Dhana ya kwamba mshahara ukiongezwa na inflation itatokea ni dhana inayopaswa kufikiriwa na kichaa tu

Hatuongezi mishahara kwa sababu hatujawaongezea kazi; badala yake tunampango wa kushusha bei za bidhaa kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa na huduma wenye tija kupitia mipango mkakati kama Rufiji na SGR.

Bado hamjamaliza kununua ndege
Bado mnakarabati nyumba za wakuu wa miko kwa mil 170

Hivi unajua ukishaishiwa hoja kinachofata ni kipi?
 
Sheria na taratibu za ajira ndio lengo la huu mjadala, kwamba taratibu za kikatiba na kimkataba juu ya ajira ziboreshwe kwa siku za usoni.

Kutaka watu waongezewe mshahara pale tu wanapokuwa wameongezewa kazi ni nia ovu?

Kutaka watu wadai kushuka kwa bei za bidhaa badala ya kudai nyongeza ya mshahara ni nia ovu?
 

Francis, nataka nijibu hoja zako kama hapo juu.
1-Wafanyakazi, kuna nyongeza kama promotion uki badilishiwa majukumu hii huna shida nayo lakini kuna nyongeza ya madaraja mfano mwalimu wa mwaka wa kwanza hawezi kupokea sawa na mwalimu wa miaka 10 wakiwa na same qualifications, akianza kazi anaanza na Minimum mshahara katika grade ile ila kila akipata ujuzi anapanda level ili afike Max katika daraja lilelile ikitokea kapanda kuwa mwalimu mkuu hapo promotion anaanza katika grade mpya Min ataanza kupanda slowly kufika Max hii ni haki ya mfanyakazi kisheria.
2- Kuna hii kuongezwa mshahara kwa ujumla wafanyakazi wote kila mwaka hii inategemea na inflation na C.Bank wao wanatoa data hapo serikali ikiona kweli inflation ni kubwa inatoa kufidia na uwezo wa serikali, lakini ukiona inflation kubwa lakini serikali hawana pesa basi uchumi mbaya na kama wakitoa basi ni lazima wa manage inflation kuwa positive. Inflation inaongeza ukuwaji wa kiuchumi ni dalili watu wanaweza kufanya manunuzi wengi, tatizo kubwa ikiwa inflation ni over supply ya pesa kwa maana labda kuna pesa chafu watu wanapiga deal wanaiba pesa nyingi hawa wataleta inflation mbaya maana wataanza kununua vitu sio bei yake na kuwaumiza wengine kama ilivyokuwa miaka fulani Dar. nchi ikiwa haina inflation kabisa hiyo ni dalili ya uchumi kusinyaa na umaskini, inflation nzuri lakini kuwa managed.
3- Umeme watapunguza tu ili tufikie ushindani na nchi zingine sababu umeme wetu ni ghali ila kusema kuwa tuajiri tu wengine je una uhakika miaka 10 ijayo uchumi utakuwa endelevu na kuwalipa hawa wafanyakazi. chukuwa mfano una mfanyakazi nyumbani kwako unamlipa laki moja, kesho anakuja anakwambia naomba nyongeza maisha magumu utamwambia badala ya kukupa bora niongeze mfanyakazi mwingine nitakupunguzia kazi za kufanya, hapana utampa alfu 20 bora kuleta mwingine.
 
Kuna aliesema cost ni umeme tu? Umeme unatolewa kama mfano wa moja ya viunganishi muhimu katika gharama za uzalishaji, unajua maana ya neno ‘Mfano’? Pia usafirishaji unatajwa kama mfano mwingine wa kiunganishi muhimu katika gharama za uzalishaji, sio kwamba ni hizo tu, ila kuna factors nyingi, kubwa zaidi zikiwa hizo , nishati (Rufiji) na usafirishaji(SGR).

Hakuna asiyefahamu kwamba nyongeza ipo kikatiba na kimkataba, ila lengo la mjadala ni kujaribu kuleta maboresho ya kikatiba na kimkataba juu ya ajira katika siku za usoni.

Sasa turudi kwenye mada; Je, tuongezee mshahara watu ambao hawajaongezewa kazi? Si sahihi zaidi badala yake kudai bei za bidhaa na huduma zishuke ili kipato kidogo alichonacho mtu (WaTz wote) kiwatoshe?
 
Mkapa hakuongeza mishahara, bei ya vitu haikupanda lakini alivyokuja JK aliongeza mishahara na bei zikapanda hovyo.
Ili mishahara iongezwe lazima kuwepo na tija sanasana watumishi wangeomba wapandishwe madaraja.
Wabunge wanakuwa na mishahara mikubwa sababu wamejitengenezea kanuni zao ingawa lazima rais aidhinishe.
 
