Demokrasia haiwafai watu aina ya Mdude Nyagali

Demokrasia haiwafai watu aina ya Mdude Nyagali

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
DEMOKRASIA HAIWAFAI WATU AINA YA MDUDE CHADEMA

Kwa Mkono wa, Robert Heriel

Mwaka juzi niliandika makala moja iliyokuwa ikimuonya na kumrekebisha Mwanaharakati na mwana chama wa Chadema, Ndugu Mdude Chadema kuwa ukosoaji wake haufai kwani anatumia lugha chafu zilizochanganyika na matusi.

Napenda wakosoaji, warekebishaji, Wanaharakati, ambao Wana misimamo mikali na wenye lugha ngumu lakini zisizo chafu wala matusi.

Mdude Chadema yakupasa ujirekebishe tena Kwa sehemu kubwa.

Kama ulivyozoea kukosoa basi Leo hii natumia nafasi hii kukukosoa kuhusu ukosoaji wako, ikiwa hii ni mara ya pili tangu nilipokukosoa mwaka 2019.

Tumia Lugha Kali Kama za wenzako kina Malisa, Maria Sarungi, Fatma Karume, miongoni mwa wengine.

Usije sema wewe u-unique wako ni kutumia lugha chafu zenye matusi. Huo ni Upumbavu.

Niliwahi andika kuwa Demokrasia haiwafai watu Masikini na Wapumbavu.

Wapumbavu wao huitumia demokrasia Kama kichaka cha kutukana wengine, kuwadhalilisha, kuwavua nguo Kwa matusi ya nguoni kabisa.

Watu dizaini ya Mdude Chadema huweza kuvumilika Kwa Watawala wenye dharau, wanaowapuuza, na wasiojali watu wapumbavu.

Lakini Kwa Watawala wasioweza kuvumilia, watu mithili ya Mdude huweza kujikuta katika taabu, dhahama na shurba isiyoelezeka.

Mdude Chadema Kwa vile hawezi kujizuia mipaka yake ya kuongea ni hatari ikiwa atakutana na mtawala asiyejua naye kujizuia mipaka yake ya mamlaka.

Hii ni kusema,
Mdude atatumia Uhuru wake wa kuongea vibaya.
Na mtawala naye atatumia Madaraka yake vibaya.

Hata hivyo,
Mdude Chadema anaweza akawa jasiri Jambo ambalo ni zuri, lakini kuwa jasiri kipumbavu ni Jambo baya.

Uwezo mzuri wa Mdude wa kuonyesha ujasiri wake ingependeza Kama angeutumia Kwa njia nzuri ya kukosoa kama mtu mwenye hekima.

Vita ya Mdude kipindi cha nyuma dhidi ya utawala wa JPM ilikuwa vita nzuri lakini iliyoharibiwa na wachezaji, wote Mdude na JPM.

Mdude alikuwa na hoja, lakini alikuwa akizitoa Kwa njia chafu na matusi Jambo ambalo halikuwa zuri na nilimtahadharisha.

Wembe alioutumia Mdude awamu ya JPM unafahamika, ulikuwa ni wembe wenye lugha chafu, matusi na lugha zenye ukakasi. Ndio maana mpaka naandika hapa ni kutokana na kuielewa kauli yake Kwa namna hiyo, nikikusudia kumtahadharisha na kumuomba atumie mbinu nyingine.

Kwa maana Kama atatumia wembe ule ule basi mtawala naye Hana budi kutumia shoka Kama alivyokuja akifanya JPM.

JPM naye hakuona ulazima wa kutumia busara Kwa kijana atumiaye upumbavu kumshambulia. Matokeo yake tunayajua.

Mdude na wenzako WA namna yako.
Lazima uelewe kuwa kanuni ya mapambano au vita hutumia Mirror principles ambapo unashambuliwa kadiri unavyokuja.

Ukija unacheka utashumbuliwa unacheka, ukija unapiga mayowe utashumbuliwa wakiwa wanapiga mayowe.

Kanuni za kioo ambazo huzingatia law isemayo input is equal to output ndio msingi WA mapambano.
Wahenga walisema; Dawa ya Moto ni Moto.

Mdude Chadema sitaki kuamini kuwa wewe ni mpumbavu ambaye Demokrasia huiwezi.

Tafadhali, fanya Sub katika mapambano yako, ingiza akili na hekima alafu mtoe upumbavu akae bench Kwanza.

Siku zote ukitumia upumbavu basi matokeo yatakayo kupata yatafanana kiwango cha upumbavu uliowekeza. Halikadhalika na ukitumia akili, hekima na maarifa.

Pambano liendelee lakini tahadhari zizingatiwe, sheria za mchezo zisipuuzwe.

Linda nchi yako, penda watu wako.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
 
Kuna yule wa uvccm aliyetaka wapinzani kuuwawa. Yule mbunge mama mwingine aliyesemea bungeni kutaka mbunge wa upinzani auawe.

