Dhamiri yamlazimisha Rais Magufuli kukiri uharibifu katika uchaguzi wa Oktoba 2020

Dhamiri yamlazimisha Rais Magufuli kukiri uharibifu katika uchaguzi wa Oktoba 2020

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
DHAMIRI YAMLAZIMISHA RAIS MAGUFULI KUKIRI UHARIBIFU KATIKA UCHAGUZI WA OKTOBA 2020!

Nilipokuwa nahojiwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, nililazimika kumueleza mmoja wa maofisa waliokuwa wananihoji nikasema kuwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020 haukuwa Huru na wala haukuwa wa Haki. Aliponiuliza kama nilikuwa na ushahidi nilimjibu kuwa ndio ninao ushahidi!

Kama Madiwani waliopatikana katika Uchaguzi ule wamekataliwa na Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa Chama chao kwa kuwaambia hadharani na ametamka kwa ujasiri kuwa hawakuchaguliwa na watu, je walichaguuliwa na nani? Jibu hapa rahisi na la wazi nalo ni kuwa walichaguliwa na Tume ya Uchaguzi!

Tunaweza kusema kuwa kwa maneno na kauli ya Rais Magufuli, Tume ya Taifa ya Uchaguzi haikutenda Haki na haijawa Huru machoni pa Watanzania na hata machoni pake yeye mwenyewe. Kama Madiwani wale hawakuchaguliwa na watu, sahihi kabisa pia kuwa Wabunge, na Rais nao hawakuchaguliwa na watu kwa kuwa wote walipatikana katika Uchaguzi mmoja uliosimamiwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo ndiyo inayolalamikiwa!

Tunawaalika Watanzania wote kujitokeza na kushiriki kwa kikamilifu katika kampeni za kuhamasisha umma wa Watanzania kuhusu umuhimu na uhitaji wa Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Nitakuwa nikingoza kampeni hizo katika nchi nzima nikiwa nimevalia majoho ya Kiaskofu!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfutate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Inabidi kuopiga kelel kumwambia Jiwe kuwa yeye si Rais maana hakuchaguliwa na watu, yeye hana tofauti na Idd Amin aliyepindua serikali halali ya Obote au huyu wa Myanmar
Min Aung Hlaing

1614219661811.jpeg

The Tatmadaw proclaimed a year-long state of emergency and declared power had been vested in Commander-in-Chief of Defence Services Min Aung Hlaing. It declared the results of the November 2020 general election invalid and stated its intent to hold a new election at the end of the state of emergency.
 
Tunawaalika Watanzania wote kujitokeza na kushiriki kwa kikamilifu katika kampeni za kuhamasisha umma wa Watanzania kuhusu umuhimu na uhitaji wa Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya! Nitakuwa nikingoza kampeni hizo katika nchi nzima nikiwa nimevalia majoho ya Kiaskofu!

Tume huru ya uchaguzi ni maneno yenye maana inayobadilika kulingana na nchi husika.

Lakini, pamoja na equivocation hiyo, bado hapa kwetu Tume ya aina hiyo ni hitaji muhimu na la lazima kwa Taifa. Kampeni ya kuidai ni muhimu.

Maandamano yanaweza kuwa sehemu ya kampeni hiyo.

Maaskofu waliovaa majoho wanaweza, na wanapaswa, kuwa sehemu ya maandamano hayo.

Lkn maandamano hayawezi, na hayapaswi, kuwa hatua ya kwanza.

Hatua ya kwani ni, na inapaswa kuwa, kujibu swali lifuatalo na kuhakikisha waandamanaji watarajiwa wanaelewa jawabu kwa swali:

TUME HURU INAYOTAKIWA TANZANIA NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?

Nadharia kabla ya utekelezaji ni muhimu sana kwa kuwa itatuwezesha kufanya tathmini baada ya kutenda.

NB:

Najua mengi yaliyofanywa na watu wasiojulikana ktk kuvuruga uchaguzi uliopita. Lakini nilichoelewa kuhusu kauli ya sasa ya Magufuli ni hiki: Madiwani wa city council hawana direct electorate. TUkitaka kujenga hoja vizuri tujiepushe na hila katika hoja zetu. Yaani tujiepushe na hila kama vile spinning iliyofanywa na Mwamakula ktk maelezo yake.
 
