Pre GE2025 DC wa Kisarawe, Petro Magoti achangia Mifuko 300 ya Saruji Ujenzi wa bweli la Msikiti, ahimiza na wengine wachangie ili Watoto Warudi mapema kusoma

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ni lazima hao watoto wakae hapo? waondolewe hapo waende shule
 
Yupo mmoja humu kaanzisha hadi uzi wa kimihemuko; Mkono Mmoja.
Dini zimekuja kutufanya majuha kabisa..... Hapa ishu ni mazingira mabovu watoto walipokua haijalishi wanasoma biblia au quran ishu ni usalama wao.

Sasa kama na usalama wa watoto ni jambo la kidini, tuna safari ndefu sana.
 
Ni lazima hao watoto walelewe hapo msikitini kwanini wasipelekwe shule wakapate elimu watoe ujinga?
Mkuu una mambo mchanganyiko sana kama unga wa ngano.

Dc kusema mahali ni pabovu ishu
Dc kuchangia cement na camera ishu
Dc kukaribisha wadau kwa mchango ishu
Sahivi tena kwanini watoto wapo hapo!!!!

Enjoy your weekend bro....
Kula bia kula bia.
 
Hiyo inaitwa "demage control" aligundua hawezi kushinda hiyo vita ya imani ya watu na endelea kubaki public fingure salama...........
 
Anajikosha!!! Hatudanganyiki. Msimamo wetu uko palepale
 
Walioanza kulalamika tena kwa mlengo wa "udini" bila shaka watabadili gia angani.....
Alifanya vizuri kutetea usalama wa watoto. Kelele za wadini zimempa wazo la kuhakikisha hatua zake hazichanganywi na udini.

Naamini angekua muijumaa asingepigiwa kelele.
Lazma amehofia na mamlaka ya uteuzi.
 
hehe! niliwaza hivi kumbe wapo wenye hekima wamemshauli haya ni step nzuri..
Kama mtu anataka kufanya biashara ya kutoa elimu kwa watoto si awekeze mtaji wake!? Na kama hana mtaji anachukua watoto wa watu kwa nini!?
 
Angeanza kufunga shule nyingi za umma hazina vyoo, shule ina wstoto 500 ina tundu moja ya choo, madarasa hamna watoto wanasomea chini ya miti, wanakaa chini madawati hamna, maji hamna.......mbona hizo shule hazijafungwa, acheni imani za watu watoto wangapi wako mitaani waliacha shule wanavuta bangi, hawana pa kulala kuna kosa gani kufundisha hao watu dini yao, acheni kuonea waislamu ni raia wa nchi hi.
 
Walioanza kulalamika tena kwa mlengo wa "udini" bila shaka watabadili gia angani.....
Bila kukemewa unafikiri angetoka kuchangia. Post yangu niliyoiandika imewafikia wakubwa zake na wamemsihi apunguze Munkari katika maamuzi yake.

Anyways ,tunampongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa msaada wa mifuko 300 ya cement ili kuharakisha ujenzi wa kituo hicho cha mafunzo ya kiislam.
 
Anajikosha tu baada ya kugundua ameyakanyaga. Kama lengo lilikuwa hilo angeenda na hizo cement tokea mwanzo.
Kabisa..tuushukuru uongozi wa Jamii forums kwa kutupa nafasi ya kuikosoa serikali na viongozi wake. Ile post yangu ya juzi imemfikia Dc petro na viongozi wenzake
 
Kwani huyu mkuu wa wilaya hawezi kutoa hiyo mifuko 300? Au kwasababu ana chuku na Imani ya uislamu.
 
Binadam hawana wema kaka, kila mtu anajikuta mtukufu hapa. Hakuna utakachofanya binadamu waone jema lako, Tangu mwanzo mheshimiwa alionesha nia njema na ndiomaan alikuwa tayri hata kuchangia nauli watoto warudishwe makwao kupisha ujenzi,
Shida watanzania tumejaa udini wa kipumbavu sana kiasi cha kufanya watu wasifikiri
 
Hakika kabisa, mi nnaona ni jambo jema sana alifanya kuwalinda watoto na mazingira mabaya.....cha ajabu walimwengu tunaingiza ujinga ujinga wa dini.

Bado nampongeza alikua sawa.
 
Msanii mzuri sana wa maigizo!
Hata mzee mstaafu Mangula anamjua vizuri!
Ila jamani haya maisha sijui kama malaika wangekuwa wanatuandikia Obituary tukifa ili zisomwe hadharani watoto na ndugu zetu wangeficha wapi sura zao!
 
Angeanza na shule za ummah zisio kua hata na matundu ya vyoo......ache wsislamu wanafundishwa dini yao hata chini ya miti.
 
Binadamu mna nongwa, bila yeye kukifungia hicho kituo mpaka kesho hao madogo wangekua wanaliwa na mbu tu.

Magoti ni shujaa wa hilo, apongezwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…