Dharau za wafanyakazi wa Tanesco dhidi ya wananchi, Waziri husika chukua hatua.

Dharau za wafanyakazi wa Tanesco dhidi ya wananchi, Waziri husika chukua hatua.

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Wakazi wa moja ya mitaa Mbagala Rangitatu hawana umeme tangu jana asubuhi mpaka muda huu ninapoandika hii Post. Wakazi hawa wapo mita mia tano toka ofisi ya Tanesco Mbagala na mita miambili toka Sub Station ya Mbagala, hata hivyo walishinda na walilala bila umeme kwa zaidi ya saa ishirini na nne japo kila wakipiga simu Tanesco jibu ni taarifa tunayo na mafundi wapo saiti!
Wakazi hawa wanapata umeme toka kwenye transifoma ambayo inasambaza umeme kwenye mitaa mingine ambayo imeendelea kupata umeme.
Wanaoishi pembeni mwa hiyo transifoma wana sema kuna kipande cha waya kilikatika asubuhi ya jana ndipo umeme ulipozima hata hivyo toka jana hakuna mafundi waliofika kutatua tatizo hilo toka jana mpaka leo licha ya kupewa taarifa mapema, hali hii ni ya kawaida kwa mafundi wa Tanesco kudharau taarifa za wananchi.
 
Huwa wanalipwa posho wakienda Kazi za mbali , Sasa Kwa sababu ninyi mpo karibu ndo shida. Ninyi kuwa karibu na tanesco kwao ni hasara. Ndiyo maana hawajaja na hawatakuja.
 
Huwa wanalipwa posho wakienda Kazi za mbali , Sasa Kwa sababu ninyi mpo karibu ndo shida. Ninyi kuwa karibu na tanesco kwao ni hasara. Ndiyo maana hawajaja na hawatakuja.
Baada ya kuwafuata walikuja na kazi iliwachukua dakika tano kuikamilisha huku sisi tukitimiza saa 38 bila umeme.
TANESCO NI TAJIRI JEURI.
 
Wakazi wa moja ya mitaa Mbagala Rangitatu hawana umeme tangu jana asubuhi mpaka muda huu ninapoandika hii Post. Wakazi hawa wapo mita mia tano toka ofisi ya Tanesco Mbagala na mita miambili toka Sub Station ya Mbagala, hata hivyo walishinda na walilala bila umeme kwa zaidi ya saa ishirini na nne japo kila wakipiga simu Tanesco jibu ni taarifa tunayo na mafundi wapo saiti!
Wakazi hawa wanapata umeme toka kwenye transifoma ambayo inasambaza umeme kwenye mitaa mingine ambayo imeendelea kupata umeme.
Wanaoishi pembeni mwa hiyo transifoma wana sema kuna kipande cha waya kilikatika asubuhi ya jana ndipo umeme ulipozima hata hivyo toka jana hakuna mafundi waliofika kutatua tatizo hilo toka jana mpaka leo licha ya kupewa taarifa mapema, hali hii ni ya kawaida kwa mafundi wa Tanesco kudharau taarifa za wananchi.
Habari Hismastersvoice, ahsante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na tunaomba radhi kwa kuchelewa kwa huduma, tunashauri wakati mwingine changamoto hiyo itakapojitokeza, tafadhali wasilisha kupitia inbox (DM) yetu au kwa kututagi TANESCO ili tuweze kuipokea kwa haraka kwa ajili ya utekelezaji. ^GK
 
Hii nchi hatuko huru. Ndiyo maana wananchi wanapuuzwa na kutawaliwa na raia wa Zanzibar (kumbuka Zanzibar ni nchi)
 
Back
Top Bottom