Demokrasia ni adui wa maendeleo

Demokrasia ni adui wa maendeleo

..kosa lingine la Gaddafi ni kufadhili ugaidi dhidi ya Western powers, na waasi katika nchi mbalimbali za Afrika.

..kwa nchi za Afrika Gaddafi alifadhili magaidi katika nchi kama Uganda, Siera Leone, na Liberia.

..Kenya, Malawi, Ghana, Senegal, ni nchi ambazo kwa muda mrefu zilikuwa katika makucha ya Madikteta.

..Kama utakumbuka Kenya ilipita katika mifumo ya kikatili sana wakati wa tawala za Mzee Kenyatta, na Mzee Moi.

..Kenya unayoiona sasa hivi ni nchi / jamii inayojitafuta kuelekea katika demokrasia ya kweli. Bado wana mambo mengi ya kuyaweka sawa ili wawe na mifumo ya kidemokrasia.

..Ghana nayo ilipita katika kipindi kibaya cha Udikteta na machafuko. Wameikubali demokrasia miaka ya 1990. Hata wao huwezi kusema kwamba wamefaulu vya kutosha.

..Naendelea kusisitiza kwamba Ethiopia, Somalia, Ghana, Malawi, Zambia, Msumbiji, na nchi nyingine nyingi za Afrika, zilishajaribu Udikteta, na zikafeli vibaya sana

..
Kwa hio miaka ya 90 hadi 2024 haitoshi kujipata? Miaka 34 hio, Una estimate miaka mingapi zaidi inahitajika? 100, 200, 1000 ama 10,000
 
Korea zote ziliendeshwa kidikteta. Moja ikawa tajiri nyingine bado. Hiyo iliyokuwa tajiri ikaamua kuwa na demokrasia. Sina mfumo ninaotaka, ninachotaka ni tukae chini na kutafuta mfumo utakaoweza kuteletea maendeleo.
Mwaka 1961 GDP Korea ya Kusini ilikuwa USD 2.42 Bilioni. GDP ya Tanganyika ilikuwa USD 2.65 Bilioni.

Mwaka 2023 GDP ya Korea ya Kusini ilifikia USD 1,818.43 Bilioni na ya Tanzania ilifikia USD 79.16 Bilioni.

Korea yake Kusini imekuwa ikiendeshwa kidemokrasia wakati Tanzania kiuhalisia (virtually) inaendeshwa kidikteta tangu tupate uhuru.

Ni fikra NYEPESI SANA kuchukulia demokrasia au udikteta kama kichocheo cha maendeleo. Kuna mambo (factors) nyingi sana zinazochangia maendeleo. Think again.
 
Mwaka 1961 GDP Korea ya Kusini ilikuwa USD 2.42 Bilioni. GDP ya Tanganyika ilikuwa USD 2.65 Bilioni.

Mwaka 2023 GDP ya Korea ya Kusini ilifikia USD 1,818.43 Bilioni na ya Tanzania ilifikia USD 79.16 Bilioni.

Korea yake Kusini imekuwa ikiendeshwa kidemokrasia wakati Tanzania kiuhalisia (virtually) inaendeshwa kidikteta tangu tupate uhuru.

Ni fikra NYEPESI SANA kuchukulia demokrasia au udikteta kama kichocheo cha maendeleo. Kuna mambo (factors) nyingi sana zinazochangia maendeleo. Think again.
Maendeleo yanasababushwa na matumizi sahii ya akili
 
Kwa hio miaka ya 90 hadi 2024 haitoshi kujipata? Miaka 34 hio, Una estimate miaka mingapi zaidi inahitajika? 100, 200, 1000 ama 10,000

..unachokishuhudia sasa hivi katika nchi mbalimbali kina afadhali kuliko nyakati za udikteta.

..Na usisahau kwamba Udikteta nao ulijaribiwa, au ulidumu ktk nchi za Afrika, toka miaka ya 60.

