Dereva Basi la Kilimanjaro Express aliyesababisha ajali na kuua watu wanne, afutiwa leseni

Dereva Basi la Kilimanjaro Express aliyesababisha ajali na kuua watu wanne, afutiwa leseni

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Dereva ambaye alisababisha ajali ya Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express iliyotokea jana Machi 14, 2022 Mkoani Songwe na kusababisha vifo vya watu wanne, Mjahid Waziri mwenye umri wa miaka 39, amefutiwa leseni ya udereva.

Ajali hiyo ilitokea wakati basi likitoka Tunduma kuelekea Dar es Salaam ambapo lililopindukia korongoni eneo la Senjele wilayani Mbozi sababu ikiwa ni mwendokasi alipokuwa akitaka kuyapita magari yaliyokuwa mbele yake likiwemo lori.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Rashid Ngonyani amesema wanamfutia leseni dereva huyo mkazi wa Dar es Salaam ikiwa ni hatua ya kwanza wakiwa wanamshikilia na baadaye watamfikisha Mahakamani.

Source: Clouds TV

Pia soma > Songwe: Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express lapata ajali, watu wanne wafariki dunia
 
Dereva ambaye alisababisha ajali ya Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express iliyotokea jana Machi 14, 2022 Mkoani Songwe na kusababisha vifo vya watu wanne, Mjahid Waziri mwenye umri wa miaka 39, amefutiwa leseni ya udereva.
Ukweli kwamba ameuwa watu wanne kwa uzembe wa kutisha..dereva kama huyu anastahili adhabu kali ili iwe fundisho kwa madereva wengine wa aina yake.. ikikubalika, ya kifungo cha maisha
 
  • Thanks
Reactions: Cyn
Ukweli kwamba ameuwa watu wanne kwa uzembe wa kutisha..dereva kama huyu anastahili adhabu kali ili iwe fundisho kwa madereva wengine wa aina yake.. ikikubalika, ya kifungo cha maisha
Mkuu......

Adhabu huwa siyo discretion ya Hakimu au Jaji. Sheria ndiyo inayotamka aina fulani ya kosa adhabu yake ni nini. You seem to be very emotional lakini hujawaza kuhusu laws and facts regarding the case at hand
 
Dereva ambaye alisababisha ajali ya Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express iliyotokea jana Machi 14, 2022 Mkoani Songwe na kusababisha vifo vya watu wanne, Mjahid Waziri mwenye umri wa miaka 39, amefutiwa leseni ya udereva.
Afutiwe hadharani vinginevyo anakwenda mlango wa nyuma anatoa mlungura anatengenezewa nyingine
 
Hiyo adhabu ni kubwa sana na ni imani yangu kwamba aliyeitpa amekurupuka. Huyu mtu ana familia, ndugu wanamtegemea kwa chakula, mavazi, matibabu, karo za shule na mengine mengi.

Kumfutia leseni kutaleta dhiki kubwa kwa wanafamilia na hata yeye mwenyewe.

Nawashauri mamlaka husika kulifikiria upya jambo hili na ikiwezekana imfungie leseni yake kwa kipindi kama sheria inavyosema na siyo kimfutia leseni yake.

Ajali zinatokea kila siku na haziwezi kuzuiwa kwa kuwafutia madereva leseni zao
 
Hiyo adhabu ni kubwa sana na ni imani yangu kwamba aliyeitpa amekurupuka. Huyu mtu ana familia, ndugu wanamtegemea kwa chakula, mavazi, matibabu, karo za shule na mengine mengi.

Kumfutia leseni kutaleta dhiki kubwa kwa wanafamilia na hata yeye mwenyewe.

Nawashauri mamlaka husika kulifikiria upya jambo hili na ikiwezekana imfungie leseni yake kwa kipindi kama sheria inavyosema na siyo kimfutia leseni yake.

Ajali zinatokea kila siku na haziwezi kuzuiwa kwa kuwafutia madereva leseni zao
Kwahiyo aendelee kuua watu kwa kigezo cha kwamba ana familia inamtegemea?
 
