Diamond anafanya biashara gani?

Diamond anafanya biashara gani?

Joined
Aug 16, 2016
Posts
43
Reaction score
56
Makala ya Raia Mwema lina habari ya kufikirisha kidogo:

Mwandishi anauliza " Diamond ana fedha, lakini anauza nini?"
Hata mimi nimejikuta nikiuliza swali hili mara nyingi tu bila majibu. Wengine wanasema anauza matangazo, wengine ana studio nk. Lakini vipi ile biashara yake ya msingi : Muziki?

soma mwenyewe hapa chini:
======

NASEEB ABDUL ‘Diamond Platnumz’ ananivutia sana miongoni mwa wasanii wa muziki wa nyumbani. Ananivutia kumsikiliza na kumtazama kwenye TV.

Akiwa ananengua jukwaani unaweza kujisemea kwanini asiwe ananengua na aachache na kuimba. Akianza kuimba bado utajisemea tena kwanini asiwe anaimba pekee na si kuchanganya vitu viwili kwa wakati mmoja?

Huyu ndiye Diamond ambaye anafanya vitu viwili kwa wakati mmoja na kuvutia wengi. Wapo wanaompenda kwa kuimba na wako wanaompenda kwa kucheza.

Amejivutia mashabiki wengi kwenye maeneo hayo mawili jukwaani. Kazi zake zimemfanya hivi sasa atajwe kama msanii anayetengeneza fedha nyingi zaidi hapa nchini.

Wingi wa fedha hizo zimefanya afungue kampuni ya WCB, inayofanya kazi za kusimamia wasanii mbalimbali.

Lakini mpaka unapoweka umakini wako kusoma andiko hili, fahamu Diamond amewahi kutoa albamu moja tu ya Nenda Kamwambie mwaka 2009.

Hii ni albamu yake ya kwanza na ya mwisho mpaka wakati huu 2016. Ni takribani miaka saba sasa imepita tangu atoe albamu hiyo ambayo haikuwa na idadi kamili ya nakala alizouza.

Inakuwaje Diamond, anayetajwa kuwa msanii mwenye fedha nyingi, awe ametoa albamu moja tu kwa zaidi ya miaka saba?

Ina maana Nenda Kamwambie ndio imemlipa kiasi hiki mpaka sasa aamue asitoe albamu nyingine?

Wanamuziki, bendi na vikundi duniani kote wanaonyesha na kutangaza utajiri wao kupitia mauzo ya kazi zao ambazo zinakuwa albamu.

Hata Ali Kiba, anayekinzana naye kimuziki aliwahi kusema albamu yake ya kwanza ya Cinderella ilivunja rekodi na kuuza ‘double platinum’ kwa kuuza nakala milioni mbili.

Mauzo ya nakala hiyo anadai yalimuingizia shilingi milioni 200. Kiba aliwahi kusema hata ukimya wake kwenye sanaa haukumfanya apumzika bure, bali alikuwa na ‘jembe’ lililofanya akae pembeni kidogo.

Kwenye dunia ya sasa, wasanii wa muziki wanayo nafasi ya kulipwa au kujiingizia pesa kutokana na vyanzo mbalimbali na hiyo yote ni kutokana na muziki wao na ndiyo maana sio kitu kigeni tena kuona msanii analipwa pale nyimbo zake zinapochezwa redioni.

Hii ni sheria inayotumika kwa baadhi ya nchi duniani, japo nyumbani haijaanza kutumika. Inawezekana sheria hii ingekuwepo nyumbani Diamond, angeingiza fedha zaidi.

Swali kubwa ambalo nimekuwa nikijiuliza ni hili; Diamond na wasanii wetu wengine ambao hawajawahi kutoa albamu wanapata wapi fedha za kuendeshea maisha yao ya kifahari wakati mauzo ya albamu zao ni sifuri?

Biashara ya muziki ni sawa na nyingine yoyote iwe ya kuuza barafu, mikate, machungwa au magari. Mfanyabiashara wa magari, hesabu yake hutokana na idadi ya magari anayouza. Vivyo hivyo kwa biashara nyingine.

Hawa wasanii wetu ambao hawauzi muziki, wanapata wapi fedha za kuendeshea maisha yao? Muziki bila kutoa albamu ni biashara gani?