..tunachotakiwa kufanya Waafrika ni kuiboresha mifumo yetu ya kiutawala, na sio kuibomoa na kurudi kwenye tawala za kiimla.

..Kwa nchi kama Tanzania ni kweli tulipitisha sheria mwaka 1993 kuwa na mfumo wa vyama vingi. Lakini tangu kipindi hicho Ccm imekuwa ikifanya kila aina ya figisu kuhujumu mfumo huo. Kwa msingi huo, huwezi kudai kwamba demokrasia imefeli wakati kinachoendelea nchini ni hujuma,na figisu dhidi ya demokrasia.
 
Huko sio kuhifadhi ni kwenda kuficha hili wala sio jambo la ajabu kwa matajiri wezi.

China inaongoza kwa Banks bora duniani tajiri au mwanasiasa anaye enda kuficha pesa Singapore au Switzerland ni mwizi anayekwepa mifumo ya kibenki ya China.
Pia China wana surplus ya dolari. Inawabidi kuzipeleka nje kuwekeza.
 
..unachokishuhudia sasa hivi katika nchi mbalimbali kina afadhali kuliko nyakati za udikteta.

..Na usisahau kwamba Udikteta nao ulijaribiwa, au ulidumu ktk nchi za Afrika, toka miaka ya 60.

..tunachotakiwa kufanya Waafrika ni kuiboresha mifumo yetu ya kiutawala, na sio kuibomoa na kurudi kwenye tawala za kiimla.

..Kwa nchi kama Tanzania ni kweli tulipitisha sheria mwaka 1993 kuwa na mfumo wa vyama vingi. Lakini tangu kipindi hicho Ccm imekuwa ikifanya kila aina ya figisu kuhujumu mfumo huo. Kwa msingi huo, huwezi kudai kwamba demokrasia imefeli wakati kinachoendelea nchini ni hujuma,na figisu dhidi ya demokrasia.
Lakini majirani zetu wamefanikiwa kutoa CCM zao na still hakuna walichofanikiwa, Zambia, Kenya na wengineo.

Mtoa mada kaongea point moja muhimu sana Kukiwa na Mfalme fisadi inakua familia moja ila kukiwa na Demokrasia mafisadi kila sehemu.

Nchi zilizoendelea ni zile ambazo zimefanikiwa kukomesha rushwa na kuangalia Strength za Nchi na ku focus kwenye hizo strength.
 
Mwaka 1961 GDP Korea ya Kusini ilikuwa USD 2.42 Bilioni. GDP ya Tanganyika ilikuwa USD 2.65 Bilioni.

Mwaka 2023 GDP ya Korea ya Kusini ilifikia USD 1,818.43 Bilioni na ya Tanzania ilifikia USD 79.16 Bilioni.

Korea yake Kusini imekuwa ikiendeshwa kidemokrasia wakati Tanzania kiuhalisia (virtually) inaendeshwa kidikteta tangu tupate uhuru.

Ni fikra NYEPESI SANA kuchukulia demokrasia au udikteta kama kichocheo cha maendeleo. Kuna mambo (factors) nyingi sana zinazochangia maendeleo. Think again.
Umri WA demokrasia WA Korea kusini na Tanzania haina tofauti, Kwa kipindi cha muda mrefu Korea imeongozwa na military dictators, unajua kuwa Park Chung Hee alibadirisha katiba na kuwa rais w maisha, mwaka 1980 kulitokea maandamano ya kutaka demokrasia ambayo yaligharimu maisha ya watu zaidi ya 600, na vyombo vya ndani havikuwa vinaripoti taarifa sahihi.

Baada ya Mapinduzi ya kijeshi 1961, dikteta Park alichukua muelekeo tofauti WA kuendesha uchumi Kwa uelekeo WA export oriented economy huku wafanya biashara wakiwa wamewekewa kama kisu shingoni Kwa kulazimishwa kufuata mpango WA maendeleo WA serikali, vinginevyo serikali ya park itampa Mali zako mfanya biashara mwingine anayefanya vizuri.

