DC Pangani, Zainab Abdallah ana moyo wa pekee. Alimshauri mumewe kuongeza mke kutokana na yeye kuwa busy na majukumu

Tatizo la mwanamke ni kufikiria siku ile ya kwanza mumewe kuongeza jiko akiwa anakula mema ya nchi huku yeye akiwa anachoma mahindi benchi! Hata hivyo ni suala la kawaida kabisa na linawezekana endapo mhusika atakuwa amejiandaa kisaikolojia.
 
Ngoja nimuoneshe hii le mbebez huenda akaniruhusu kuongeza namba 2... Lol.
 
Nikibahatika kupata uteuzi na mimi nitamwambia mume aongeze mke, ila kwa sharti moja tu.. Mume atulie na mkewe mpya, mimi asinisumbue... anipe nafasi ya kuhudumia wananchi huko wilayani
Nani atakaekuwa anakukuna huko kwenye majukumu?
 
Mwanamke wa Kiislamu amepokonywa uhuru wa nafsi na dini yake. Hakuna kupenda mtu mmoja watu wanne bali kupeana nafasi ya kushea basi. Mwanaume wa Kiislamu hapati upendo wa dhati toka moyoni bali maigizo ya watu wenye sononeko la nafsi. Povu ruksa.
Hii comment yako imenikumbusha novel inaitwa So long a letter by Mariama Ba'. Nimejikuta nimekikumbuka sana hii novel ya mama msenegali. Nimeisoma kitambo kweli.
 
Hiyo ni tafsri yako mkuu. Tatizo kila mtu anakuwa na tafsri ya maandiko kwenye kichwa chake. Ukweli ni kwamba kwenye Biblia hakuna Amri inayosema "na usiwe na mke zaidi ya mmoja". Hakuna amri kama hiyo.

Yakobo alikuwa na wake wawili na zaidi ya hapo akawachukua na mahouse girls(vijakazi) na kuwafanya wake zake pia na akazaa nao watoto. Jumla yake watoto 12 ndiyo hao taifa la Israeli leo hii ambalo ndilo taifa teule la MUNGU. Tena MUNGU akambariki sana Yakobo na watoto wake. Hivyo kama kuwa na mke zaidi ya mmoja ingekuwa ni machukizo kwa MUNGU, basi ni lazima BWANA MUNGU angemkemea Yakobo na asingekaa kimya na kuendelea kumbariki. Ukisoma maandiko utaona kuna mahali imeandikwa; "Maana yeye ambaye BWANA ampenda humrudi, naye humpiga kila mwana amkubaliye". Hivyo kama kuoa wake wengi ingekuwa ni makosa, BWANA angemrudi Yakobo na kumkanya. Kumbuka jinsi alivyomkanya na kumrudi Daudi kwa kosa la kuchukua mke wa Uria. Sababu kuchukua mke wa mwingine ni makosa, lakini kuoa wake wengi siyo makosa.

MUNGU wa Yakobo ndiyo huyo huyo MUNGU wetu leo hii, hajabadilika. Ikiwa hakumkasirikia Yakobo kwa kuoa mke zaidi ya mmoja, kwanini akukasirikie wewe?? MUNGU hana substandards hata siku moja. MUNGU ni mkamilifu tena sana na ndiyo maana tunasema MUNGU ni yule yule, jana na leo na kesho na milele yote. Kama kuoa zaidi ya mke mmoja ni makosa, basi wakati ule MUNGU anampa Musa amri kumi na sheria ya Torati, pia hili swala la kuoa mke zaidi ya mmoja lingewekwa kwenye Torati, lakini halipo kabisa ndani ya Torati. Tena fahamu kwamba YESU KRISTO hakuja kuleta amri mpya wala kuifuta Torati, bali alikuja kuikamilisha na kuifafanua.

Mkuu vespere unahitaji hekima na busara kulielewa neno la MUNGU.
 
Wanawake watatu kwanza sio wawili. Kuna boya mmoja humu alisema watu mpaka tuone insta ndo tujue wakati ndoa imefungwa ina week sijui watu tunajua. Kampa mimba Aggy tunajua. Bwana harusi ni balaa. Akifika miaka 30 atakua kaoa na kuacha wake wengi sana
 
Hii raha tele wa ndugu,laiti nisingekuwa,myahudi,ningekuwa Islam,nipate mambo kama haya,saafi kabisa,bila kokoro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…