 
Kwa kazi aliyonayo na zama hizi za hapa kazi tu! amefanya uamuzi sahihi sana. Vinginevyo nafasi ingeweza kuota mbawa!! nawaza tu
Hahahaa. KajiOsha baba asimuwahi
 





Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi. Zainab Abdallah, ameushangaza umma baada ya kumpongeza mume wake kwa kuongeza mke wa pili, kwani ni kitendo cha nadra sana kwa wanawake kufanya hivyo licha ya kuwa misingi ya dini inaruhusu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram mkuu wa wilaya huyo ameandika ujumbe huku akiujulisha umma kuwa wazo la mume wake kuongeza mke wa pili lilitoka kwake, baada ya kuona majukumu ya kazi yanambana na kushindwa kutekeleza majukumu ya ndoa.

“Assalaam Alaykum, nichukue nafasi hii kumpongeza Mume wangu kwa kuongeza mke wa pili. Kwa kuwa dini yetu ya Kiislam inaruhusu, wazo la kufanya hivyo lilitoka kwangu, kulingana na uzito wa majukumu yangu nalazimika mda mwingi kuwa mbali na nyumbani na hivyo mume wangu kukosa huduma za msingi”, ameandika Bi. Zainab Abdallah.

Mheshimiwa huyo wa serikali ya wamu ya tano aliendelea kuandika kuwa ...”Namshkuru kwa kunielewa na kulifanyia kazi ombi langu, hatimaye nimempata mwenzangu wa kusaidiana naye majukumu mazito ya ulezi wa mume. Alhamdulillah, M/Mungu ametupa riziki na uwezo, hivyo tunapaswa kutumia neema hizi na wengine. Mavazi ya mume wangu nimeyaandaa mwenyewe, yaa rabb atupe stara inshaaAllah.

 
Labda kapata kipozeo kingine huko anakokuwa busy, mumewe kumpa taarifa ya kuongeza mke akaona isiwe shida.
Lazima. Mwanamke hawezi kukubali kuongezewa mwenzie kama na yeye hana substitute.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…