Wakati huo Korea kusini ilikuwa inapokea massive support ya kifedha, kisoko na teknolojia toka Kwa USA, Japan, Germany na hata UK kwenye ship building, pia France kwenye nuclear plants

Wakati huo Tanzania ilichagua njia ambayo sio sahihi ya kutengeneza state monopolies enterprises ambazo hazikuwa na ufanisi wowote maana targets zilikuwa chini, njia za nyerere zilitenga wajasiliamali(domestic private sectors) kushika usukani WA maendeleo kiuchumi maana ujamaa hautaki matabaka

Na bahati mbaya hatukua na privilege kama za Korea Kusini toka Kwa nchi matajiri, 1961-1979 Korea kusini ilitengeneza misingi mizuri ya industrialization na uwekezaji ukaanza kutoa faida miaka 1980 hata baada ya Park kuuwawa.

Wakati huo Tanzania ikaingia kwenye kipindi kigumu Sana miaka ya 1980-ujamaa unaporomoka, china imeshabadilisha Sera zake, Na nchi ikageukia IMF na WB, Sera ambazo ziliua kabisa industrialization process nchini

Mpaka mwaka 1979 Korea kusini GDP ilifika $69 billions, wakati Tanzania ilikuwa $10, yaani zaidi ya mara 6.

Kati 1961-1993 udikteta Korea ulikuwa mkubwa kuliko Tanzania
 
Umri WA demokrasia WA Korea kusini na Tanzania haina tofauti, Kwa kipindi cha muda mrefu Korea imeongozwa na military dictators, unajua kuwa Park Chung Hee alibadirisha katiba na kuwa rais w maisha, mwaka 1980 kulitokea maandamano ya kutaka demokrasia ambayo yaligharimu maisha ya watu zaidi ya 600, na vyombo vya ndani havikuwa vinaripoti taarifa sahihi.

Baada ya Mapinduzi ya kijeshi 1961, dikteta Park alichukua muelekeo tofauti WA kuendesha uchumi Kwa uelekeo WA export oriented economy huku wafanya biashara wakiwa wamewekewa kama kisu shingoni Kwa kulazimishwa kufuata mpango WA maendeleo WA serikali, vinginevyo serikali ya park itampa Mali zako mfanya biashara mwingine anayefanya vizuri.

Wakati huo Korea kusini ilikuwa inapokea massive support ya kifedha, kisoko na teknolojia toka Kwa USA, Japan, Germany na hata UK kwenye ship building, pia France kwenye nuclear plants

Wakati huo Tanzania ilichagua njia ambayo sio sahihi ya kutengeneza state monopolies enterprises ambazo hazikuwa na ufanisi wowote maana targets zilikuwa chini, njia za nyerere zilitenga wajasiliamali(domestic private sectors) kushika usukani WA maendeleo kiuchumi maana ujamaa hautaki matabaka

Na bahati mbaya hatukua na privilege kama za Korea Kusini toka Kwa nchi matajiri, 1961-1979 Korea kusini ilitengeneza misingi mizuri ya industrialization na uwekezaji ukaanza kutoa faida miaka 1980 hata baada ya Park kuuwawa.

Wakati huo Tanzania ikaingia kwenye kipindi kigumu Sana miaka ya 1980-ujamaa unaporomoka, china imeshabadilisha Sera zake, Na nchi ikageukia IMF na WB, Sera ambazo ziliua kabisa industrialization process nchini

Mpaka mwaka 1979 Korea kusini GDP ilifika $69 billions, wakati Tanzania ilikuwa $10, yaani zaidi ya mara 6.

Kati 1961-1993 udikteta Korea ulikuwa mkubwa kuliko Tanzania

Mkuu kwenye avatar yako namuona fundi Park Chung Hee

Au nimeona vibaya?
 