Vipi yule aliyewauwa kina Azory Mawazo Ben. Aliyewajeruhi kina Lissu, kudhulumu watu, nk.

Kuna ushauri wowote mliwahi kuwapa au ni machozi mengine ya mamba tu?
 
Mdude hajakosea

Na mimi nasema hivi, kama Samia atafuata njia ileile ya kidikteta ya Magufuli, basi wembe uleule tuliotumia kumnyoa Magufuli tutamnyoa nao na yeye pia...

Kila mtu atatumia alichonacho

Mwenye mdomo atumie mdomo
Mwenye pesa atumie pesa
Mwenye mamlaka atumie mamlaka
Mwenye uchawi atumie uchawi
Mwenye Mungu amtumie Mungu

Mbona yeye hajaenda mahakamani??

Hoja ipo nzuri Ila uwasilishwaji uzingatiwe.

Maana kila mmoja akisema atumie alichonacho basi mwenye nguvu ndiye atakayeshinda.

Ukisema Waende mahakamani, nao watauliza mbona wewe/yeye hakuenda mahakamani?
 
Huyu Samia ndo alitoa kauli kuhusu Lissu kupigwa risasi kuwa "askari wao huwa hawakosei"

Juzi hapa naye anatoa kauli kuwa “Rais hakosei"

Amewahi kusema kuwa hata wasipopigiwa kura na wananchi watashinda tu

Kisha akamaliza kwa kutoa kauli ya kuvunja katiba kuwa Vyama vifanye mikutano ya ndani tu

Sasa huyu mama ambaye naye ameonyesha kumbe ana elementi za kidikteta akichiwa si ataanza kuwa kama Magufuli?

Kuna haja wembe uliotumika kumnyoa Magufuli utumike huohuo kumnyoa na yeye, Yaana mapambano ya kupinga udhalimu wake non stop
 
Uzuri wa Mdude ni confidence aliyonayo, anaongea mawazo yake kwa uwazi na anatafuta platform sahihi.

Anatapotakiwa kujiweka sawa ni uwezo wa kujenga hoja kwa kutumia maneno ya busara. Akiwa na hivi viwili atakua kiongozi bora zaidi.
 
Huyu Samia ndo alitoa kauli kuhusu Lissu kupigwa risasi kuwa "askari wao huwa hawakosei"

Juzi hapa naye anatoa kauli kuwa “Rais hakosei"...
Wapi ametukana na kutumia lugha chafu??

Kuhusu kupigwa risasi Lisu, utekaji, mauaji ya kihole holela yote hayo tuliyapinga Kwa nguvu moja.

Ninachokisema hivi leo ni kuwa matokeo ya hayo hutokana na uvukaji wa mipaka baina ya wapambanaji.

Mmoja anatumia lugha mbaya na chafu(kavuka mipaka yake)
Mwingine anatumia Madaraka yake vibaya (kavuka mipaka yake) ili kumtuliza hasimu wake
 
Uzuri wa Mdude ni confidence aliyonayo, anaongea mawazo yake kwa uwazi na anatafuta platform sahihi.

Anatapotakiwa kujiweka sawa ni uwezo wa kujenga hoja kwa kutumia maneno ya busara. Akiwa na hivi viwili atakua kiongozi bora zaidi.

Hao ndiyo watakaoleta mafanikio kwenye mchakato huu.

Lugha kama za huyo mwamba ndiyo wanazozielewa vizuri.

CCM wamejikita kwenye kuwa brainwash kada hiyo ya watu wenye huo uthubutu wakijua ni tishio kwao.

Yale ya mambo ya wanyonge yote ni fix.
 
Hakuna matusi yoyote aliyotumia,mseme tu hamkuipenda lugha aliyotumia.

Ni kweli bado hajaongea lugha chafu wala hajatukana mtu.

Ila statement yake ya kusema wembe atakaoutumia ni ule ule alioutumia Kwa awamu iliyopita.

Na wembe huo ninaoufahamu ulijawa na matusi, lugha chafu zenye ukakasi, ndio sababu ya Mimi kumtahadharisha
 
Sasa Kama ndio mara yako ya Kwanza kusoma nyuzi zangu unafikiri nitakujibu vipi?

Wewe Kama hukuona nyuzi zangu hapa nafikiri siwezi kukujibu chochote.
Sijawahi kukuona ukikemea lugha za fujo za Bashe, Heri James, Magufuli na Makada mbalimbali wa CCM juu ya kuwapiga wapinzani
 
Sasa Kama ndio mara yako ya Kwanza kusoma nyuzi zangu unafikiri nitakujibu vipi?

Wewe Kama hukuona nyuzi zangu hapa nafikiri siwezi kukujibu chochote.
Kwa hali kama hizo busara ni kuweka rejea husika. Hayupo mwenye kusoma kila bandiko. Tutachapa kazi saa ngapi?
 
Back
Top Bottom