Demokrasia ni adui wa maendeleo

Demokrasia ni adui wa maendeleo

LKY alikuwa dikteta jambo ambalo hata yeye binafsi hakuwahi kupinga sifa hiyo na siku zote alikuwa proud kuonekana hivyo na hakuwahi kuipenda demokrasia katika maisha yake.

Nimeweka records sawa
LKY alikuwa dikteta katika mambo gani?
Ni mambo gani aliyoyafanya yaliyomtambulisha kama dikteta??
 
Huyo anus kama ulivyomtaja, hakuwa na sera maalum ya maendeleo. Leo anaongelea viwanda kesho ananunua ndege Cash, keshokutwa anafilisi mifuko ya hifadhi ya jamii na kuvuruga mfumo mzima wa ajira serikalini na sekta binafsi. Alikuwa Anus kweli kweli.

On a separate note, Afrika kusini ipo bara la Afrika lakini kimaendeleo inachuana na India, Singapore, Vietnam na baadhi ya nchi za Europe. Mfano Sekta ya elimu, ukitaja vyuo vikuu 10 Bora Afrika, vyuo 7 kati ya 10 vinatoka Afrika kusini na vyuo hivyo vinashika nafasi nzuri kwenye global rank vyuo 3 vilivyobaki ni vipo Egypt. Kwa ufupi hata Tanzania ingeshindanishwa na Johannesburg pekee Bado tungefunikwa.
Mijitu mivivu na mijizi sikuzote hulaumu...
 
Kwahiyo Wizi wa kura ndio mfumo mzuri kwa Nchi?!
Nyerere alitutawala kwa mfumo wa Authoritarian Maendeleo yalikiwepo?
 
Ukiangalia Historia madikteta wengi wamekuwa wanaingia madarakani kwa mapinduzi ,vita, kama falme, kupitia vyama vya kidikteta na wachache kama Hitler huwa wanachaguliwa kabisa kama wanademokrasia katika mifumo ya kidemokrasia kabisa halafu wanageuka kuwa madikteta wakiwa madarakani. Nyie nafikiri mchague hiyo ya mwisho ambayo ni ya bahati nasibu, tafuteni mtu mnayeoona anafaa kuwa dictator mzuri kutoka katika vyama halafu muhakikishe mnampigia kura na anashinda uchaguzi.

Ni mwendawazimu tu ndiye anayeamini Tanzania haipaswi kuwa na demokrasia, mimi sio mwendawazimu.
Ili kufahamu kama ni demokrasia au udikteta ndio unaohitajika Tanzania tutazame demokrasia tuliyonayo. Utagundua kwamba misingi ya demokrasia ambayo inahusisha chaguzi kila baada ya miaka mitano ipo lakini misingi mingine ya demokrasia haipo. Misingi hii mingine ni kama uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa maoni kuhusu maswala ya nchi kutoka Kwa wananchi, uhuru wa fikra na hata uwepo wa upinzani kama afya kwenye demokrasia. Chama tawala kina wanyima wananchi haki za msingi ambazo ni muhimu kwenye demokrasia yoyote. Elewa kwamba demokrasia iliyopo Tanzania ni "Illiberal democracy" , ambayo haina tofauti sana na udikteta. Ila nina kubaliana na wewe, udikteta unahitaji uhakika wa Rais anayegombea na serikali yake. Jambo hili limewashinda wengi na benovelance kwenye nafasi ya authority ni Jambo ambalo haliendani na ubinadamu wa kawaida. Kama demokrasia itaendelea kudumu, misingi yote inatakiwa kitiliwa maanani na kutekelezwa Kwa manufaa ya wananchi.
 
Kule kutajwa tu kuwa ni Nchi zinazofuata Utawala wa kidemokrasia hata kama haki za kidemokrasia hazifuatwi tayari zimo kwenye matatizo kama alivyofafanua mleta hii mada !!

