Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Imeandikwa afichaye dhambi hatafanikiwa.

Dhambi tajwa hapo juu, kwamwe huwezi tubu pekeako sirini ukatoboa.

Ni kheri kutii kuliko kuwa mbishi.

Amen
 
hivi ninyi mnasali kanisa gani, mbona mnaficha kanisa lenu, au ni kanisa la uongo? tuambieni mnasali wapi tuwajue ili tujue kati yetu sisi na ninyi nani wa kusaidiwa kiroho. mpo nyuma sana kumjua Mungu na ninawaombea kwa Mungu awasaidie.
 
Unafanya KAZI ya Sauli, kuua na kupinga akina Petro ukiamini unamtetea Mungu kumbe unapotosha unamuudhi.

Mungu akusaidie.
 
Hebu niambie umuhimu/kazi sadaka unayoitoa wewe ukiondoa kwamba ni 'shukurani', umuhimu mwingine ni upi ?
kuendeleza kazi ya Mungu, shukran kwa Mungu, kumbariki mtu yeyote mwenye uhitaji, fungu la kumi,malimbuko, nakadhalika. umuhimu wake ni kuonyesha upendo wangu kwa Mungu, au kwa ndugu au kutii agizo la Mungu alilotuambia tutoe sadaka katika mazingira mbalimbali.

hoja yetu sasa ni hii, unapoenda kutubu na umeshika sadaka, unashukuru nini tu? unashukuru kusamehewa hata kabla haujaomba msamaha? huoni kama unamhonga Mungu akusamehe? ninyi mnasali wapi? tuambieni hat akwenye DM tu.
 
Umetoa mfano mzuri sana, kwamba Yesu alimwambia Anania aende kwa Paulo ....... unadhani ni kwanini Yesu alimtuma tena Anania aende kwa Paulo wakati alishakutana nae njiani ?
 
hivi ninyi mnasali kanisa gani, mbona mnaficha kanisa lenu, au ni kanisa la uongo? tuambieni mnasali wapi tuwajue ili tujue kati yetu sisi na ninyi nani wa kusaidiwa kiroho. mpo nyuma sana kumjua Mungu na ninawaombea kwa Mungu awasaidie.
Tunasali Kanisa Gani??!!!

1. Hekalu ni mwili wangu.

2. Madhabahu ni Moyo wangu.

3. KANISA ni Mimi mwenyewe.

4. Mwalimu ni ROHO MTAKATIFU.

Taa na chakula CHETU ni Neno la Mungu lenye Pumzi yake.

Unataka tusali wapi ilhali Ibada imo ndani yetu?
 
Unafanya KAZI ya Sauli, kuua na kupinga akina Petro ukiamini unamtetea Mungu kumbe unapotosha unamuudhi.

Mungu akusaidie.
kinyume chake wewe ni ajenti wa shetani bila kujijua, na utahukumiwa kwa upotoshaji huu. unadhihaki sadaka ambayo Yesu Kristo aliitoa kwa machungu mengi, wewe unaona kama haikutosha?

hakuna aliyesema tusitoe sadaka. kiujumla, mafungu ya kumi, malimbuko na sadaka za upendo kwa Mungu ni lazima utoe, ndivyo Neno la Mungu linasema. ila kutoa fungu la kumi unapoenda kutubu ni ushetani na upotofu ambao shetani ameupanda kwenye mioyo yenu mpate kiuipotosha kweli. jueni kuwa Mungu hana uhitaji wa sadaka zenu, Mungu ni Mungu hata bila Sadaka zenu, hahongwi, usije kwenda kwake kutubu hizo dhambi ambazo Yesu alizifia ukiwa umeshika sadaka ukajiona mtakatifu, mtume wako amekupotosha na mnaelekea wote motoni.

kitu pekee ambacho najua nimekufanya hapa, nimeenda kinyume na mafundisho ya mtume wenu au nabii wenu anayoyatumia kupiga pesa, au pengine ninyi wenyewe ni manabii wa uongo, mnapotosha watu hapa. wekeni mistari ya Biblia, hamna, mnaongea porojo tu. mshindwe kwa Jina la Yesu.
 
Umetoa mfano mzuri sana, kwamba Yesu alimwambia Anania aende kwa Paulo ....... unadhani ni kwanini Yesu alimtuma tena Anania aende kwa Paulo wakati alishakutana nae njiani ?
hakuna aliyebisha kuombewa, tunachobisha hapa ni sadaka. hata mimi nilipookoka nilitubu kwa kuombewa, na ninawaombea watu kwa kuwawekea mikono wanapotubu waokoke au kuomba pamoja nao rehema kwa Mungu. lakini hawatakiwi kuja na sadaka. hoja hapa Ni SADAKA. sadaka sadaka.
 