Nafahamu kuna maonyesho mbalimbali ambayo baadhi yao wanapata. Lakini, msanii ambaye kwa mwezi anapata maonyesho manne yenye thamani ya shilingi milioni sita hadi nane; anawezaje kutoa video ambazo tunaambiwa zina thamani ya milioni 30?

Hizi hela za kutengeneza video za milioni 30 wanapata wapi wakati hawana albamu hata moja? Wanauza nini?

Vanessa Mdee ‘Vee Money’ anapokea pesa nyingi nje ya nchi kutokana na nyimbo zake kuchezwa kwenye Radio na runinga za Afrika Kusini. Katika taifa hilo, vituo vya redio na luninga huwalipa wasanii kwa nyimbo wanazozipiga ingawa hilo si kwa wasanii wote.

Kwa mfano, wasanii wanaotoka nje ya nchi kuna vigezo vinatazamwa kukuwezesha kusajiliwa na mamlaka husika na baada ya hapo unakuwa kwenye mzunguko wa kulipwa kama wasanii wengine wa nchi hiyo wanavyolipwa.

Wasanii wote maarufu duniani kama vile Chris Brown, Rihanna, Eminem, Wiz Khalifa na wengine wote wanafahamika kwa kuuza albamu zao.

Hadi leo, Michael Jackson anafahamika kwa kuuza nakala milioni 100 za albamu yake ya Thriller iliyotoka kwenye miaka ya 1980.

Kwenye biashara ya muziki, hakuna msanii aliyetengeneza fedha kwa sababu ya Fiesta au matamasha ya Kili Tour. Msanii anapata fedha kwanza kupitia albamu anazotoa.

Tunafahamu mazingira yaliyosababisha wasanii wetu waachane na utaratibu wa kutengeneza albamu. Kinachotakiwa kufanyika ni kupambana kuhakikisha kuwa mazingira yanaboreshwa ili wasanii wapate wanachostahili kwenye mauzo ya albamu zao kwanza.

Vinginevyo swali langu hili halitaisha. Diamond anapata wapi fedha za kufanya anayoyafanya wakati albamu yake ya mwisho ilitoka miaka saba iliyopita?
 
Album hazilipi si kama zamani nilimsikia master Jay akihojiwa alisema kwa sasa soko la album halilipi, ila watu wanatoa kwa ajili ya kuipa hadhi na heshima mziki wake basi, zinazolipa sana ni tour na ndio maana msanii akitoa album faster tour zinaanza , ila soko album halilipi, labda hizo ring tone, ela inayotokana na airplay basi lkn TOUR ndio mpango mzima. Diamond platnumz mwaka huu amepiga show nyingi alikuwa na tour ulaya na sasa anatour ya Africa, tusiwe na mawazo kila anayefanikiwa ni muuza ngada au freemason kwani hayo ni mawazo ya kimasikini.
 
Album hazilipi si kama zamani nilimsikia master Jay akihojiwa alisema kwa sasa soko la album halilipi, ila watu wanatoa kwa ajili ya kuipa hadhi na heshima mziki wake basi, zinazolipa sana ni tour na ndio maana msanii akitoa album faster tour zinaanza , ila soko album halilipi, labda hizo ring tone, ela inayotokana na airplay basi lkn TOUR ndio mpango mzima. Diamond platnumz mwaka huu amepiga show nyingi alikuwa na tour ulaya na sasa anatour ya Africa, tusiwe na mawazo kila anayefanikiwa ni muuza ngada au freemason kwani hayo ni mawazo ya kimasikini.

Mkuu joseph1989 , kwani kuna watu wanasema anasukuma ngada?
 
Kuna sehemu umesema ali kiba baada ya kutoa album yake ya cinderella na kufanya poa alikaa kimya kwenye sanaa ila alikuwa na jembe linalomuingizia sasa je wew toka umemsikia diamond ameanza mziki umewahi ona amekaa kimya hilo ndilo jembe lake linalompa mavuno mwisho wa siku na yeye akikaa kimya ujue kapata jembe jingine litalopelekea kupata mavuno.
 
Nilijua tu Chanzo lazima kitakuwa DAR.

