Pre GE2025 DC wa Kisarawe, Petro Magoti achangia Mifuko 300 ya Saruji Ujenzi wa bweli la Msikiti, ahimiza na wengine wachangie ili Watoto Warudi mapema kusoma

Pre GE2025 DC wa Kisarawe, Petro Magoti achangia Mifuko 300 ya Saruji Ujenzi wa bweli la Msikiti, ahimiza na wengine wachangie ili Watoto Warudi mapema kusoma

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Binadamu mna nongwa, bila yeye kukifungia hicho kituo mpaka kesho hao madogo wangekua wanaliwa na mbu tu.

Magoti ni shujaa wa hilo, apongezwe.
Kwani hao madogo walianza jana kusoma?
 
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti ametoa mifuko ya saruji 300 akianza kutanguliza mifuko 150 kwa ajili ya ujenzi wa bweni (hosteli) litakalotumika kwa ajili ya Watoto wanaopata mafunzo ya Dini ya Kiislamu Wilayani hapo ikiwa ni siku mbili tangu alipotoa maelekezo ya kusitishwa kulaza Watoto Msikitini hapo kutokana na mazingira kutokuwa rafiki ya kufundishia na kulaza watoto.
View attachment 3041341
Mifuko 150 imetolewa kwa Msikiti wa FALAF na Mifuko mingine 150 imetolewa kwa Msikiti wa Abdul-Aziz-Asharqiy, kwaajili ya Mabweni ili Watoto wasomee mazingira mazuri ambapo Misikiti yote ipo Kiluvya Madukani Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa Pwani

DC Magoti alifika eneo la tukio akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama na kukuta Watoto 96 wapo kituoni hapo na kumuelekeza Sheikh wa Msikiti kusitisha huduma hiyo na kuagiza Watoto hao warejeshwe kwenye famili zao.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, DC Magoti amesema:

Lengo kubwa la Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuwa kila shughuli lazima tushirikishe viongozi wa dini, mimi nikiwa Msaidizi wake ngazi ya Wilaya, tulipopata taarifa kuhusu uwepo wa mazingira haya ambayo sio mazuri tukaona tuwatoe ili ufanyike utaratibu mzuri ili kuboresha mazingira.

Ikiwa Serikali inaweza kujenga miundombinu ya gharama kubwa kwa nini tushindwe kujenga hosteli nzuri na ya kisasa kwa faida ya Watoto wetu!

Baada ya kutoa maelekezo ya Watoto kuondolewa pale, kesho yake nilirejea eneo la tukio Usiku wa Saa Nne nikakuta utekelezaji umefanyika wa kuwaondoa Watoto hao.

Mimi naheshimu sana dini, natambua ndio inaleta upendo, mshikamano na viongozi wa dini mnafanya kazi kubwa sana.

Kwa leo kwa kuanzia, nimeleta mifuko 150 ya saruji kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa hosteli.

Wale wanaotaka kutuchonganisha tuwakemee na kuwataka nao waje kuchangia ili Ujenzi uishe mapema watoto waendelee na Masomo.

Mimi kama mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama ni jukumu langu kuangalia usalama wa Watu wote wa Kisarawe.

Niwaombe, lengo lenu ni zuri lakini twendeni kwa haraka ili tujenge hosteli ya kisasa na itakayokuwa na mazingira bora.

Pia soma: Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi
Haka kajamaa kenye kibiongo kalikurupuka kakagusa dini ya wanaotawala kwa sasa!
Kaliposhituka, wenye dini Yao, wameenda kulia Lia kwa mtume wao pale magogoni, kakaona Bora kafanye juu chini, kapereke chochote msikitini, ndio hiyo cement,
ukikauliza, pesa ya kununulia hiyo cement imetoka kwenye bajeti ipi ya wilaya! Ilipangwa lini? Je huko ilipochukuliwa, nakisi italipwaje?
Upuuzi mtupu
 
Ndio uongozi huo kiongozi ana wadau wengi ni kuwaambia wadau na kuendesha harambe kwa kushirikisha jamii husika.
Na sio mambo ya amri amri tu unatatua changamoto baada ya kusikia changamoto zao.
Mazingira yakiwa magumu kiongozi unayafanya yawe rahisi.
 