Kwani mtoa mada kaja na solution kwamba tuongoze nchi zetu kwa mifumo wa nchi izo ulizotaja?

Hata mimi sijatoa solution. Nime highlight the fact kwamba Africa, kwa asilimia kubwa, Haina democracy na bado inaongoza kwa umaskini na maendeleo duni which defeats argument ya mleta uzi.
 
Lakini majirani zetu wamefanikiwa kutoa CCM zao na still hakuna walichofanikiwa, Zambia, Kenya na wengineo.

Mtoa mada kaongea point moja muhimu sana Kukiwa na Mfalme fisadi inakua familia moja ila kukiwa na Demokrasia mafisadi kila sehemu.

Nchi zilizoendelea ni zile ambazo zimefanikiwa kukomesha rushwa na kuangalia Strength za Nchi na ku focus kwenye hizo strength.

..Kenya ya sasa hivi ina ahueni kubwa sana kulinganisha na enzi za udikteta wa Mzee Kenyatta, au Mzee Moi.
 
..Kenya ya sasa hivi ina ahueni kubwa sana kulinganisha na enzi za udikteta wa Mzee Kenyatta, au Mzee Moi.
Raisi mmoja tu ndio utasema ana ahueni Uhuru, ila kina Kibaki, Huyu Ruto na wengi tu ni so and so
 
Hata hizo Nchi zilizoendelea kuna Deep state ambayo ipo juu ya sheria, Nchi kama Usa Raisi sio kiongozi mkubwa kabisa, kuna watu ambao raisi hawezi wagusa, Deep state = Disctator = Mfalme etc
Amerika zipo Strong institutions ambazo kwa mujibu wa Katiba yao haziwezi kuingiliwa na mtu yeyote hata angekuwa mkubwa kiasi gani !
Kila taasisi inafanya mambo yake kwa mujibu wa sheria sio kwa maelekezo kutoka kwa yeyote yule !!
 
DEMOKRASIA NA NCHI MASIKINI

Leo nakuja tena na hii mada.

Kwanza ijulikane kuwa hakuna nchi masikini imewahi endelea ikIwa chini ya demokrasia. Ukifutilia historia utaona kuwa hakuna nchi imewahi kutoka kwenye umaskini ikiwa inaongozwa kidemokrasia. Nchi zote zilizofanikiwa kutoka kwenye umaskini zimeongozwa kidikteta au kifalme.

Demokrasia ni anasa ya matajiri. Nchi masikini ikiingia kwenye demokrasia inajichimbia kaburi. Kwanza sababu ni kuwa ni gharama kubwa sana kuendesha nchi ya kidemokrasia. Nchi ya kidemokrasia ina walaji wengi sana.

Msomi mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya udikteta na demokrasia ni idadi ya watu unaotakiwa kuwaridhisha ili uendelee kushika madaraka. Idadi hiyo ni kubwa sana kwenye demokrasia. Wanaridhishwa kwa kupewa vyeo vingi vilivyoundwa kwa ajili yao. Na mzigo wote wa kuwalipa na kuwagharamia unaangukia nchi ambayo ni maskini.

Serikali ya kidemokrasia haiwezi kuja na sera za maendeleo ambazo zitawataka wananchi wafunge mikanda. Kuna wakati ili nchi iendelee ni lazima watu wafunge mikanda. Mfano nchi inaweza kusema hatutaagiza ngano ila tutahakikisha tunazalisha wenyewe kiasi cha kututosha. Kwenye nchi ya kifalme au kidikteta hilo linaweza kufanyika na baada ya muda nchi ikajitosheleza kwa ngano. Kwenye nchi ya kidemokrasia ngano ikiadimika wiki tu watu watangia barabarani na kuiangusha serikali. Wapinzani watapiga kelele za ajabu. Rais mwenye maono wa Liberia aliangushwa kwa namna hii na nchi ikachukuliwa na watu wazembe kama Samuel Doe. Ukisema tukuze textile industry yetu hivyo tulinde soko letu watu watazama barabarani na kukunyofoa madarakani. Waliotuletea demokrasia walijua vema wanachokifanya.

