Diamond aachia wimbo mpya: Nitampata Wapi? - Nov 20, 2014

el nino

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2013
Posts
4,712
Reaction score
5,058
Mwanamuziki nguli wa miondoko ya Afro pop ukanda wa afrika mashariki Nasib Abdul Juma ama "Diamond" amewafurahisha mashabiki wa muziki mzuri baada ya kutangaza kuachia ngoma yake katika media za tz zote hapo kesho kuanzia saa nne huku vituo vya kimataifa vikipata nafasi ya kuuonyesha exclusive kuanzia leo hii ...

Wimbo huo utakuwa ukiitwa "nitampata wapi" ' wafuatiaji wa maswala ya Burudani wameshangazwa na Dimond kuamua kutoa ngoma kwa haraka wakati mdogomdogo ikiwa bado ipo kwenye nafasi za juu katika chati na kumbi za starehe mjini hata hivyo inatabiriwa Diamond atajivunjia rekodi yake ya kutwa tuzo saba aliyoiweka mnamo mwaka 2014 kutokana na mafanikio makubwa zaidi aliyoyapata ambayo hayajawahi kufikiaa na msanii yeyote katika historia ya muziki wa Bongofleva.




Video ya wimbo "Nitampata Wapi"


 
Last edited by a moderator:
sio mbaya tunavsubiri kwa hamu,ila mkuu hii mada tayari ipo ndani ya ile special thread ya diamond fans' ingekua vyema kama ungekuja kutupa updates kule ndani.

Mashairi ya wimbo ' Nitampata wapi?'

[h=2][/h]
Sura yake mtaratibu, mwenye macho ya aibu. Msahau majaribu ila namkumbuka sanaa
Umbo lake mahabibu, kwenye maradhi alinitibu, siri yangu kaharibu. Bado namkumbuka sanaa

Alienifanya silali jua kali nimtafute tukale, lakini hata hakujali mentali akatekwa na wale....X2

Kiitikio...

Nitampata wapi kama yule nampendaga sana X2
Nitampata wapi kama yule ananipendaga sana x2

Beti 2

ai nyota, nyota ndio tatizo langux2, ai nyota mpaka nalia peke yangu
ai nyota, nyota ndio shida yangu.X2
Nyota wamenizidi wenzangu,

alidanganywa na wale,wenye pesa nyumba gari, mi kapuku hakujali akanikimbia x2

alonifanya silali jua kali nimtafute tukale lakini wala hakujali mentali akatekwa na wale.

Kiitikio

Bado ananijia ndotoni,ila nikiamka simwoni.x2
Bado ananijia nikilala, haki ya Mungu sio masihara. X2

Hii ni sauti ya Rais iliyomshindaga ibilisi, kwa mwanadamu sio rais,.
Na umwambie
lazima ujue kutofautisha kati ya jumlisha na msalaba, x na zidisha.x2

Bado namuota nikilala haki ya Mungu sio masihara
 


Video ya wimbo wa Diamond (ntampata wapi) ishakamilika na kabla haijaanza kuoneshwa rasmi katika vituo vya nyumbani,tayari vituo vya nje vimeanza kuionyesha na kuitambilisha, jana ilichezwa Trace tv na leo imetambulishwa kwenye kituo cha mtv base,lakini pia imechezwa kwenye tv za Nigeria ikiwemo sound city tv.

Ni utaratibu wa Diamond kuachia video na audio kwa pamoja ,ambapo kesho ndio vitaachiwa rasmi hapa nyumbani...
kwa wasiofahamu nyimbo ya ntampata wapi ni moja ya nyimbo kibao za Diamond anazorekodi kila siku aingiapo studio na nyimbo hii alianza kuitease instagram miez michache iliyopita.
 

Attachments

  • Mtv.jpg
    48.2 KB · Views: 19,484
  • Mtv2.png
    120.2 KB · Views: 1,693
Naona nyumbani keshaona miyeyusho kweli FIESTA ni sheeeeeeeeeedahhh

Na wao watakapoamua kumuyeyushia asithubutu kutuletea kelele za akina lady jay dee, mara ooh nyimbo zangu hazichezwi kwenye media za nyumbani... kwani kaamua kuwadharau na kuona sio wa muhimu tena wakati ndio waliompandisha chati.
 
Ungeandka mwanamzki mkali na sio nguli..

Nguli ni legend,kitu ambcho diamond hajafkij

We unahisi kuw legend mpaka uwe na mvi...mpaka sasa kwa mafanikio ya Dimond teyri ni legend
 
Wale wapenz wa chibu kaeni mkao wa kula kitu kipya is about to be released sooooon........japo wengine tushakiskia tayari NICE WORK DIAMOND👏
 

Attachments

  • 1416459972993.jpg
    70.3 KB · Views: 1,111
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…