Dhamira ya kuua upinzani ni kwa faida ya Chama Tawala au Ubinafsi wa mtu mmoja?

Dhamira ya kuua upinzani ni kwa faida ya Chama Tawala au Ubinafsi wa mtu mmoja?

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2019
Posts
9,863
Reaction score
20,806
Wanabodi za asubuhi!naenda moja kwa moja kwenye mada.

Kwa wale makomredi wa chama tawala naombeni ufafanuzi wenu kuhusu lengo la kuua upinzani nchini linaisaidiaje CCM kama chama tawala? Upinzani si ndio kioo? kama kwa miaka mingi upinzani umekuja na ajenda nyingi za wananchi ambazo serekali imefanyia kazi kwanini mnauua? Ni kwa faida ya chama au mtu mmoja?

Wakati wa JK upinzani ulizuia nini? Ulizuia ujenzi wa miundo mbinu? Ulizuia uchumi? Mbona ulikuwepo na nchi ilisonga mbele? Ni nani huyu anaeuua? Ni CCM au mtu? Kama ni mtu ana ajenda gani binafsi ambazo chama tawala hakijui? MIMI TANGU NIPATE AKILI SIJAWAHI ONA UPINZANI UKIWA KIKWAZO CHA MAENDELEO

Mniambie ni maendeleo gani ambayo yamezuiwa na upinzani? Je ni stigglers gorge? Hawakusema taratibu za bajeti zifuatwe? Je ununuzi wa ndege? Hawakusema bunge ndio lenye idhini ya kupitisha bajeti ya manunuzi? Je ni elimu bure? Je hawakusema wao wanataka kuanzia msingi hadi chuo?

Makomredi naombeni majibu. Kuua upinzani je ndani ya ilani ya CCM imeidhinishwaje? Mkakati ndani ya ilani unasemaje? Ndio huku kukimbia kupokea fomu za wagombea wa upinzani? Ndio huku kununua wapinzani? Ndio ilani ya CCM imesema hayo? Huyo anaeua upinzani mnadhani ana malengo ya kutoka madarakani? Kama anaua upinzani ni kwa faida ya nani kama ataondoka madarakani? JIULIZENI UPINZANI UNAKUFA KWA FAIDA YA NANI? JE NI NCHI? MTU? AU CHAMA?

KARIBUNI MAKOMREDI WA KIJANI KWA MAJIBU MJARABU!!!
 
vingi ulivyoandika ni hisia binafsi zisizo na uhalisia wala ukweli.

Kifo cha upinzani rasmi kilianza 2012 ni katika kipindi hiko maandamano yalikuwa mengi sana na wenyewe kuamini kuwa maandamano na migomo itajenga chama , tulikaa pembeni na tukaawaambia mnayofanya ni hatari kwenu ila hamkusikiliza. Leo mnalalamika kufa kwa upinzani huku mnajua mmeua wenyewe?

si CCM wala mtu binafsi kutoka CCM aliyeua upinzani wala mwenye dhamira ya kuua upinzani, mbinu zenu mnazotumia ninyi wapinzani ndio zinawaua na msimlalamikie yeyote yule.

CCM nitaitetea kwa nguvu zote na viongozi wake ,kipindi ambcho sisi CCM tulikuwa tunajenga chama ninyi mlikuwa mnatafuta " cheap political popularity " kutoka kwa makundi yasiyoweza kufanya uamuzi wala kupiga kura kama watoto walio chini ya miaka 18
 
Unajiua wenyewe, walipoanza kipata nguvu ya uma wakajisahau, sasa hawana mawazo ya wananchi sasa wanatumia miujiza yao kichwani wakifikili wamebeba akili za wananchi, wamevimbewa sasa watapukutika, siku wakipatikana wenye weledi upinzani utakomaa.
 
1. Wapinzani hasa viongozi takribani wote wanakesi zaidi ya mbili ..... naomba uelezee kwanini hayakutokea wakati wa Mkapa, au Kikwete?