Kwani hapo senjele kuna nn naona sauli nayenyewe imepata ajali
FB_IMG_1647330477588.jpg
 
banana republic

polisi ana revoke leseni ya mtu
tena inafanywa ndani ya masaa 24

lakini nikiri mbele za Mola, nisingeishi Ulaya nisingejua kwamba leseni inapaswa kufutwa na mahakama, baada ya mchakato wa kimashtaka na utetezi
 
Afutiwe hadharani vinginevyo anakwenda mlango wa nyuma anatoa mlungura anatengenezewa nyingine
Hii inakuwa kama yale mabasi ambayo kampuni yake unaambiwa imefungiwa kwa kusababisha ajali,kinachofuata wanabadili rangi na jina la kampuni baada ya hapo wanaendelea na kazi kama kawaida...
 
Niliamini sana Kilimanjaro bus,

Imani ilipungua tarehe 14 December mwaka jana nilipokata tiketi nipandie mbeya mjini kiti kikauzwa mara mbili, ilikuwa fedheha kubwa,

Sasa dereva kafanya yake.

Nitapanda bus ipi tena
 
Hiyo adhabu ni kubwa sana na ni imani yangu kwamba aliyeitpa amekurupuka. Huyu mtu ana familia, ndugu wanamtegemea kwa chakula, mavazi, matibabu, karo za shule na mengine mengi.

Kumfutia leseni kutaleta dhiki kubwa kwa wanafamilia na hata yeye mwenyewe.

Nawashauri mamlaka husika kulifikiria upya jambo hili na ikiwezekana imfungie leseni yake kwa kipindi kama sheria inavyosema na siyo kimfutia leseni yake.

Ajali zinatokea kila siku na haziwezi kuzuiwa kwa kuwafutia madereva leseni zao
Nchi za wenzetu unafutiwa leseni
Tu, sharia hiyo inasaidia
Inawafanya madereva kunyooka
Na kutofanya mambo ya ajabuajabu

Ova
 
Hiyo adhabu ni kubwa sana na ni imani yangu kwamba aliyeitpa amekurupuka. Huyu mtu ana familia, ndugu wanamtegemea kwa chakula, mavazi, matibabu, karo za shule na mengine mengi.

Kumfutia leseni kutaleta dhiki kubwa kwa wanafamilia na hata yeye mwenyewe.

Nawashauri mamlaka husika kulifikiria upya jambo hili na ikiwezekana imfungie leseni yake kwa kipindi kama sheria inavyosema na siyo kimfutia leseni yake.

Ajali zinatokea kila siku na haziwezi kuzuiwa kwa kuwafutia madereva leseni zao
Hata marehemu walikuwa na watu wakiwategemea,,
 
Dereva ambaye alisababisha ajali ya Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express iliyotokea jana Machi 14, 2022 Mkoani Songwe na kusababisha vifo vya watu wanne, Mjahid Waziri mwenye umri wa miaka 39, amefutiwa leseni ya udereva.

Ajali hiyo ilitokea wakati basi likitoka Tunduma kuelekea Dar es Salaam ambapo lililopindukia korongoni eneo la Senjele wilayani Mbozi sababu ikiwa ni mwendokasi alipokuwa akitaka kuyapita magari yaliyokuwa mbele yake likiwemo lori.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Rashid Ngonyani amesema wanamfutia leseni dereva huyo mkazi wa Dar es Salaam ikiwa ni hatua ya kwanza wakiwa wanamshikilia na baadaye watamfikisha Mahakamani.

Source: Clouds TV

Pia soma > Songwe: Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express lapata ajali, watu wanne wafariki dunia
Kwanza wanamfutia leseni, na baadaye watampeleka mahakamani. Ina maana wanamfutia leseni kabla hajapatikana na hatia. Vipi akifikishwa mahakamani na ikaonekana hiyo ilikuwa ajali tu ambayo hakuwa na uwezo nayo wa kuizuia? Ina maana hana hatia. Nini hatima ya kufutiwa leseni iwapo itatokea hivyo?
 
Kwanza wanamfutia leseni, na baadaye watampeleka mahakamani. Ina maana wanamfutia leseni kabla hajapatikana na hatia. Vipi akifikishwa mahakamani na ikaonekana hiyo ilikuwa ajali tu ambayo hakuwa na uwezo nayo wa kuizuia? Ina maana hana hatia. Nini hatima ya kufutiwa leseni iwapo itatokea hivyo?
Nasikia polisi ni mahakama ndogo ndani ya mahakama kubwa. Huko barabarani ukipigwa tochi ya overspeeding, ujue Tiganga na Kibatala huwa hawajafanya mambo yao ya PGO, lakini pesa lazima ulipe!
 
Back
Top Bottom