Habari za leo wana GT.
Niende kwenye hoja ya msingi.
Kwa utambulisho huu mimi si mgeni humu ila ID nliyotumia ni mpya niliona nifungue hii ili nisiwezekujulikana na wanaoifahamu ID yangu iliyozoeleka hasa mke wangu.
Kwa hakika hapa nilipo nina msongo wa mawazo unanisumbua na ninahisi ninapoelekea sio pazuri, Miaka mitano nyuma nilichukua mkopo kwenye bank moja hivi hapa nchini. Huu mkopo nilichukua kwa udhamini wa mshahara wangu wa kipindi kile.
Kuna jambo lilitokea ofisini hivyo ilinibidi ni resign ndani ya 24hrs hivyo sikupata chochote pale ofisni, (hii nitakuja kuisimulia siku nyingine) lakini nilijipa moyo kuwa maisha hayatonisumbua kwa vile ile pesa nilianzsiha miradi mbalimbali.
Lakini bila kujua kuwa sina uzoefu na usimamizi wa hii miradi yangu niliingia kichwa kichwa mambo yalianza kwenda mrama. Miradi iliyumba mingine niliifunga ilinibidi niuzie gari yangu niweze kusimama tena , lakini bado kama vile nilijiongezea dhiki tu.
Sasa nina miezi 10 sijapeleka rejesho la bank, na bank wanapiga simu sana mpaka waliniambia nijitahidi niweke chochote kile ili nisiwekwe kwenye blacklist. Watoto wangu nimewarudisha shule za Kayumba, hela ya kula imekuwa changamoto kiasi kwamba natamani hata kufa ili nisione hawa watoto wangu wanavyoteseka.
Nafikiri niuze nyumba hii moja niliyobaki nayo ili tu nijaribu tena bahati yangu kwenye biashara zingine lakini nahofia hiyo biashara ikifilisika hawa watoto nitawaweka wapi.
Hofu kubwa niliyonayo ni hawa watu wa hii taasisi ya bank nao wasije wakaniuzia nyumba yangu maana nimeshavurugwa mpaka kila ninalowaza naona haliwezekani.
Kwa upande mwingine naendelea kutafuta kazi nimeshafanya interview sehemu nyingi tu lakini sijabahatika kuitwa, miezi mitatu iliyopita interview yangu ya mwisho niliambiwa nitaitwa kwa ajili ya kuanza kazi mwezi wa saba au wa nane. Lakini mpaka sasa hivi sioni faraja yoyote ile ya kuitwa kwenye hiyo taasisi ya kimataifa.
Wana GT naomba neno la faraja kutoka kwenu nifanyaje ili niweze kumudu hizi heka heka za maisha na hasira za watu wa bank wasije kunipeleka mahakamani na kunifilisi.