Dhambi ya kikokotoo cha wastaafu ni mbaya kuliko dhambi ya mauti

Dhambi ya kikokotoo cha wastaafu ni mbaya kuliko dhambi ya mauti

Mchawi wa watumishi wa Tanzania hasa walimu wetu ni Cwt ambao waliiomba serikali siku ya sherehe za mei mosi zilizofanyika Mwembetogwa Iringa kwamba serikali ipunguze mafao ya mkupuo kutoka asilimia 50 hadi 25 ili mtumishi apate package kubwa ya hela ya mwezi huku bado akiwa amepanga nyumba au yuko nyumba ya makuti.Hakika vyama vya wafanyakazi Tanzania ni majanga .Sijui wanapata nini hao walimu wetu waliowachangia mamilioni kama ada ya uanachama wakiishi maisha mabovu?
Vyama vya wafanyakazi ni upuuzi mtupu, wanapunguza hata hicho kidogo mfanyakazi anacholipwq. Ni heri tubaki bila vyama vya wafanyakazi malipo yetu halali tutayakuta kwa Mungu. TUCTA na cwt tunawaona siku za Mei mosi TU na kutupoza na t-shirt. Wanatuona sisi mazuzu. Mishahara midogo fedha zinaibwa na wajanja wao wapo TU.
 
Aliyeanzisha kikokotoo ni nani kwani
Ni marehemu kwa sasa. Huyu wa sasa ameamua kurithi mikoba ya bosi wake marehemu. Naamini ipo siku muda utafika tu, watumishi wa uma watakikataa hiki kikokotoo chao kwa vitendo.
 
Serikali ya ccm itakuja kufa kifo kibaya sana kutokana na huu uhuni wanaoufanya kwa wastaafu, kupitia vibaraka wao TUCTA na CWT.
Weee!!! CCM inawajuwa vema watanzania na wanachama wake, inazifahamu tabia na sifa za wanachama wake na watanzania kwenye matukio mbalimbali. Kila mtawala anatawala kulingana na tabia na hulka ya anaowatawala. Mfano, kama anajuwa kuwa watu wake wanaleta vurugu kubwa kama wakikosa mikate atahakikisha kuwa mikate haikosekani mitaani. wanaCCM kazi Yao ni kuimba iyenaiyena TU hata kama maisha Yao binafsi sio mazuri na tabia ya watanzania ni kushitaki kwa Mungu na kutarajio Iko siku serikali itakiona Cha mtema Kuni na siku zinapita na awamu zinapita. Kazi kubwa ya kiongozi ni kumaliza awamu yake tu salama huko mbele watajuwa wengine. Anachojua ni kwamba hatashitakiwa kwa matendo yake katiba inamhakikishia hilo
 
Back
Top Bottom