Kwenye nchi ya kidemokrasia ajenda kuu ya mtawala ni namna ya kubaki madarakani. Maamuzi yake yote yanazingatia kutimizwa kwa ajenda hii, hata kama yapo kinyume na maslahi ya nchi. Mfalme au dikteta anakuwa yupo imara madarakani. Anaweza kuwaza namna ya kukuza uchumi na hivyo kujiongezea kipato.

Nchi kama S Korea, Singapore, Malaysia na Shelisheli zimeweza kutoka kwenye umaskini kupitia madikteta.

Nchi kama UAE, KSA na Brunei zimeweza kufanya vizuri chini ya Ufame.

Bado hakuna nchi ya kidemokrasia iliyojitoa kwenye umaskini. Kila aina ya utawala ina mapungufu yake lakini demokrasia ni mfumo wa hovyo zaidi.

Habari kubwa kwenye nchi za kidemokrasia si za maendeleo, bali habari kuhusu michakato ya kidemokrasia.

DEMOKRASIA NA NCHI ZILIZOENDELEA

Nchi iliyoendelea na inayofuata demokrasia lazima itarudi kwenye umaskini. Nchi ya kidemokrasia iliyoendelea lazima itageuka ya kisocialist. Yaani wananchi wake watakuwa wanadai huduma kutoka kwa serikali kila leo hadi serikali itashindwa kuhudumia. Wananchi watataka afya bure. Mwanasiasa atakaye waahidi hilo wanamchagua. Kesho watadai elimu bure, kesho kutwa mishahara mikubwa, ruzuku wakulima nk nk. Nchi hizi zinajikuta zina matumizi makubwa kuliko mapato. Na wakati huo huo wanachi wakiwachagua wanasiasa wanaowaahidi kodi ndogo. Mwisho zinajikuta zina madeni wasiyoyaweza na deficit(nakisi) kwenye bajeti. Kaangalie nchi zinazodaiwa madeni ya kutisha, utakuta nchi za kidemokrasia zilizoendelea hasa ndizo zinaongoza kwa madeni, wala si nchi maskini zinazotangazwa kila leo. US deni lake ni asilimia 90 ya GDP yake. UK ni kama asilimia 250 wakati China ni kama 13%.

Hili la nchi kushindwa kumudu gharama limetokea kwa Argentina na nchi nyingi zilizoendelea zinaenda muelekeo huo.

Wafanyakazi wa nchi zilizoendelea na zinazofuata demokrasia wanaunda unions, na kudai mishahara mikubwa, benefits na haki nyingi. Matokeo yake gharama za uzalishaji zinakuwa kubwa na nchi kushindwa kushindana na bidhaa za kutoka mataifa mengine kama China. Matokeo yake viwanda vinafunga.

Gharama za kujenga miundombinu kwenye nchi za kidemokrasia ni kubwa sana. China imeziacha mbali sana nchi za magharibi kwenye suala la treni ziendazo kasi. Sababu kubwa ni mchakato mgumu na gharama kubwa za kufanya hivyo kwenye nchi za kidemokrasia. Kwenye nchi za kidemokrasia ukitaka kujenga kitu utakutana na red tapes za maana. Kila kikundi kitatoa sauti zao. Wenye ardhi watagoma reli isipite kwenye mapori yao au watadai fidia za ajabu na kukupeleka mahakamani juu.

Wengi wape lakini wakati mwingine wengi hukosea vibaya sana. Suala la Brexit ni mfano wa hili. Watu wengi walipiga kura UK ijiondoe EU. Leo hii baada ya athari kubwa za Brexit waingereza wengi wanajuta na kusema kuwa suala la Brexit halikuwa sawa. Mambo ya kitaalamu hayapaswi kuendeshwa kidemokrasia.