Hizo taratibu za kikatiba na kimkataba juu ya upandishaji mishahara sote tunazifahamu, na lengo la mjadala ni kuona namna gani hizo taratibu za kikatiba na kimkataba zinaweza kuboreshwa.

- Mwalimu aliyekaa miaka 10 shuleni, kila mwaka anaongezewa kazi?

- Unataka tuongezee nyongeza ya ujumla ya mshahara watu ambao hawajaongezewa kazi?

- Si sahihi zaidi tukadai gharama za bidhaa na huduma zishuke bei ili kipato kidogo hicho hicho kitoshe na waTz wote wanufaike?
 
NB: Naenda kunywa chai, mwenye hoja za ziada asubiri nirudi kwanza..
 
Mishahara iongezwe kwa wafanyakazi bei kushuka haiwezi sababu watu wengi wako private sector au kujiajiri uchumi ukiwa unakuwa mahitaji yataongezeka tu maana sijui idadi ya wafanyakazi wa serikali lakini nadhani number ndogo tu watu wa nje ya mfumo wa serikali wakiwa na kipato kizuri mahitaji yataongezeka. Sukari imepanda, mafuta ya kula yamepanda nini sababu? umeme? hapana sababu ni nyngi ndio maana huwezi kuwa na wafanyakazi miaka 5 hakuna ziada na hata madaraja juzi ndio wamenza kupewa haki zao. ongeza mshahara boost spending za watu ila gharama hazipunguzwi sababu ya SGR au umeme wa Rufiji maana hata miaka ya nyuma umeme ulikuwa Mtera lakini mbona huo umeme haukuwa rahisi.
 
Kuongezwa kazi haikufanyi pia kupata nyongeza kuna criteria wanatumia kufanya review ya Job description halafu wanapanga grade.

mfano grade 10 ya mshahara unaanza 10000 mpaka 50000
grade 11 60000-100000

sasa ukiajiriwa kama grade 10 unaweza kupangiwa kuanza kati au chini alfu 10 ila kila mwaka unapanda kutokana na juhudi zako mpaka siku utafika alfu 50 ndio mwisho baada ya hapo labda upate promotion, ukipata unaenda grade 11 alfu 60 then utapanda kila mwaka mpaka 100000 ni hivyo inavyoenda. Sasa mifumo ya mishahara iko mingi inategemea Tanzania wanatumia mfumo gani ila yote inafanana ukiwa unafanya evaluation ya Job Description na hata ukimuongezea mtu majukumu katika grade ileile unafanya evalution kama kazi za ziada inatosha kumpa points aka move grade nyingine au hazitoshi na akabaki hapohapo
 
Mawazo mfu kabisa! We ukiambiwa Wafanyakazi unaelewa wale tu wanaoingia ofisini, sio? Unajua nyuma ya kila mfanyakazi mmoja kuna wategemezi wangapi? Fanya hesabu yako upya!!
 
Labda kulingana na wachumi kuotoka jalalani
 
Mshahara 2015 tshs 230,000 bei za bidhaa mf sukari shs1400. mshahara 2021 tshs 230,000.sukari 2800.huo ni mfano mmoja kati ya mingi iliyopo. Huyo mtumishi unamwambia asiongezewe mshahara uendane angalau na uhalisia wa maisha. Atamuduje maisha aweze kutimiza wajibu wake?
 
Huyo mtu ni much know tu! Hakuna anacho kielewa! Yeye amekaza shingo tu eti wafanyakazi waongezewe kazi! Sijui ni kazi gani hiyo anayo taka waongezewe!

Maisha ya kukariri ni mabaya sana! Wengi wasio wafanyakazi, wanaumia sana kusikia/kuona wafanyakazi wanadai haki zao! Wivu tu na chuki vimewajaa!
 
Tupambane bei ya sukari ishuke, miwa ipo, mahitaji yapo, hatushindwi, na si bidhaa zote zimepanda kwa kasi hiyo, sukari na mafuta ya kula ni special case; ila kikubwa ninachosema, tudai tija katika uzalishaji ili bei zishuke
 
Hasa kichaa yule wa chato ambaye amenyakuliwa mawinguni, wakati yeye alikua anahonga hadi ukuu wa wilaya na ukurugenzi ili wapate maslahi lakini kwa wengine alikua anaona kuwaongezea mshahara ni anasa rot in hell

Umesahau na yule anaye sema kodi ya simu kwa siku 1000 kupamdisha uchumi umesahau kweli tuna watu wa ajabu nchi hii hakuna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…