Viongizi wa Africa,wakiapishwa hawana tena Cha kuwaza zaidi ya uchaguzi ujao, ayo maendeleo unayoyasema kwa mlolongo huo utayapataje?na ilo ni zao la kulazimisha mifumo isiyoendana na sisi katika nchi zetu kama iyo democrasia. Mtoa mada yupo sawa

Congo Brazzaville, Cameroon, Lesotho, Eswatini, Sudan, Uganda etc zina maendeleo gani ilhali hazina democracy?
 
LKY alikuwa dikteta katika mambo gani?
Ni mambo gani aliyoyafanya yaliyomtambulisha kama dikteta??
Alifunga wapinzani wake kisiasa,zuia maandamano ya kisiasa, alizuia harakati zote za kisiasa zilizokuwa kinyume na mtazamo wake na wa chama chake.
 
Kwa maana hiyo hoja yako unaona ni bora tubadili Katiba na Sheria zetu ili turudi mahameni siyo (chama kimoja kushika hatamu za uongozi)
Swali; toka mwaka 1961 hadi 1992 (30 yrs) wakati tunabadili katiba yetu ni maendelea gani chanya yalitokea ambayo unaweza kuyatumia kama vielelezo ili kujenga hoja yako ipate nguvu.
 
Watu wanaiba mali za Umma wanafanya kila aina ya Ubadhirifu lakini wakipelekwa Mahakamani eti kwa sababu ya Demokrasia na Utawala wa Sheria wanashinda kesi kwa kutumia mali hizo hizo walizozikwapua. !

Watu wanavurunda sehemu zao za Kazi kwa kufanya kila aina ya madudu lakini Kiongozi anashindwa kumuwajibisha kwa sababu atakuwa amefanya Udikiteta 🤣😳

Mwamba alijaribu jaribu kidogo tu na mambo yalishaanza kukaa kwenye msitari 😅🙌👍

Watu wanatumbuliwa juu kwa juu hata huko mikutanoni 😳
Hakuna mchezo !
Tena yeye alikuwa na afadhali lakini huko China Korea Japan Vietnam huko huwa wanakula kitanzi tu !
Tanzania hakuna demokrasia sababu msingi wa demokrasia ni kuwepo kwa uchaguzi huru, bunge na huru mahakama Mfano nchi za demokrasia Rais akiwa nje ya madaraka anaweza shtakiwa na kufungwa
 
Msomi mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya udikteta na demokrasia ni idadi ya watu unaotakiwa kuwaridhisha ili uendelee kushika madaraka. Idadi hiyo ni kubwa sana kwenye demokrasia. Wanaridhishwa kwa kupewa vyeo vingi vilivyoundwa kwa ajili yao. Na mzigo wote wa kuwalipa na kuwagharamia unaangukia nchi ambayo ni maskini
Kama nakuelewa vile...!
 
Alifunga wapinzani wake kisiasa,zuia maandamano ya kisiasa, alizuia harakati zote za kisiasa zilizokuwa kinyume na mtazamo wake na wa chama chake.
Nitajie hao wapinzani wake waliofungwa?
 
DEMOKRASIA NA NCHI MASIKINI

Leo nakuja tena na hii mada.

Kwanza ijulikane kuwa hakuna nchi masikini imewahi endelea ikIwa chini ya demokrasia. Ukifutilia historia utaona kuwa hakuna nchi imewahi kutoka kwenye umaskini ikiwa inaongozwa kidemokrasia. Nchi zote zilizofanikiwa kutoka kwenye umaskini zimeongozwa kidikteta au kifalme.

Demokrasia ni anasa ya matajiri. Nchi masikini ikiingia kwenye demokrasia inajichimbia kaburi. Kwanza sababu ni kuwa ni gharama kubwa sana kuendesha nchi ya kidemokrasia. Nchi ya kidemokrasia ina walaji wengi sana.

