Dharau kubwa, waziri wa CCM anawaza simu za mkopo wakata taifa lina shida ya maji na umeme kila kona

Dharau kubwa, waziri wa CCM anawaza simu za mkopo wakata taifa lina shida ya maji na umeme kila kona

Kamanda Asiyechoka

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2020
Posts
3,315
Reaction score
5,058
CcM imejaa tabu na matatizo
👇
Screenshot_20230107-144357.jpg
 
Yeye ndio waziri wa umeme na maji? Au tuziunganishe ziwe pamoja? Mtandao wa maji ujumuishwe na wasimu na wauchukuzi kwa ajili kuchukulia maji?

Kila wizara ina waziri wake ana bajeti yake, sera, sheria, kanuni nk

Ni wajibu wa kila waziri kutimiza majukumu yake ktk wizara yake, labda wafanye kama lile zoezi la wizara kuungana pamoja kwenda kutatua kero za wananchi
 
Shida ya Maji na umeme kila kona?.. wengine toka mwaka mpya hatujapata shida ya Maji wala umeme...
Wapi mnapokaa nyinyi kuna shida hizo?
 
Yeye ndio waziri wa umeme na maji? Au tuziunganishe ziwe pamoja? Mtandao wa maji ujumuishwe na wasimu na wauchukuzi kwa ajili kuchukulia maji?

Kila wizara ina waziri wake ana bajeti yake, sera, sheria, kanuni nk

Ni wajibu wa kila waziri kutimiza majukumu yake ktk wizara yake, labda wafanye kama lile zoezi la wizara kuungana pamoja kwenda kutatua kero za wananchi
Unajua maana ya serikali?
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpatieni... Mheshimiwa Waziri anahangaikia sekta yake... maswala ya maji na umeme waulizwe WaTanga...pia tumshauri Mheshimiwa Waziri kwamba hiyo huduma anayotaka iletwe nadhan hajaelewa jinsi inavyofanya Kazi kwa nchi zilizoendelea...wateja nchi hizo hawakopeshwi simu tuu kwa matakwa au ombi la Waziri...wao wanakopesheka kutokana na kipato au ajira endelevu.. lakini pia waki-default ni rahisi sana kuwafuatilia kwani wanajulikana wanapoishi na kufanya Kazi kutokana na kuwa na makazi na anuani rasmi...sasa huku kwetu bwana Waziri milingoti ya mitaa tuu imeshindikana, wananchi asilimia zaidi ya 90 wanaishi makazi holela(unplanned)...Watumiaji zaidi ya 80% wa huduma za simu hawana ajira rasmi,sasa hakuna kampuni yoyote ya kibiashara itakuwa tayari kuchukua risk ya kuwakopesha watu ambao ni ngumu sana kuwadai.... nadhan Mh.Waziri ashauriwe, atilie mkazo kutengeneza physical addresses nchi nzima na atumie ujumbe wake wa Baraza la Mawaziri kuishauri Serikali kupitia wizara ya Ardhi na Mipango iwekeze katika kutengeneza mpango kabambe wa matumizi Bora ya ardhi ili sasa iwe ni rahisi kusambaza huduma anazotaka na nyingine muhimu kwa wananchi ambao yeye na watumishi wenzake wa kada Mbali mbali wamepewa dhamana ya kuwahudumia.
 
Simu ya mkopo unalipa kidogokidogo then bundles bei juu, ina maana gani sasa?
Maana yake ni kwamba 'wajinga ndio waliwao'
Hapo wanataka kuzidi kukukamua wananchi wanyonge kupitia tozo za miamala na bando za simu.

Yaani bora mtu ukose mali upate akili (maarifa).

Sijawahi kukopa simu na sitakaa niwaxe kukopa simu, labda kama hiyo simu naitumia kuzalisha au kuendesha biashara. Kama sina smart, ntatumia kiswaswadu vipo hadi vya elfu 10.

Na kwa mpango huu, tusahau kuhusu kutetea vijana kuhusiana na kamari (betting) za mitandaoni. Watu wanaliwa hafi basi. Mtu ancheza hadi laki 1 anapata elfu 20??hahahahaaaaa, ahaaaaaa!
 
CcM imejaa tabu na matatizo
👇
View attachment 2472044
We kweli mbumbumbu ndiyo maana hata mwalimu wako alishindwa kukufundisha. Hizo sekta ulizozitaja hazina mawaziri? Hata somo la Uraia ulishindwa kuielewa? Hakuna waziri wa Maji? Hakuna waziri wa Nishati? Nape aongelee mambo ya maji na umeme yanamhusu? Kijana rudi darasani ndiyo shida za kusoma shule za kata nyie ni bomu la ujinga nchi hii. Nape ni waziri wa Mawasiliano,Habari na Teknolojia anaongelea mambo yanayohusu sekta yake. Eti waziri wa CCM, kuna wizara inaitwa CCM? hata km mtu humpendi au hupendi chama chake tumia akili kuandika jambo lenye mantiki. Chuki ni mzigo mzito sana kuubeba
 
Shida ya Maji na umeme kila kona?.. wengine toka mwaka mpya hatujapata shida ya Maji wala umeme...
Wapi mnapokaa nyinyi kuna shida hizo?
Njiro
Jana wamekata
Saa nne asbh mpaka saa 11 nasepa haujarudi.
 
Simu ya mkopo unalipa kidogokidogo then bundles bei juu, ina maana gani sasa?
Hivyo ni vitu viwili tofauti. Unataka ununuliwe na bando? Mbona makampuni ya simu yanakopesha bando? Km umekata tamaa jitundike tu umsalimie Magu. Maisha ya kwako kila kitu unataka upate wa kumlalamikia!
 
😂😂

Ndio tatizo la kupeana vyeo kwa ubini
 
Back
Top Bottom