Demokrasia haifai kwa nchi maskini. Tukae chini tutafute mfumo mwingine.
Hivi ni vituko

Yaani wewe unadhani mwanadamu mmoja mwenye mapungufu kama mimi na wewe aje hapa duniani achape wanadamu wenzie viboko kuwalazimisha kufanya vitu anavyotaka yeye?

Demokrasia ni the best form of governing

Watu wazima kama wewe wawe huru kuamua watakacho hata kama kinawaumiza ni wao kwa utashi wao ilimradi hawajavunja sheria yeyote

Na uhuru wa kuvunja sheria kila mtu apewe ilimradi awe na uwezo kuvumilia consequences zake mahakamani

Kiongozi wa serikali asimamie sheria tu,maamuzi binafsi ni maamuzi binafsi

Udikteta ni ujinga wa kuungilia maamuzi binafsi ya watu binafsi na maisha yao

Wewe simamia serikali,watu binafsi waache

Kama kusimamia serikali kama chombo ni kazi inayokushinda mpaka ufatilie uhuru wa watu binafsi tayari huna akili na hutufai

Watu wazima wakiamua kua huru bila kuvunja sheria zilizopo achana nao,unaogopa nini uhuru wa watu?

Majitu yenye low IQ hua yanakimbilia udikteta kuwatawala wanadamu wengine,shame!
 
Hawajapata Viongozi wenye maono kama kwa mfano wangempata mtu kama JPM ungeona maajabu ndani ya muda mfupi sana 😳 !

Kwahiyo kumbe tatizo ni maono sio democracy? Democracy haiwezi toa Kiongozi mwenye maono?
 
Kwahiyo kumbe tatizo ni maono sio democracy? Democracy haiwezi toa Kiongozi mwenye maono?
Demokrasia itamuwekea vikwazo vingi asiweze kutekeleza maono yake. Ataishia kufanya business as usual.
 
Amerika zipo Strong institutions ambazo kwa mujibu wa Katiba yao haziwezi kuingiliwa na mtu yeyote hata angekuwa mkubwa kiasi gani !
Kila taasisi inafanya mambo yake kwa mujibu wa sheria sio kwa maelekezo kutoka kwa yeyote yule !!
Ni rahisi kubadili sheria na kufit hao mabwana wa kubwa na pia hao jamaa wanaweza vile vile wasifuate sheria.

Nakupa mifano.
1. Matajiri Usa/West hawalipi kodi, Kodi inalipwa na walalahoi

Hii article inaongelea west kiujumla

Ukisoma hapo unaona Mabilionea wanalipwa 0.5% ya tax haifiki hata asilimia 1 wakati kina kajamba nani wanalipishwa na ndio wanaendesha nchi.


Nyengine hii inakazania hivyo hivyo

2. Hao wanaotajawa kama Deepstate whether unataka ama hutaki wakiwa na jambo lao wanafanya mfano vita vya Iraq, kwa sheria zote za kimataifa na hata Marekani hivi vita havikua halali ila umesikia hata mtu mmoja kapelekwa mbele ya vyombo vya sheria?


3. sheria zinawekwa kufaidisha wao na sio wananchi etc.
Mfano mzuri sheria ya kumiliki silaha bila kibali inafaidisha zaidi makampuni ya kutengeneza silaha kuliko wananchi
Takribani, Asilimia 58 ya Marekani wanataka stricter gun laws, wakati asilimia 26 pekee ndio wanaridhika na Sheria ya sasa ya Silaha.


Kuna mambo mengi tu yapo hivyo hao ambao wapo juu ya sheria wanafanya wanavyotaka wao. Na sio mimi na conspiracy theories tu hadi watu wakubwa kama Trump ama Putin utawasikia mara kwa mara wakiongea kuhusu hizi deep States.
 
Back
Top Bottom