Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,051
- 461
kamwe sijekuchelewa,kwako mama ninasema,
miezi tisa kulelewa,na wewe tumboni mama,
maneno ulirushiwa,mbele na ulitizama,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Wengi waliyasema,ni utazaa jambazi,
Jibu kwao hukusema,maneno yako ni tenzi,
Ulienda kwa neema,ukayaacha mapenzi,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Najua mama ulipo,umelala kwa salama,
Muumba daima na yupo,zake mbawa dhahama,
watoto wako na wapo,kukukosa we daima,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
najua nawahi mama,kukwambia siku yako,
kumbuka we ulisema,kuwahi chelewa mwiko,
ulienda kwa heshima,zote mpaka na uliko,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
sina zaidi kukupa,mpaka siku tuwe wote,
ila kwako ulinipa,mapenzi wakati wote,
miezi tisa ulinipa,tumboni wakati wote,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
maua nimeyaweka,tayari siku ifike,
ulipo kuyatandika,harufu kwako ifike,
siku pia nitafika,mungu na anialike,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Nakumbuka lipotoka,chozi lilitiririka,
miaka kupukutika,kichwani nakukumbuka,
tabasamu nakumbuka,kabla haujatoka,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Chozi laanza nitoka,anifuta malaika,
hata yeye akumbuka,siku ulipong'atuka,
mafuta alikupaka,kwa heri hutafufuka,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
miezi tisa kulelewa,na wewe tumboni mama,
maneno ulirushiwa,mbele na ulitizama,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Wengi waliyasema,ni utazaa jambazi,
Jibu kwao hukusema,maneno yako ni tenzi,
Ulienda kwa neema,ukayaacha mapenzi,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Najua mama ulipo,umelala kwa salama,
Muumba daima na yupo,zake mbawa dhahama,
watoto wako na wapo,kukukosa we daima,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
najua nawahi mama,kukwambia siku yako,
kumbuka we ulisema,kuwahi chelewa mwiko,
ulienda kwa heshima,zote mpaka na uliko,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
sina zaidi kukupa,mpaka siku tuwe wote,
ila kwako ulinipa,mapenzi wakati wote,
miezi tisa ulinipa,tumboni wakati wote,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
maua nimeyaweka,tayari siku ifike,
ulipo kuyatandika,harufu kwako ifike,
siku pia nitafika,mungu na anialike,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Nakumbuka lipotoka,chozi lilitiririka,
miaka kupukutika,kichwani nakukumbuka,
tabasamu nakumbuka,kabla haujatoka,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,
Chozi laanza nitoka,anifuta malaika,
hata yeye akumbuka,siku ulipong'atuka,
mafuta alikupaka,kwa heri hutafufuka,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,