Diamond anapata wapi kiburi cha kuidharau BASATA na kuimba wimbo uliopigwa marufuku?

Diamond anapata wapi kiburi cha kuidharau BASATA na kuimba wimbo uliopigwa marufuku?

umenikumbisha safar moja nimeenda boda ya tarakea,kuna wahuni wamening'iniza mirungu upande wa Kenya halaf wanaishi bongo yani mtu akitaka wanavuka wanamuuzia anasaga huko huko halaf anaingia bongo yuko safi askari hawana cha kufanya,halikadhalika na pombe hivyo hivyo wamekataza kuuza mchana but mida wote watu wako njwiii kumbe wanaenda kulewea kenya wanarudi ardhi ya TZ washapendeza na askar wanakodoa tu hahahahah
Hahahaha hao majamaa noma aisee,,wakirudi bongo full andasi
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kenya wakiruhusu bhangi itakuwa rahaa...unavutia kule unavuka mpaka unakuja bongo
umenikumbisha safar moja nimeenda boda ya tarakea,kuna wahuni wamening'iniza mirungu upande wa Kenya halaf wanaishi bongo yani mtu akitaka wanavuka wanamuuzia anasaga huko huko halaf anaingia bongo yuko safi askari hawana cha kufanya,halikadhalika na pombe hivyo hivyo wamekataza kuuza mchana but mida wote watu wako njwiii kumbe wanaenda kulewea kenya wanarudi ardhi ya TZ washapendeza na askar wanakodoa tu hahahahah
 
Kama inavyofahamika kwamba hivi karibuni baraza la sanaa Tanzania (BASATA) liliufungia wimbo wa "Mwanza" ulioimbwa na mwanamuziki Diamond kutokana na maneno ya matusi aliyoyangiza makusudi kwenye wimbo huo..katika kuufungia wimbo huo BASATA walieleza wazi (kama inavyoonyesha barua ambatanishi) kuwa msanii Diamond hatakiwi kuutumia huo wimbo huo tena kwa vyovyote vile na vyombo vya habari pia vilionywa visiutumie kamwe lakini katika hali ya kushangaza jana usiku akiwa jukwaani nchini Kenya aliuimba huo wimbo...Swali je wapi Diamond anapata kiburi cha kutofuata masharti ya BASATA.. Natumai kwa dharau hizi alizoonyesha BASATA watamfungia si chini ya miezi sita kufanya shoo zake tena waanze kesho...
Hahaha huo wimbo leo wabunge walikuwa wanauimba
 
Inaweza ikawa ni makosa nchini kwako ila ni ruksa nchi ya mwingine...


Mfano bangi hii hii ambayo ni marufuku nchini kwako, ila nchi zingine ruksa...


Cc: mahondaw
 
Mkuu nasikia Leo wabunge wakiongozwa na naibu spika walikuwa wakicheza hiyo nyimbo.
Sasa washitaki na hao wabunge kwa basata.
Fanya ya kwako roho mbaya haisaidii
Sana tu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kiukweli ule wimbo haufai kimaadili lakini nani anajali!
Kinachoangaliwa ni kiwa hajamtaja kiongozi wa serikali kwa kimkosoa.
Maadili hayana mpango alimradi muimbaji asiwe na rikodi ya upinzani wa kukosoa.

Watu wanalinda wanalinda maslahi na vyeo vyao sio maadili yasiyo na mpango kwao.
 
Huu wimbo wa MWANZA huku mtaani unapigwa kila siku aisee,mpaka huwa najiuliza inamaana hawa watu hawafahamu kama huu wimbo umefungiwa!?
Ukipita barabarani,bodaboda wanaupiga kama hawana akili nzuri!
Kwenye vibanda vya kuingiza/kurusha nyimbo wanaupiga kama hawana akili nzuri!
Kuna nyumba hapa mtaani kwetu wana kawaida ya kuzima umeme mchana na kuwasha jioni,basi umeme ukiwashwa tu,utasikia wimbo wa MWANZA unakiki kwa spika.
Tena kuna wakati huwa ninapishana na vitoto vidogo kabisa hapa mtaani kwetu vinaimba huu wimbo.
BASATA wajipange aisee,huu wimbo umewashinda nguvu.
 
Aisee kuna watu mambumbumbu yani unaanzisha uzi serious kuzungumzia sheria za nchi nyingine kabisa.

Labda kaidharau KASATA ila sio BASATA.
 
Aisee kuna watu mambumbumbu yani unaanzisha uzi serious kuzungumzia sheria za nchi nyingine kabisa.

Labda kaidharau KASATA ila sio BASATA.
Itakuwa BASAKE badala ya BASATA na sio KASATA Mkuu... Hahahahaa!!
 
Siku nyingine usikurupuke kujibu tu thread bila kusoma kwa undani barua ya BASATA haikuwa na mipaka alipigwa marufuku kuutumia popote...hata yeye aliomba msamaha kwa kukili kuwa wimbo una matusi wala hawezi imba mbele ya wazazi wake..hilo linatosha kumchukulia adhabu
Mkuu usiwe na kichwa kigumu kuelewa BASATA ni kwajiri ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom