Ryan The King
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 2,788
- 2,690
Nawasalimu kwa lugha zenu, ishara na mitindo mbalimbali ya salamu zenu kwa kuzingatia umri, elimu, tamaduni mitazamo, falsafa na Itikadi Zenu.
Nafurahishwa na uwepo wenu katika jukwaa hili, basi na iwe furaha kwenu kama ilivyokuwa desturi kwangu.
Nikirudi kwenye Mada;
Maisha ni uwepo wa ukinzani baina ya mambo mawili yasiyofanana. Huu ni mtazamo wangu kulingana na jinsi nilivyotafakari. Bila kuwa na ukinzani basi ni wazi hakuna maisha.
Ukinzani ni kitendo cha mambo mawili kutokubaliana katika jambo moja. Ukinzani huu umenifanya nitoe kanuni ambayo nimeiita "UWILI".
Bila kuathiri kanuni za asili na zile za kibinadamu, kanuni hii ya Uwili ndio inafanya maisha yaweze kuendelea.
Je kuna wakati ulijiuliza moja ya maswali yafuatayo:-
1- kwa nini kuna nyuma na mbele, Juu na chini, mashariki na Magharibi, Jinsia ya kike na kiume, Wema na ubaya nakadhalika.
2- Je kungekuwaje ikiwa kanuni hizi za Uwili zisingekuwapo?
Ukweli ni kuwa hakuna maisha bila Kanuni ya Uwili.
Kanuni hii ndio huleta maana kamili ya dhana nzima ya Maisha. Kanuni hii ndio humfanya kiumbe katika ulimwengu wa nje kuwa jinsi alivyo japokuwa katika Ulimwengu wa ndani yaani wa kiroho kanuni hii hafanyi kazi.
Maisha ni vile mtu alivyo, ajionavyo, alivyonavyo, Pamoja na vile na wale wanaomzunguka. Hii huweza kuwa maana kamili ya dhana ya Maisha.
Hakuna maisha zaidi ya jinsi mtu alivyo, ajionavyo na mazingira yake.
Hivyo hatuwezi kutamani au kutafuta mambo yaliyo nje ya uwezo wetu.
Ikiwa mtu atataka mambo yaliyo nje ya uwezo wake basi hujitafutia matatizo yake mwenyewe katika Ulimwengu huu unaoonekana, hivyo kuathiri baadhi ya Elementi za Ulimwengu wa ndani kama Furaha, amani, na Upendo(Kanuni chanya za rohoni). Na Elementi hizi zikiharibiwa mtu huyo hujikuta katika maradhi ya mwili ambayo huweza kudhani amelogwa.
Pia kama mtu atafanya mambo chini ya kiwango chake basi matokeo huweza kuwa mabaya kuliko ya yule aliyetenda juu/nje ya uwezo wake.
MAISHA NI MTAZAMO, NJIA, MATOKEO
Mtu huweza kuwa na mtazamo Chanya lakini hutumia njia hasi hivyo hupata matokeo mabaya.
Mtu fulani ataungana na Mimi kuwa, watu wengi ukiwauliza jambo lolote katika kufanikiwa katika maisha, huwa mawazo mazuri, maono, na mitazamo ya faida lakini ukiyaangalia maisha yao utashindwa kushangaa jinsi Ufukara ulivyowapiga.
Pia Mtu huweza kuwa na mitazamo hasi lakini hutumia njia Chanya na mwishowe kupata matokeo mazuri.
Ikumbukwe kwamba Mitazamo huathiri Njia au mbinu, na hakuna mahusiano ya moja kwa moja baina ya Mitazamo ya Maisha na Matokeo yake katika Maisha. Bali kuna uhusiano wa njia na Matokeo.
Maisha huongozwa na kanuni ya UWILI.
Nafurahishwa na uwepo wenu katika jukwaa hili, basi na iwe furaha kwenu kama ilivyokuwa desturi kwangu.
Nikirudi kwenye Mada;
Maisha ni uwepo wa ukinzani baina ya mambo mawili yasiyofanana. Huu ni mtazamo wangu kulingana na jinsi nilivyotafakari. Bila kuwa na ukinzani basi ni wazi hakuna maisha.
Ukinzani ni kitendo cha mambo mawili kutokubaliana katika jambo moja. Ukinzani huu umenifanya nitoe kanuni ambayo nimeiita "UWILI".
Bila kuathiri kanuni za asili na zile za kibinadamu, kanuni hii ya Uwili ndio inafanya maisha yaweze kuendelea.
Je kuna wakati ulijiuliza moja ya maswali yafuatayo:-
1- kwa nini kuna nyuma na mbele, Juu na chini, mashariki na Magharibi, Jinsia ya kike na kiume, Wema na ubaya nakadhalika.
2- Je kungekuwaje ikiwa kanuni hizi za Uwili zisingekuwapo?
Ukweli ni kuwa hakuna maisha bila Kanuni ya Uwili.
Kanuni hii ndio huleta maana kamili ya dhana nzima ya Maisha. Kanuni hii ndio humfanya kiumbe katika ulimwengu wa nje kuwa jinsi alivyo japokuwa katika Ulimwengu wa ndani yaani wa kiroho kanuni hii hafanyi kazi.
Maisha ni vile mtu alivyo, ajionavyo, alivyonavyo, Pamoja na vile na wale wanaomzunguka. Hii huweza kuwa maana kamili ya dhana ya Maisha.
Hakuna maisha zaidi ya jinsi mtu alivyo, ajionavyo na mazingira yake.
Hivyo hatuwezi kutamani au kutafuta mambo yaliyo nje ya uwezo wetu.
Ikiwa mtu atataka mambo yaliyo nje ya uwezo wake basi hujitafutia matatizo yake mwenyewe katika Ulimwengu huu unaoonekana, hivyo kuathiri baadhi ya Elementi za Ulimwengu wa ndani kama Furaha, amani, na Upendo(Kanuni chanya za rohoni). Na Elementi hizi zikiharibiwa mtu huyo hujikuta katika maradhi ya mwili ambayo huweza kudhani amelogwa.
Pia kama mtu atafanya mambo chini ya kiwango chake basi matokeo huweza kuwa mabaya kuliko ya yule aliyetenda juu/nje ya uwezo wake.
MAISHA NI MTAZAMO, NJIA, MATOKEO
Mtu huweza kuwa na mtazamo Chanya lakini hutumia njia hasi hivyo hupata matokeo mabaya.
Mtu fulani ataungana na Mimi kuwa, watu wengi ukiwauliza jambo lolote katika kufanikiwa katika maisha, huwa mawazo mazuri, maono, na mitazamo ya faida lakini ukiyaangalia maisha yao utashindwa kushangaa jinsi Ufukara ulivyowapiga.
Pia Mtu huweza kuwa na mitazamo hasi lakini hutumia njia Chanya na mwishowe kupata matokeo mazuri.
Ikumbukwe kwamba Mitazamo huathiri Njia au mbinu, na hakuna mahusiano ya moja kwa moja baina ya Mitazamo ya Maisha na Matokeo yake katika Maisha. Bali kuna uhusiano wa njia na Matokeo.
Maisha huongozwa na kanuni ya UWILI.