MGOGOHALISI
JF-Expert Member
- Apr 16, 2011
- 3,294
- 4,920
Nimeona clip ikisambaa mitandaoni inayomwonyesha aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam mheshimiwa Paul Makonda akimtuhumu mmoja wa aliyewahi kuwa msaidizi wake kuwa alikua akichukua gari na kwenda kupora kwenye biashara za watu. Kwa kuwa uporaji ni jinai na jinai haifi ni wakati muafaka kwa jamhuri kuchukua hatua stahiki. Ifunguliwe kesi aitwe makonda ili mtu huyo ajulikane na haki itendeke.
Pia soma: Makonda: Dereva wangu alikuwa anafunga namba za RC DSM na kutapeli watu
Ikumbukwe kuwa Paul Makonda amekua akihusishwa na vitendo vya kihalifu kipindi akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na inaaminika hata kuwekwa pembeni ilikua ni mkakati wa kuwatuliza walalamikaji. Kwa kutoka kwake Paul Makonda na kutamka hadharani kuwa ni msaidizi wake alikua akifanya vitendo hivyo nitashangaa kama jamhuri kupitia mwendesha mashtaka watakaa kimya.
Pia soma: Makonda: Dereva wangu alikuwa anafunga namba za RC DSM na kutapeli watu
Ikumbukwe kuwa Paul Makonda amekua akihusishwa na vitendo vya kihalifu kipindi akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na inaaminika hata kuwekwa pembeni ilikua ni mkakati wa kuwatuliza walalamikaji. Kwa kutoka kwake Paul Makonda na kutamka hadharani kuwa ni msaidizi wake alikua akifanya vitendo hivyo nitashangaa kama jamhuri kupitia mwendesha mashtaka watakaa kimya.