2. Msajili wa vyama kupambana na wapinzani akisema katiba inavuja

A) kaihujum Cuf mpaka imesambaratika kwa msaada wa dola....polisi nk kwanini anaingilia mambo ya ndani? Jadili hili ukilinganisha nyakati za a) Mkapa b) Kikwete

2. Mikutano ya kisiasa kupigwa marufuku
A) katiba ya Tanzania inasemaje .....Msajili wa vyama anasimamia upande upi? jadili hili la kuiheshimu katiba ukilinganisha wakati wa Mkapa na Kikwete

B. Niwakati gani?
a) Chama kinajiimarisha
b) Kinatoa Elimu kwa watanzania

3. Bungeni, tumeshuhudia kinachoendelea, je?
a) Bajeti inapangwa ikulu? Jadili kwa mifano
- bajeti ya manunuzi ya ndege
- stiglers mradi wa umeme
- uwanja wa ndege chato

b) Nini dhamira ya bunge kuondoa matangazo ya moja kwa moja television .. kwa wapigakura nikuona kazi waifanyao wabunge wao? Wanaficha nini? Kwa faida ya nani ilikulinganisha hoja na utekelezaji pia ufanisi

c) Jadili fukuzafukuza ya wabunge hususani wa upinzani ukirejea nyakati za kikwete na Mkapa, kutosikilizwa na kugomea hotuba zao zisisomwe, nikwa faida/hasara ya nani? Kwanini zisisomwe ili watanzania wazihukumu kwa ulinganifu wa hoja?

Nitaendelea nikipata muda.
 
Naona wamepania sas hivi hupati mkopo wa elimu ya juu bila kuwa mwanachama wa UVCCM, licha ya kuwa hii ni kosi y watanzania wote, bila kujali chama, admin endelea kufuta uzi zngu
 
Sidhani kama chama changu cha mapinduzi kina nia hii ya hovyo kwani kilikuwepo toka enzi na enzi , ninachokiona ni dhamira ya watu au kikundi cha watu wachache wenye kujitakia maslahi binafsi,
Refer, malalamiko ya viongozi wengi waliopita wa juu wa chama.
 
Hawataki kuulizwa au kuhojiwa na yeyote yule. Wanataka wawe huru kufanya walitakalo hata wakibweteka ni sawa tu. Baba akiamua kupeleka hela ya ada kutumbua na nyumba ndogo ni sawa tu.
 
adolay,

A great thinker..nakionea huruma kizazi cha sasa kilichopo mashuleni mana kinakaririshwa ujinga wa kiwango cha lami eti Uzalendo ni kusifia kila kitu kinachofanywa na viongozi wa kiserikali hata kama ni cha kipumbavu...
Mzungu wa South Africa amedhulumiwa mali zake,ameibiwa ameshtaki ili kudai haki yake tunashurutishwa kumpinga na kuwa kinyume nae,Uzalendo sio Wizi Uzalendo ni kutenda yaliyo mema kwa wengine ili nasi pia tusitendewe mabaya..
Unapomfundisha mtoto wako wizi aibe or adhulumu cha jirani siku akikuibia ww mwenyewe usilalamike kuwa mtoto wako ni mwizi..
 
Upinzani hauwezi kufa Bali ndio unazidi naimani hiyo ukiangalia Uganda au Rwanda pamoja na ukandamizaji unaoendelea bado upinzani upo na utaendelea kuwepo,

Nchi km Uganda au Rwanda pamoja na kujitapa kwa viongozi wao kuwa wamefanya makubwa Kwa nchi yao lkn ukaitishwa Leo uchaguzi wa haki wataangukia pua
 
Upinzani hakuna wa kuuua kinachofanyika ni kuwaonea,kuwatesa na kuwaua watu waliopo Upinzani lakini upinzani utakuwepo milele
 
Back
Top Bottom