Hata mzee mstaafu Mangula anamjua vizuri!
Ila jamani haya maisha sijui kama malaika wangekuwa wanatuandikia Obituary tukifa ili zisomwe hadharani watoto na ndugu zetu wangeficha wapi sura zao!
Alivyo mzee wa mikakati mikali siku ya utambulisho huko kisarawe kaonyesha familia ya mke tu yake kaificha!
 
Nadhani walianza muda mrefu, wamesoma kwa shida mpaka Magoti alipowaibua.
Mmh sio kweli neenda votuo vingi vya dini ya kiislamu viko hivo ata ukiweka ma bweni watoto wengi watapendelea kulala mskitini.......ni kutojua utamaduni wa dini ya kiislamu na mila zao ndo linalo msumbua magoti, watu wazima wanaacha majumba yao na kulala mskitini sembuse hao watoto wa madrasa.
 
Safi sana, Waislam mshindwe wenyewe sasa.

Mfanye mabweni ya kisasa na muweke majiko ya maana na wapishi, siyo mnawaweka wanafunzi kijinga jinga.
 
Mmh sio kweli neenda votuo vingi vya dini ya kiislamu viko hivo ata ukiweka ma bweni watoto wengi watapendelea kulala mskitini.......ni kutojua utamaduni wa dini ya kiislamu na mila zao ndo linalo msumbua magoti, watu wazima wanaacha majumba yao na kulala mskitini sembuse hao watoto wa madrasa.
Kwahiyo hayo mazingira magumu yanawekwa kwa makusudi?
Malazi duni, watoto wa miaka 3 hadi 8 kujipikia na kulala mahala pabovu na kutoenda shule??

Na kama uliangalia hata yule sheikh alikiri kua amefanya kosa, na walikua na mipango ya kuboresha maana walishanunua matofali, walishafanya upembuzi yakinifu juu ya hilo bweni.
 
Kwahiyo hayo mazingira magumu yanawekwa kwa makusudi?
Malazi duni, watoto wa miaka 3 hadi 8 kujipikia na kulala mahala pabovu na kutoenda shule??

Na kama uliangalia hata yule sheikh alikiri kua amefanya kosa, na walikua na mipango ya kuboresha maana walishanunua matofali, walishafanya upembuzi yakinifu juu ya hilo bweni.
Kwani DC awe na huruma ya watoto wakiislamu kuliko wazazi wao wenyewe, aiche unafiki hapa k.koo kuna watoto zaidi ya 1000, hawana pa kuishi na pa kula....kwanini asikisanye hao kwanza.
 
Itakuwa wazee wenye busara wamemuweka chini wakamchana live ... Kuna watu wa kuwachezea unavyotaka lakini sio imani ya kiislam .. DC utafanye ziara za kushtukiza misikitini usiku wa manane
 
Kwani DC awe na huruma ya watoto wakiislamu kuliko wazazi wao wenyewe, aiche unafiki hapa k.koo kuna watoto zaidi ya 1000, hawana pa kuishi na pa kula....kwanini asikisanye hao kwanza.
Sasa huyo ni Dc wa huko kariakoo??

Ishu sio huruma ni je haki za mtoto zimefuatwa?
Mzazi yuko Tanga huko anajua hata mtoto wake ananala wapi?

Kila kitu mkiendelea kukiweka kwenye mlengo wa kidini, mtaishia kusema mnaonewa kila siku.
 
PAMOJA NA YOTE HAYA, LAKINI NI BUDI VITUO HIVI VIKAJULIKANA NA BAKWATA, NA HATA WAALIMU WAKE WAKAWA WANATAMBULIKA NA BAKWATA!
 
Back
Top Bottom