Kule waliko haribu kama Mtwara baada ya kuwapoka korosho zao, walipitisha madiwani na wabunge bila kupingwa.
Tatizo huyu bwana ni kigeugeu yaani mbele za camera huwa anaropoka kuwaumiza waliojitoa kufuata alichokitaka/maagizo yake alafu kwenye audience anawaanika. NYUMA YA PAZIA HUWA NI YEYE AMBAE ANAAGIZA VYOTE HIVYO
 
Tatizo huyu bwana ni kigeugeu yaani mbele za camera huwa anaropoka kuwaumiza waliojitoa kufuata alichokitaka/maagizo yake alafu kwenye audience anawaanika.NYUMA YA PAZIA HUWA NI YEYE AMBAE ANAAGIZA VYOTE HIVYO
Ninaanza kuamini kuwa kuna mtu ana file kwenye ile hospital ya taifa ya maswala ya ubongo.
 
Ukiona magufuli ana act kama kukiri kosa basi huo ni muda wa kuwa makin kuliko maelezo.. sio muda atawapiga kanzu.sawa wapinzan? Anawatia chenga kuja kushtuka mmepigwa tobo goli la 3 chaliii...msisema sikusema
 
Tume huru ni hitaji muhimu la Taifa. Kampeni ya kuidai ni muhimu.

Maandamano yanaweza kuwa sehemu ya kampeni hiyo.

Maaskofu waliovaa majoho wanaweza, na wanapaswa, kuwa sehemu ya maandamano hayo.

Lkn maandamano hayawezi, na hayapaswi, kuwa hatua ya kwanza.

Hatua ya kwani ni, na inapaswa kuwa, kujibu swali lifuatalo na kuhakikisha waandamanaji watarajiwa wanaelewa jawabu kwa swali:

TUME HURU INAYOTAKIWA TANZANIA NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?

Nadharia kabla ya utekelezaji ni muhimu sana kwa kuwa itatuwezesha kufanya tathmini baada ya kutenda.

Achana na manadharia ya darasani maana wanaozuia katiba ya wananchi hawatumii elimu zaidi ya mabavu, hila na uhuni. Kinachotakiwa kwa sasa ni katiba mpya, na bila mashinikizo haiwezi kupatikana. Wewe subiri ikipatikana utatumia hizo nadharia zako za darasani kuiboresha.
 
Tatizo huyu bwana ni kigeugeu yaani mbele za camera huwa anaropoka kuwaumiza waliojitoa kufuata alichokitaka/maagizo yake alafu kwenye audience anawaanika.NYUMA YA PAZIA HUWA NI YEYE AMBAE ANAAGIZA VYOTE HIVYO

Kimsingi haya maagizo ya kuvuruga uchaguzi ni yake kwa 100%, lakini anajikuta kwenye wakati mgumu maana anaona kabisa amekipotezea chama chake mvuto, na kwenye box la kura hawapati matokeo aliyotegemea, na watu hawataki kupiga kura tena, na sababu hasa ni yeye.
 
Na unafiki pia wa kujiona yeye mporaji alichaguliwa lakini madiwani hawakuchaguliwa katika uchaguzi ule ule uliosimamiwa na Tume FAKE.
Si unafiki ni utawala wa mabavu, hatuna demokrasia Tanzania. Hatuna haki ya kuchagua viongozi tunao waamini na kuwapenda.
 
Hivi huyu askofu ni mzaliwa wa mkoa gani haswa?

Maana kama anatoka sehemu za mipakani naona afadhali aandae orodha ya kuanzia mababu wa mababu na akumbuke vizuri yalipo makaburi yao.
 
Ni Mwenyeji wa Mbeya Mkuu.
Hivi huyu askofu ni mzaliwa wa mkoa gani haswa?
Maana kama anatoka sehemu za mipakani naona afadhali aandae orodha ya kuanzia mababu wa mababu na akumbuke vizuri yalipo makaburi yao.
 
Back
Top Bottom