Hii ni tahadhari kwetu haswa tunaoshabikia mambo ya hovyoWewe ndio unazidi kumpa kiki hapa
Mwacheni Almasi wetuuu..
amejikamatisha makusudi ili naye aandikwe hahahahha. Kweli amefuliaBaada ya fununu na malalamiko mengi hatimaye Diamond nae kaitwa kutoa maelezo polisi.
Hata hivyo,bado haijafahamika kaitwa kwa tuhuma gani.
Tetesi ni kwa kosa la kuendesha gari huku akicheza wimbo wa Marry you na kuachia usukani akiwa na familia yake kwenye gari,au tuhuma za madawa ya kulevya zinazomuandama.
Swali ni je,Diamond nae atalala kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani kama wenzie?
My take; kama ni suala la madawa ya kulevya basi WCB wengi wana tuhuma za madawa ya kulevya.
Wakiwemo Dansa Mose Iyobo,Queen Darling na Shetta.
Haki itendeke na sio janjajanja za kuitwa polisi na kuachiwa ili kutufunga midomo tuliokuwa tunapiga kelele.
Nifah
=======
UPDATES;
=======
View attachment 470944
Si kweli kwamba Diamond aliitwa kuhojiwa sababu ya kujihusisha na Madawa ya Kulevya, Bali aliripoti Polis baada ya Video yake kusambaa ikimuonesha akivunja sheria za barabarani.
Haya ndio Maneno aliyoyaandika Diamond...
View attachment 470892
Leo nilireport kituo kikuu cha polisi wa usalama barabarani kutokana na Vidoe Clip tuliyopost naendesha gari barabarani bila kufunga mkanda na pia kuachia usukani na kucheza.... Nikapewa Onyo na Kulipa faini kulingana ya Mujibu wa sheria... Tafadhali watanzania na Vijana wenzangu...
Tuhakikishe tunafunga mikanda pindi tupandapo na tuendeshapo Magari Maana ni Hatari kwa Maisha yetu na inaweza kukupeleka kunyea debe pia..
Pole sana mkuu kwa maandishi ni jinsi gani umeumia kwa kitendo alichofanya braza chibuMimi ni mshabiki wa muziki wa Bongo fleva na pia mshabiki mzuri wa Diamond. Najua nitakera watu wengi lakini kwenye ukweli wengi watanielewa ni kitu gani namaanisha.
Labda Diamond hajitambui kama yeye ni mwanamuziki mkubwa na anastahili kuwa na matendo mema kwa jamii. Sote tunajua kila tukio laa Diamond ni lazima vyombo vya habari viliandike. Hata kama akiachia ushuzi, lazima magazeti yataandika!! Nimesikitishwa sana na tendo la Diamond kukamatwa na Polisi wa Usalama Barabarani. Yaani mwanamuziki mkubwa kama yeye anafanya tukio la kuendesha gari barabarani huku ameuachia usukani na kucheza muziki!!
Sote ni mashahidi na tuliona jinsi ule wimbo wa Darassa ulivyoleta zahma kwa wale Vijana wa Singida. Hawa vijana walikwenda mung'anda na kunyea debe. Sijui hatma yao ikoje mpaka hivi sasa. Walifanya lile tukio kwa mzuka wa ule muziki wa Darassa na kwa bahati mbaya mwenye wimbo hakushirikishwa kabisa kwenye lile tukio. Darassa hakujua na wala hakuwatuma katika kuandaa lile tukio, hakutaka kutumia mbinu chafu ili kuupa kiki wimbo wa "Muziki". Ule wimbo ulijiuza wenyewe kwa kuwa unavionjo vya kupandisha mzuka, wimbo umepangwa kiufasaha.
Leo Diamond anafanya tukio la ajabu ili kuupa kiki muziki wake. Anahatarisha maisha ya watumiaji wengine wa barabara na familia yake ambao wote walikuwepo ndani ya gari wakati akilifanya hilo tukio. Lengo lake ni kuupa 'extra mile' wimbo wake wa "Marry You".
Hivi wimbo wake umekwama kuwavutia mashabiki mpaka anaamua kutafuta mbinu za ajabuajabu ili kuupa kiki wimbo wake? Atambue waungwana wanasema kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.
Kwa hili tukio la kujitakia alistahili adhabu kali zaidi ya wale vijana wa Singida ili kuukomesha kabisa mtindo huu wa kuhatarisha maisha yake na viumbe wengine.
Si kwamba naandika ili kumkwamisha. Au namchukia. La hasha. Lengo ni kuwaasa wengine wasifanye mzaha au mambo ya ajabu ili kutafuta sifa za kijinga ili kutafuta umaarufu au kuongeza idadi ya mashabiki. Najua kuna watu hawatopenda haya maneno, lakini kwenye mambo yasiyofaa tuambizane ukweli!!
Mpinga nae anatafuta kutambulika njee hapo kafurahiii anaenda kung'aa kwenye mitandao na platnam