Msomi mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya udikteta na demokrasia ni idadi ya watu unaotakiwa kuwaridhisha ili uendelee kushika madaraka. Idadi hiyo ni kubwa sana kwenye demokrasia. Wanaridhishwa kwa kupewa vyeo vingi vilivyoundwa kwa ajili yao. Na mzigo wote wa kuwalipa na kuwagharamia unaangukia nchi ambayo ni maskini.

Serikali ya kidemokrasia haiwezi kuja na sera za maendeleo ambazo zitawataka wananchi wafunge mikanda. Kuna wakati ili nchi iendelee ni lazima watu wafunge mikanda. Mfano nchi inaweza kusema hatutaagiza ngano ila tutahakikisha tunazalisha wenyewe kiasi cha kututosha. Kwenye nchi ya kifalme au kidikteta hilo linaweza kufanyika na baada ya muda nchi ikajitosheleza kwa ngano. Kwenye nchi ya kidemokrasia ngano ikiadimika wiki tu watu watangia barabarani na kuiangusha serikali. Wapinzani watapiga kelele za ajabu. Rais mwenye maono wa Liberia aliangushwa kwa namna hii na nchi ikachukuliwa na watu wazembe kama Samuel Doe. Ukisema tukuze textile industry yetu hivyo tulinde soko letu watu watazama barabarani na kukunyofoa madarakani. Waliotuletea demokrasia walijua vema wanachokifanya.

Kwenye nchi ya kidemokrasia ajenda kuu ya mtawala ni namna ya kubaki madarakani. Maamuzi yake yote yanazingatia kutimizwa kwa ajenda hii, hata kama yapo kinyume na maslahi ya nchi. Mfalme au dikteta anakuwa yupo imara madarakani. Anaweza kuwaza namna ya kukuza uchumi na hivyo kujiongezea kipato.

Nchi kama S Korea, Singapore, Malaysia na Shelisheli zimeweza kutoka kwenye umaskini kupitia madikteta.

Nchi kama UAE, KSA na Brunei zimeweza kufanya vizuri chini ya Ufame.

Bado hakuna nchi ya kidemokrasia iliyojitoa kwenye umaskini. Kila aina ya utawala ina mapungufu yake lakini demokrasia ni mfumo wa hovyo zaidi.

Habari kubwa kwenye nchi za kidemokrasia si za maendeleo, bali habari kuhusu michakato ya kidemokrasia.

DEMOKRASIA NA NCHI ZILIZOENDELEA

Nchi iliyoendelea na inayofuata demokrasia lazima itarudi kwenye umaskini. Nchi ya kidemokrasia iliyoendelea lazima itageuka ya kisocialist. Yaani wananchi wake watakuwa wanadai huduma kutoka kwa serikali kila leo hadi serikali itashindwa kuhudumia. Wananchi watataka afya bure. Mwanasiasa atakaye waahidi hilo wanamchagua. Kesho watadai elimu bure, kesho kutwa mishahara mikubwa, ruzuku wakulima nk nk. Nchi hizi zinajikuta zina matumizi makubwa kuliko mapato. Na wakati huo huo wanachi wakiwachagua wanasiasa wanaowaahidi kodi ndogo. Mwisho zinajikuta zina madeni wasiyoyaweza na deficit(nakisi) kwenye bajeti. Kaangalie nchi zinazodaiwa madeni ya kutisha, utakuta nchi za kidemokrasia zilizoendelea hasa ndizo zinaongoza kwa madeni, wala si nchi maskini zinazotangazwa kila leo. US deni lake ni asilimia 90 ya GDP yake. UK ni kama asilimia 250 wakati China ni kama 13%.

Hili la nchi kushindwa kumudu gharama limetokea kwa Argentina na nchi nyingi zilizoendelea zinaenda muelekeo huo.

Wafanyakazi wa nchi zilizoendelea na zinazofuata demokrasia wanaunda unions, na kudai mishahara mikubwa, benefits na haki nyingi. Matokeo yake gharama za uzalishaji zinakuwa kubwa na nchi kushindwa kushindana na bidhaa za kutoka mataifa mengine kama China. Matokeo yake viwanda vinafunga.

