Diamond atangaza ujio wa Wasafi FM na Wasafi TV

hahahaa ndiyo mkuu
 
Hongera ziende kwa Joseph Kusaga maana ndio MWENYE WASAFI TV na RADIO wala sio Nasibu
Unaweza kuhisi ni uongo lakini ukihisi vizuri kunaweza kuwa na kiukweli.

Kuna JOTI SNACKS
Kuna DIAMOND KARANGA

Licha ya biff lakini bado CLOUDS wanatangaza DIAMOND KARANGA, Kusaga yuko karibu na MABOSS wa DIAMOND KARANGA Kuliko DIAMOND.

, Je, kama DIAMOND KARANGA ni ya DIAMOND licha ya kuwa ilikuwepo kabla haijanasibishwa na DIAMOND na JOTI SNACKS ni za JOTI ???

- Isn't just a MARKETING STRATEGY.

- Kuhusu Kusaga kuwa na mkono hapo wala siyo jambo la ajabu maana jamaa anaamini biashara ya TV/RADIO kuliko kawaida na ndio maana anafungua viredio vipya kila siku
 
Tofauti iliyopo ni kuwa hao uliowataja wao wenyewe HISA zao ni PUBLIC na zinafahamika na ni wasema kweli kuliko hawa wa KWETU wapenda KIKI, SIFA na DRAMA wanaona wakisema kweli mtawaona wamebuma. Wanataka watu wajue wana HISA 100% wakati hakuna ukweli wowote
 
Mimi nipo mtaa wa mabatini kijiji cha mnkola kata ya ibihwa wilaya ya bahi mkoa wa Dodoma. Huku mambo ya TV na ving'amuzi bado hayajafika. Vipi redio wamewasha?
Bado wanatafuta kiberiti
 
Hongera ziende kwa Joseph Kusaga maana ndio MWENYE WASAFI TV na RADIO wala sio Nasibu
Wewe kweli akili ndogo, Yani kusaga aiue Clouds Media kwa mikono yake mwenyewe!!?? Kusaga ni Founder na C.E.O wa CMG kwahiyo atapambana kwa kila namna kuisimamisha Clouds na siyo kuiangusha. Tukubaliane tu na tuweke chuki pembeni; WASAFI TV NI MALI YA DIAMOND na clouds watapambana sana kuishusha, tusubiri VITA ya mafahari hawa.
 
Mkuu una point...ila pia wasafi inaweza ikawa na mtu/watu wengine nyuma yake,ila diamond ni upfront kwa sababu ya brand yake
 
Naiona wasafi Tv kupitia Azam decoder Chanell # 122. Ki ukweli mmeanza vizuri, Quality ya picha ni mzuri.
Mmechagua vyema kuweka ktk decoder ya Azam kwani kwa sasa hakina mpinzani kwa Tz.

Nawatabiri makubwa zaidi!

HONGERA DIAMOND na Uongozi wako!
Namuona luge kaangalia nilipogonga hodi mlangoni akawa anaangaika kuitoa Ila nikamuwah
 
Kusaga ni Founder na C.E.O wa CMG, kama ana hisa WASAFI hilo ni jambo la kusubiri maana ni ngumu sn kuamini kuwa Kiongozi wa kampuni A anaweza kununua hisa (kusupport) kampuni B ambao ni washindani wake kibiashara wenye lengo la kuishusha kampuni yake A. Nnachoamini Kusaga na Ruge watapambana kwa kila namna kuisimamisha Clouds na siyo kuiangusha. Tukubaliane tu na tuweke chuki pembeni; WASAFI TV NI MALI YA DIAMOND na clouds watapambana sana kuishusha, hilo suala la Hisa ni jambo la kawaida sana kwa kampuni yoyote ile Duniani inayolenga mafanikio lkn kati ya Wana hisa tumtoe Kusaga maana huyu ni mshindani. Haya sasa tusubiri VITA ya mafahari (CMG vs WASAFI)
 
Mkuu una point...ila pia wasafi inaweza ikawa na mtu/watu wengine nyuma yake,ila diamond ni upfront kwa sababu ya brand yake
Sahihi kabisa, kwa namna walivyoanza nalazimika kuamini kuwa kuna mikono ya watu (shareholders) nyuma ya uwekezaji huu. Nnapokataa mimi ni hapo kwa Kusaga. Hisia zangu zinanituma kuwa Mkuu wa Mzizima ana maslahi makubwa (amewekeza) kwenye Biashara hii. Tusubiri tutajua mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…