Degree ni karatasi tu, haisaidii lolote kiuchumi?

Degree ni karatasi tu, haisaidii lolote kiuchumi?

Only in Tanzania but in so many other countries around the World especially the Western countries degree is very important to open up so many doors for you.
Nakubaliana na wewe mitaala yetu ya elimu ndio tatizo.
 
Hizo kazi za social media zina malipo kuliko hata hizo kazi nyingine , sasa kwann waumie kusoma saana

Inamsaidia nini mwanachi ambae atahitaji kutibiwa kama kijana badala asomee Uganga
Huyo wa aliyeko kwenye tiktok na kupata hela au YouTube na kupata hela akifika miaka 20 ijayo ataweza kuisaidia jamii kwa lipi?

Hapo nazungumzia hao ambao wanategemewa kuwa wataalamu baadae ila wame drop shuleni kisa anauza bidhaa kwenye Amazon

Mkuu angalia ya mbele hao hao watakuja kutuhitaji sisi maana tiktok na YouTube haitawasaidia wananchi wao

Huyo unasema anatengeneza hela hiyo ni faida yake bali jamii haisaidii lolote na ni upotevu wa rasilimali watu

Naongelea kwa ujumla na uhalisia wa maisha yatakavyokuwa baadae
Ila kila mmoja anavyoona na wewe unavyoona ndio hivyo
 
Shukran Sana mkuu unaona mbali sana

Natamani kama waafrika tutaliona hili na kuwaza tofauti
Tuna kila kitu kuwazidi na neema zote ziko kwetu
Kuna nchi zina hela ila hata nyanya hawajui inaotaje

Hakika tusifurahie kuja kwao kununua Ndizi kwa matani huu ndio mwanzo
Watajazana mpaka wengine watanunua na ardhi kwenye serikali mbovu za Africa

Mungu Ibariki Tanzania [emoji1241]
 
Japo maisha siyo kutesa Kila siku ila pesa ndiyo Kila kitu...

Ngoja waje kutia miongozo...
 
Ndg.Asubuhi nimesikiliza mjadala wa saa 2 katika ile platform ya club house ya midset transformation. katika mjadala huo watu watatu wenye degree zaidi ya nne na mmoja mwenye PHD kwa kudai kuwa kupata degree is just a paper na kwamba katika maisha yao hazijawahi kuwasaidia lolote.

Wamekwenda mbali zaidi kuwa watanzania wengi wanaendesha maisha nje ya degree walizopata.

Wamepata wakati mgumu baada ya members kuwataka watoe ufafanuzi maana humo wapo vijana wanaosikiliza na wanajipanga kuelekea vyuoni lakini wamesisitriza tena kuwa mtu anayetegemea kutumia degree imsaidie anachemka.

Yamesemwa mengi lakini binafsi nikaona si vibaya nikaleta humu kisima cha great thinker tuidadavue maana hawa motivation speakers pasua kichwa
Shida namba moja hapa tanzania kwenye sekta ya elimu ni kwamba hatuwafunzi wasomi wetu lengo rasmi la elimu bali tunawapa tamaa ya kupata fedha kiwepesi kwa kupitia elimu na ajira rasmi.Jamii huwaaminisha vijana wetu tangu utoto wao, endapo watasoma watakuwa na ajira yenye tija ndio maana si ajabu kuona kijana akiulizia kozi gani inalipa akaisomee chuoni. Hivyo chachu ya wasomi wengi(si wote) ya kusoma kwa bidii msingi wake ni fedha kupitia ajira nzuri ili asaidie familia yake, wakati malengo halali ya elimu ni kutoa huduma kwa jamii(kila taaluma kwa nafasi yake), kutawala mazingira yetu,kuifanya dunia kuwa mahali bora pakuishi sisi na vizazi vijavyo(making better Earth) na kuamisha ujuzi kwa vizazi( Transfer knowledge through generations) na hayo mambo ya fedha kwa mtu huja kama zawadi ya utoaji huduma kwa jamii. Hili kosa ndo hupelekea wasomi wapenda rushwa maofisini,magraduate wasiojua fani zao vyema, kukosa utu na kunyanyasa watu ktk ofisi za umma, uzalendo mdogo kwa taifa, maendeleo madogo ya kitaaluma na technolojia, degree kuonekana karatasi tu na mengine mengi..
Yaaani unakuta mtu yupo kazini ila anaenda kuongeza elimu ili apande cheo tu au ngazi ya mshahara pekee na sio ongezeko la utoaji bora wa huduma kwa jamii na taifa lake. Pia leo huko mitaani kipimo cha usomi wa mtu kinapimwa kwa namna alivyofanikiwa kiuchumi yaani ajabu sana ...hii ndo husababisha wasomi waliokosa ajira rasmi kudharaulika/ kudharau elimu zao na kuita karatasi tu kwa kuwa hawana matumizi nazo nje na lengo la fedha za ajira rasmi.
 