Gharama za kujenga miundombinu kwenye nchi za kidemokrasia ni kubwa sana. China imeziacha mbali sana nchi za magharibi kwenye suala la treni ziendazo kasi. Sababu kubwa ni mchakato mgumu na gharama kubwa za kufanya hivyo kwenye nchi za kidemokrasia. Kwenye nchi za kidemokrasia ukitaka kujenga kitu utakutana na red tapes za maana. Kila kikundi kitatoa sauti zao. Wenye ardhi watagoma reli isipite kwenye mapori yao au watadai fidia za ajabu na kukupeleka mahakamani juu.

Wengi wape lakini wakati mwingine wengi hukosea vibaya sana. Suala la Brexit ni mfano wa hili. Watu wengi walipiga kura UK ijiondoe EU. Leo hii baada ya athari kubwa za Brexit waingereza wengi wanajuta na kusema kuwa suala la Brexit halikuwa sawa. Mambo ya kitaalamu hayapaswi kuendeshwa kidemokrasia.

Demokrasia haifai kwa nchi maskini. Tukae chini tutafute mfumo mwingine.
Hata hizo Nchi zilizoendelea kuna Deep state ambayo ipo juu ya sheria, Nchi kama Usa Raisi sio kiongozi mkubwa kabisa, kuna watu ambao raisi hawezi wagusa, Deep state = Disctator = Mfalme etc
 
Nitajie hao wapinzani wake waliofungwa?
Operation coldstore 1963 zaidi ya wakomunisti 100 walikamatwa.

Lee did not believe that "democracy necessarily leads to development" and that "the exuberance of democracy leads to undisciplined and disorderly conditions which are inimical to development".

So when people say, 'Oh, ask the people!' It's childish rubbish. We are leaders. We know the consequences. You mean that ice-water man knows the consequences of his vote? They say people can think for themselves? Do you honestly believe that the chap who can't pass primary six knows the consequences of his choice when he answers a question viscerally on language, culture and religion? —Lee Kuan Yew, 1998.

Lee was an outspoken critic of Western ideals of democracy, stating that "with a few exceptions, democracy has not brought good government to developing countries." He argued that in states such as China, the concept of democracy was simply "not workable", because of the large population size that had to be canvassed, while in India, the results of democracy "have not been spectacular". He believed in the state interference of the media and personal lives of citizens. He has been criticised for using his political power to wage lawsuits to bankrupt and imprison his political opponents, as in the case of J. B. Jeyaretnam and Chee Soon Juan. Francis Seow, the former solicitor-general of Singapore, has described Lee as such:

he prime minister uses the courts… to intimidate, bankrupt, or cripple the political opposition. Distinguishing himself in a caseful of legal suits commenced against dissidents and detractors for alleged defamation…, he has won them all.
 
Watu wanaiba mali za Umma wanafanya kila aina ya Ubadhirifu lakini wakipelekwa Mahakamani eti kwa sababu ya Demokrasia na Utawala wa Sheria wanashinda kesi kwa kutumia mali hizo hizo walizozikwapua. !

Watu wanavurunda sehemu zao za Kazi kwa kufanya kila aina ya madudu lakini Kiongozi anashindwa kumuwajibisha kwa sababu atakuwa amefanya Udikiteta 🤣😳

Mwamba alijaribu jaribu kidogo tu na mambo yalishaanza kukaa kwenye msitari 😅🙌👍

Watu wanatumbuliwa juu kwa juu hata huko mikutanoni 😳
Hakuna mchezo !
Tena yeye alikuwa na afadhali lakini huko China Korea Japan Vietnam huko huwa wanakula kitanzi tu !
Tanzania hakuna demokrasia sababu msingi wa demokrasia ni kuwepo kwa uchaguzi huru, bunge na huru mahakama Mfano nchi za demokrasia Rais akiwa nje ya madaraka anaweza shtakiwa na kufungwa
 
Operation coldstore 1963 zaidi ya wakomunisti 100 walikamatwa.