Umetoa mfano mzuri sana, kwamba Yesu alimwambia Anania aende kwa Paulo ....... unadhani ni kwanini Yesu alimtuma tena Anania aende kwa Paulo wakati alishakutana nae njiani ?
Swali zuri,

Maana ilitosha Yesu kumwambia nimekusamehe, Damu yangu inatosha.

Kwanini amtume aende kutafuta watumishi?
 
Tunasali Kanisa Gani??!!!

1. Hekalu ni mwili wangu.

2. Madhabahu ni Moyo wangu.

3. KANISA ni Mimi mwenyewe.

Unataka tusali wapi?
basi inatosha, ninyi ni maajenti wa shetani. kwamwambieni shetani aliyewatuma mmekutana na watu wa Mungu huku wamejua njama zenu.
 
Yesu alipokufa pale msalabani pazia la hekaru lilipasuka maana yake ametoa mpaka kati ya Mungu na mwanadamu hivyo tukiwa na shida ikiwemo kutubu sio lazima kwenda kwa mchungaji sisi wenyewe anatusikia

Labda kuvunja maagano ya giza muda mwingine mtu peke yako huwezi! Inakubidi umuombe mchungaji msaada!
 
Mungu anapenda Rehema kuliko sadaka.

Mathayo 9:13
Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.


Na hatutoi sadaka ili tusamehewe dhambi, maana sadaka zetu haziwezi kufuta dhambi isipokuwa sadaka moja tu ambayo ni damu ya Yesu.
 
shenziii kabisaa eti sadakaa πŸ˜–πŸ˜–πŸ˜–
 
Naomba orodhoshe hizo dhambi zingine unazoweza kutubu peke yako?
 
Kwamfano kuvuta sigara ni dhambi au sio dhambi.

Kuvuta bangi ni dhambi au sio dhambi?
 
DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.


kwa kifupi, nimejaribu kusoma andiko lako, hayo maneno mekundu hapo juu ndio yameharibu kila kitu. na huo ndio msingi wa mafundisho ya kishetani. tunasamehewa dhambi bure, Yesu alilipa deni la dhambi bure, msitoze watu ili wasamehewe dhambi, ni wizi kama wizi mwingine tu, Yesu angekuwa anatoza watu pesa hivyo wengine tusingeokoka manake hatukuwa na pesa.
 
Upo sahihi kabisa, hapo kwenye kuvunja maagano ya giza kuna wakati tunahitaji watumishi wa Mungu watupe muongozo.
 
basi inatosha, ninyi ni maajenti wa shetani. kwamwambieni shetani aliyewatuma mmekutana na watu wa Mungu huku wamejua njama zenu.
Rudi kusoma na uombe Mungu akusaidie kuelewa.

Sadaka ni AMRI.

Ikiwa Mungu alimtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo, sisi pia lazima tuendapo nyumbani mwa BWANA twende na sadaka,

Na sadaka hiyo Si mbadala wa Damu ya thamani ya Yesu,

Sadaka hiyo ni shukrani Kwa zawadi ya uhai na shukrani Kwa Yesu wetu.

Amen
 
sasa umeelewa, ndicho nilichokuwa nasema.
 
amri kutoka kifungu gani cha Biblia wewe kwamba twende kuomba rehema/msamaha kwa Mungu tukiwa na sadaka? unasema tuendapo nyumbani mwa Bwana tuwe na sadaka, nakubaliana na wewe, hoja tunayobishana hapa ni wakati ule wa kutubu, kwani kwenda kwa mtumishi wa Mungu utubu lazima iwe nyumbani mwa Bwana, huwezi kumfuata nyumbani kwake, kazini kwake au popote alipo uombe akuombee? manake hapo unaongelea kutoa sadaka kama kawaida uingiapo nyumbani mwa Bwana, hapo ndipo unapochanganya.

hatupingi kutoa sadaka, uingiapo nyumbani mwa Bwana hautakiwi kuingia mikono mitupu, sawa, ila wakati wa kutubu sio lazima uende na sadaka kwanza sio lazima mtumishi anayekuombea kama nikiamua kukubaliana na wewe kwamba awe nyumbani mwa BWana, anaweza akaja hata nyumbani kwako ukatubu akashiriki na wew ekumsihi Mungu akusamehe, au ukaenda kwake, au ukaenda kazini kwake au popote nje ya kanisa/madhabahuni. ingekuwa hivyo basi tusingetubu hadi siku ya ibada ifike. na kama unaenda nyumbani, kasini au akija kwako ukamweleza dhambi yako wazi muombe au akuombee, anachukua sadaka ya nini sasa wakati pale sio nyumbani mwa Bwana na yeye hana gharama yeyote ameitoa kusamehewa dhambi zako, atakula sadaka kwa kazi gani sasa ameifanya kwa ajili ya msamaha wa dhambi zako. au sadaka zenu ninyi huwa zinapaa mbinguni kama zilivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…