Wataalamu wa masuala ya uchumi wanasema mpaka kufika mwaka 2039 Africa itategemewa kwa mambo mengi sana kuanzia Elimu na maisha mengi tu kama chakula na hata maji

Tukianza na elimu kama mnavyoona wale watoto wa kizungu waliokuwa wanategemewa kuwa engineers na doctors Leo wengi wamejikita kwenye social media na kuwa actors, singers, comedians na ubunifu usiokuwa na tija kwa jamii bali wafuasi milioni

Hapo kama tutawekeza kwenye elimu wao ndio watatuhitaji zaidi kuwa doctors na kazi nyingi tu

Rejea wameanza taratibu kuchukua nurses toka Kenya kuja UK

Waarabu pia walishtuliwa zamani wakafikiri watauza mafuta kwa wingi maisha yao yote ila mambo yatakuwa magumu sana kwani Solar zitatawala na magari ya umeme yatakuwa mengi na kuyatupa yanayotumia mafuta

Tuna wakati mzuri sana wa kujipanga na vijana kusoma sana kwa vitendo sio kukariri

Msiwasikilize hao kwani walienda kukariri sio kusoma

acha kujidanganya ndugu
 
acha kujidanganya ndugu

Huo ndio ukweli ila kwa sisi tunaangalia kesho tunakula nini
Ya miaka 40 au 50 ijayo hayatuhusu kwani hatuna la kuvumbua kwa hiyo tunasubiri watutafunie kila kitu

Kubali au kataa utakuwa mtumwa wao tu kama hutabadili mentality hii
 
Shida namba moja hapa tanzania kwenye sekta ya elimu ni kwamba hatuwafunzi wasomi wetu lengo rasmi la elimu bali tunawapa tamaa ya kupata fedha kiwepesi kwa kupitia elimu na ajira rasmi.Jamii huwaaminisha vijana wetu tangu utoto wao, endapo watasoma watakuwa na ajira yenye tija ndio maana si ajabu kuona kijana akiulizia kozi gani inalipa akaisomee chuoni. Hivyo chachu ya wasomi wengi(si wote) ya kusoma kwa bidii msingi wake ni fedha kupitia ajira nzuri ili asaidie familia yake, wakati malengo halali ya elimu ni kutoa huduma kwa jamii(kila taaluma kwa nafasi yake), kutawala mazingira yetu,kuifanya dunia kuwa mahali bora pakuishi sisi na vizazi vijavyo(making better Earth) na kuamisha ujuzi kwa vizazi( Transfer knowledge through generations) na hayo mambo ya fedha kwa mtu huja kama zawadi ya utoaji huduma kwa jamii. Hili kosa ndo hupelekea wasomi wapenda rushwa maofisini,magraduate wasiojua fani zao vyema, kukosa utu na kunyanyasa watu ktk ofisi za umma, uzalendo mdogo kwa taifa, maendeleo madogo ya kitaaluma na technolojia, degree kuonekana karatasi tu na mengine mengi..
Yaaani unakuta mtu yupo kazini ila anaenda kuongeza elimu ili apande cheo tu au ngazi ya mshahara pekee na sio ongezeko la utoaji bora wa huduma kwa jamii na taifa lake. Pia leo huko mitaani kipimo cha usomi wa mtu kinapimwa kwa namna alivyofanikiwa kiuchumi yaani ajabu sana ...hii ndo husababisha wasomi waliokosa ajira rasmi kudharaulika/ kudharau elimu zao na kuita karatasi tu kwa kuwa hawana matumizi nazo nje na lengo la fedha za ajira rasmi.
Umenena vyema
 
Degree ni muhimu sababu mtu akijuwa umesoma ndio atakapoanzia kukusaidia au msomi mwenyewe ataangalia opportunity kwenye field yake
Ubaya tunaona hvyo wengi tumesoma fata mkumbo au tulichaguliwa na wazazi sio kitu tulipenda toka udogoni au moyoni
 
Wako sahihi PhD ya uchumi inashindwa kutafuta vyanzo vya mapato inakimbilia mihamala ya simu
 
Wataalamu wa masuala ya uchumi wanasema mpaka kufika mwaka 2039 Africa itategemewa kwa mambo mengi sana kuanzia Elimu na maisha mengi tu kama chakula na hata maji

Tukianza na elimu kama mnavyoona wale watoto wa kizungu waliokuwa wanategemewa kuwa engineers na doctors Leo wengi wamejikita kwenye social media na kuwa actors, singers, comedians na ubunifu usiokuwa na tija kwa jamii bali wafuasi milioni

Hapo kama tutawekeza kwenye elimu wao ndio watatuhitaji zaidi kuwa doctors na kazi nyingi tu

Rejea wameanza taratibu kuchukua nurses toka Kenya kuja UK

Waarabu pia walishtuliwa zamani wakafikiri watauza mafuta kwa wingi maisha yao yote ila mambo yatakuwa magumu sana kwani Solar zitatawala na magari ya umeme yatakuwa mengi na kuyatupa yanayotumia mafuta

Tuna wakati mzuri sana wa kujipanga na vijana kusoma sana kwa vitendo sio kukariri

Msiwasikilize hao kwani walienda kukariri sio kusoma
Conspiracy Theories zinakuharibu! Degree hizi za UDSM ndio ziwe tegemeo la baadae, Yena kama kuna sehemu Duniani ambayo Elimu imeshindwa kuonesha faida yake basi ni Africa. Angalia hadi leo hii hali yetu kulingana na Idadi ya wasomi tulionao.
 
Tatizo ni umaskini, mapinduzi ya viwanda waliyopitia wenzetu miaka 300 iliyopita ndio yali solve problems walizokuwa nazo ambazo ndizo tunazo sisi kwa sasa.
Democracy
Uchumi
 
Back
Top Bottom