Lee did not believe that "democracy necessarily leads to development" and that "the exuberance of democracy leads to undisciplined and disorderly conditions which are inimical to development".

So when people say, 'Oh, ask the people!' It's childish rubbish. We are leaders. We know the consequences. You mean that ice-water man knows the consequences of his vote? They say people can think for themselves? Do you honestly believe that the chap who can't pass primary six knows the consequences of his choice when he answers a question viscerally on language, culture and religion? —Lee Kuan Yew, 1998.

Lee was an outspoken critic of Western ideals of democracy, stating that "with a few exceptions, democracy has not brought good government to developing countries." He argued that in states such as China, the concept of democracy was simply "not workable", because of the large population size that had to be canvassed, while in India, the results of democracy "have not been spectacular". He believed in the state interference of the media and personal lives of citizens. He has been criticised for using his political power to wage lawsuits to bankrupt and imprison his political opponents, as in the case of J. B. Jeyaretnam and Chee Soon Juan. Francis Seow, the former solicitor-general of Singapore, has described Lee as such:

he prime minister uses the courts… to intimidate, bankrupt, or cripple the political opposition. Distinguishing himself in a caseful of legal suits commenced against dissidents and detractors for alleged defamation…, he has won them all.
Naona umekariri tu vitu visivyo na muunganiko. Kigezo cha kwanza kikuu cha demokrasia ni uchaguzi huru na wa haki, Singapore imeshafanya chaguzi 13 tangu uhuru ambazo hazijawa na malalamiko ya wizi wa kura au uchakachuaji wa matokeo. Ni huyo Lee pia ambaye alisema ni muhimu sana kwenye nchi raia wakachagua viongozi wanaowataka wao kuwaongoza ili nchi ifanikiwe.
 
..Udikteta umeshindwa kuleta maendeleo Afrika, ndio maana kumekuwepo na kelele za kudai demokrasia.
Ghadafi mfano mzuri na Morocco Nchi zao huwezi fananisha na Zetu, pia Hata hapa Tanzania Nyerere alifeli tu sera za Uchumi ila other aspects kama Elimu tulikua vizuri tu, moja ya data kali za Nyerere miaka ya 1970 literacy rate ya Tanzania ilikua asilimia 90, compare na sasa literacy rate imeshuka hadi asilimia 80 na bado quality ya elimu ni mbovu mno compare na Zamani.
 
Ghadafi mfano mzuri na Morocco Nchi zao huwezi fananisha na Zetu, pia Hata hapa Tanzania Nyerere alifeli tu sera za Uchumi ila other aspects kama Elimu tulikua vizuri tu, moja ya data kali za Nyerere miaka ya 1970 literacy rate ya Tanzania ilikua asilimia 90, compare na sasa literacy rate imeshuka hadi asilimia 80 na bado quality ya elimu ni mbovu mno compare na Zamani.
Morocco ni nchi ya uchumi wa kawaida tu lakini yenye rasilimali nyingi sana.
 
Naona umekariri tu vitu visivyo na muunganiko. Kigezo cha kwanza kikuu cha demokrasia ni uchaguzi huru na wa haki, Singapore imeshafanya chaguzi 13 tangu uhuru ambazo hazijawa na malalamiko ya wizi wa kura au uchakachuaji wa matokeo.
Nini unacho jaribu kupinga na kutetea kuhusu Singapore ya LKY maana hata hueleweki
Unaita vipi nchi ya kidemokrasia mahali ambapo wapinzani wana gandamizwa ? Na kiongozi mkuu asiye amini katika huo utaratibu wa kidemokrasia unaoutetea wewe ?
Kuna vitu vya kutetea lakini sio Singapore ya Lee ambaye yeye mwenyewe mfumo mzima wa kidemokrasia alikuwa kinyume nao na alikuwa proud of Singapore mpaka leo hii haitoi uhuru bora wa maandamano moja ya legacy ya huyo LKY unaye mtetea
 
Back
Top Bottom