Waandishi na Aibu ya Taaluma.
Waandishi wengi wa habari wanashindwa kuielewa,wao waangalie mfano kwa Madaktari
Wote wataitwa Madokta,ila kila mmoja ana specific profession yake.
Ila waandishi wetu hawa,unakuta mwandishi kama daladala,yaani yeye anaandika chochote tu bila kujua uwezo wake.

Mwaandishi wa Taaluma ya Michezo na Burudani(Sanaa kwa ujumla)lazima awe amesomea Sanaa,na Chuo Kikuu cha Dar wanatoa Degree ya masuala hayo kama sikosei,na kama nakumbuka vizuri Marehem Mzirai alikuwa anasoma Pale.Na Chuo cha Bagamoyo kinatoa Kozi nzuri sana ya masuala ya Sanaa na Uchumi,ambapo utashangaa pale unakuta Wazungu wanasoma ila waswahili na waandishi na wasanii wanapita kama polisi,wanenda kwa warsha tu na vi seminar vya kuzugia ili wapate certificate of attendance

Sasa Mwandishi lazima awe na taaluma.Sasa kwa akili ya kawaida,hivi unashindwa kufanya analysis tangu alipotoka Diamond mpaka leo hii na mafanikio yake?
-Na sio lazima kila biashara mtu aweke wazi,yale ni maisha binafsi,kuna watu humu hata wake zao na waume zao hawajui anapokea kiasi gani kama Mshahara.Na ni mwili mmoja,sasa itakuwa Diamond?

Maisha yanaanza kwa Shilingi moja,then inategemea umeiwekeza vipi.Wapo watu walianza na pesa za madafu tu tena milioni moja tu,leo hii ni milioneaz wakubwa na tunawaheshim.

Diamond ana nidham kubwa sana ya Pesa tena Sana.
Kwa mtizamo wa haraka unaweza kushangaa kwanini Diamond Jina kubwa halafu anahitaji Management?Jibu moja tu ni kwamba anajtambua na anajifunza kwa Wenzie Nje ya Nchi

Hivi Unajua Billionea Dangote,ni maarufu sana Nigeria,ila kuna watu wanaishi Lagos-Nigeria,hawajui kwamba Anakiwanda cha Cement Tanzania.
Sasa maisha ni akili,sio kila kitu mtu anadi.
Big UP Diamond,licha ya kwamba kanikera kuimba Nyimbo ya matusi matupuuu ya Salome(usiingie huku Diamond,matusi matupu hayo jua ni soft copy na mungu yupo na unaiacha milele).
 
Nilijua tu Chanzo lazima kitakuwa DAR.

Waandishi na Aibu ya Taaluma.
Waandishi wengi wa habari wanashindwa kuielewa,wao waangalie mfano kwa Madaktari
Wote wataitwa Madokta,ila kila mmoja ana specific profession yake.
Ila waandishi wetu hawa,unakuta mwandishi kama daladala,yaani yeye anaandika chochote tu bila kujua uwezo wake.

Mwaandishi wa Taaluma ya Michezo na Burudani(Sanaa kwa ujumla)lazima awe amesomea Sanaa,na Chuo Kikuu cha Dar wanatoa Degree ya masuala hayo kama sikosei,na kama nakumbuka vizuri Marehem Mzirai alikuwa anasoma Pale.Na Chuo cha Bagamoyo kinatoa Kozi nzuri sana ya masuala ya Sanaa na Uchumi,ambapo utashangaa pale unakuta Wazungu wanasoma ila waswahili na waandishi na wasanii wanapita kama polisi,wanenda kwa warsha tu na vi seminar vya kuzugia ili wapate certificate of attendance

Sasa Mwandishi lazima awe na taaluma.Sasa kwa akili ya kawaida,hivi unashindwa kufanya analysis tangu alipotoka Diamond mpaka leo hii na mafanikio yake?
-Na sio lazima kila biashara mtu aweke wazi,yale ni maisha binafsi,kuna watu humu hata wake zao na waume zao hawajui anapokea kiasi gani kama Mshahara.Na ni mwili mmoja,sasa itakuwa Diamond?

Maisha yanaanza kwa Shilingi moja,then inategemea umeiwekeza vipi.Wapo watu walianza na pesa za madafu tu tena milioni moja tu,leo hii ni milioneaz wakubwa na tunawaheshim.

