Pre GE2025 DC wa Longido aliyesema alihusika kutengeneza mazingira ya Madiwani kushinda 2020 atenguliwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Ametenguliwa kwa kuwa amesema ukweli mchungu sana unaochoma moyoni.


Huu ni Ukweli mchungu sana.

CCM KUENDELEA KUBAKI MADARAKANI AU KUSHINDA KWENYE UCHAGUZI HAITEGEMEI KUPIGIWA KURA NA MTU YOYOTE YULE KATIKA UCHAGUZI WA SIASA HAPA NCHINI TANZANIA.

Aidha, katika Uchunguzi uliofanyika kwa kificho ulibaini kwamba wale Watu waliohusika kwenye Usimamizi wa Uchaguzi wa Siasa hapa Tanzania Mwaka 2020 walikuwa ni aidha Mawakala wa Siri wa TISS au Maaskari Polisi. Siku chache kabla ya Uchaguzi huo Watu hao Walikusanywa kwenye Makambi kwa ajili ya kupewa Mafunzo Maalumu ya Kuhujumu Uchaguzi huo ili kuipa Ushindi CCM.
Ma-DSO wote waliokuwepo walikabidhiwa jukumu naalym la kuratibu na Kusimamia Mpango huo.

Kwa wale Watu wengine waliohudhuria mapema kwenye Vituo vya Kupiga Kura siku ya Uchaguzi Mwaka huo wa 2020 nafikiri mtakuwa mashuhuda wazuri kwamba mliwakuta Vijana waliobeba mabegi kwenye vituo vya kupigia Kura, hao ndio watu wenyewe ninaowazungumzia hapa.
 
Hapo ndio atajua nguvu ya cheo na wali nyumbani mbele ya Mke
Ni mwendo wa matukio tu 😄
Tatizo hawajui majukumu yao, bali kuropoka chochote tu
 
Hivi hakunaga msamaha
Hata kama mmetengua uteuzi wake lakini Marco Ng’umbi kasema ukweli mchungu.

Kauthibitishia Umma mambo matatu-;

1. Kathibitisha kuwa Maccm hatakubaliki,

2. Kathibitisha kuwa maccm huwa yanaiba Kura,

3. Kathibitisha kuwa Serikali huwa inateka watu na kuwatupa kwenye mapori.
 
Huyu ndio Samia wa 4R, mapumbavu ya Jiwe yanajisahau, yakiibuka mama anapiga kichwa
 
Kwa muda huu DC alietumbuliwa yuko zake anatengeneza mazingira na mke wake, kama alivotengeneza mazingira 2020
 
Kwa kifupi uongozi uliopo unatakiwa ukanushe taarifa hii,sio kumtumbua na kunyamaza.
Huyu DC chadema wanamhitaji kama ccm haimtaki
 
Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu,kanusheni taarifa ya DC au muikubali ili tusonge mbele. Ila watanganyika ushahidi umepatikana.
 
Atatengua wangapi kama kila mmoja atatoka hadharani na kuanza kuuongea ukweli? Ukweli haufichwi kwa kutishia kuwaondoa watu kwenye nafasi alizowapa.
Wako walioandika na vitabu baada yakutoka madarakani.Ukweli nisawa na haja,utavumilia ila huwezi kutulia hadi uitoe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…