Diamond ana nidham kubwa sana ya Pesa tena Sana.
Kwa mtizamo wa haraka unaweza kushangaa kwanini Diamond Jina kubwa halafu anahitaji Management?Jibu moja tu ni kwamba anajtambua na anajifunza kwa Wenzie Nje ya Nchi

Hivi Unajua Billionea Dangote,ni maarufu sana Nigeria,ila kuna watu wanaishi Lagos-Nigeria,hawajui kwamba Anakiwanda cha Cement Tanzania.
Sasa maisha ni akili,sio kila kitu mtu anadi.
Big UP Diamond,licha ya kwamba kanikera kuimba Nyimbo ya matusi matupuuu ya Salome(usiingie huku Diamond,matusi matupu hayo jua ni soft copy na mungu yupo na unaiacha milele).
Mkuu hao Wanigeria wasiojua umiliki wa kiwanda cha Cement cha huyo Tajiri wa Africa labda wale wasiokuwa na mitandao ya kijamii.Especially wale waishio Kwa Mtogole ya Lagos. Ila sio wale wanaofuatilia latest news every time.
 
Utaishia kuandika makala wengine wanaishi kama wapo dunia ya kwanza...
 
Nilijua tu Chanzo lazima kitakuwa DAR.

Waandishi na Aibu ya Taaluma.
Waandishi wengi wa habari wanashindwa kuielewa,wao waangalie mfano kwa Madaktari
Wote wataitwa Madokta,ila kila mmoja ana specific profession yake.
Ila waandishi wetu hawa,unakuta mwandishi kama daladala,yaani yeye anaandika chochote tu bila kujua uwezo wake.

Mwaandishi wa Taaluma ya Michezo na Burudani(Sanaa kwa ujumla)lazima awe amesomea Sanaa,na Chuo Kikuu cha Dar wanatoa Degree ya masuala hayo kama sikosei,na kama nakumbuka vizuri Marehem Mzirai alikuwa anasoma Pale.Na Chuo cha Bagamoyo kinatoa Kozi nzuri sana ya masuala ya Sanaa na Uchumi,ambapo utashangaa pale unakuta Wazungu wanasoma ila waswahili na waandishi na wasanii wanapita kama polisi,wanenda kwa warsha tu na vi seminar vya kuzugia ili wapate certificate of attendance

Sasa Mwandishi lazima awe na taaluma.Sasa kwa akili ya kawaida,hivi unashindwa kufanya analysis tangu alipotoka Diamond mpaka leo hii na mafanikio yake?
-Na sio lazima kila biashara mtu aweke wazi,yale ni maisha binafsi,kuna watu humu hata wake zao na waume zao hawajui anapokea kiasi gani kama Mshahara.Na ni mwili mmoja,sasa itakuwa Diamond?

Maisha yanaanza kwa Shilingi moja,then inategemea umeiwekeza vipi.Wapo watu walianza na pesa za madafu tu tena milioni moja tu,leo hii ni milioneaz wakubwa na tunawaheshim.

Diamond ana nidham kubwa sana ya Pesa tena Sana.
Kwa mtizamo wa haraka unaweza kushangaa kwanini Diamond Jina kubwa halafu anahitaji Management?Jibu moja tu ni kwamba anajtambua na anajifunza kwa Wenzie Nje ya Nchi

Hivi Unajua Billionea Dangote,ni maarufu sana Nigeria,ila kuna watu wanaishi Lagos-Nigeria,hawajui kwamba Anakiwanda cha Cement Tanzania.
Sasa maisha ni akili,sio kila kitu mtu anadi.
Big UP Diamond,licha ya kwamba kanikera kuimba Nyimbo ya matusi matupuuu ya Salome(usiingie huku Diamond,matusi matupu hayo jua ni soft copy na mungu yupo na unaiacha milele).
Umelonga Kitu aisee.
 
Sasa yeye mwandishi ambae kabla hajaandika anatakiwa kwanza kufanya utafiti na kutoa majibu kinyume chake ndo kwanza anakuja na maswali... sasa anataka amjibu nani?! Au ngoja mimi nimrahisishie--
  • Jamaa anauza dawa za kuleya
  • Freemason
  • Anasafirisha meno ya tembo
  • Illuminat
  • (Nafanya utafiti kufahamu vyanzo vingine)
 
Back
Top Bottom