Tatizo lenu ni kwamba hata kama ninyi ndiye washauri wa huyo bwana basi mtazidi kila siku kumshauri vitu ambavyo sana sana vitamchelewesha kufika akutakako..
Subiri nikupe mfano mdogo tu ambao hata yeye kama atasoma hapa naamini atauzingatia.. Diamond nasikia ana zaidi ya mashabiki Million 2 kwenye mitandao. Kati ya hao almost 90% ni vijana below 30 yrs na kati ya hao 90% ambao ni vijana karibia 70% yao ni wanafunzi na vijana wasio na uwezo/kipato cha kueleweka.. Kwahiyo tunaweza sema 80% ya mashabiki wake sio watu wenye vipato vya kueleweka.. Sasa hauwezi ku ignore 80% ya mashabiki wako udili na 20% ambao pia huna hakika kama watapenda kile unachokiweka mezani kwa sababu mbalimbali, either bei au prestige ya hao mashabiki (unafahamu matajiri wetu wanavyohusudu vya nje).
Sasa tuanze kudili na hao 90% ambao ni almost 1.8 Million ambao kila siku wako kwenye mizunguko either ya kishule au kutafuta maisha. Ukiweka kinywaji ambacho utauza kwa shilling 500 tu na kila siku kati ya mashabiki wako hao 1.8M, asilimia 10 pekee ndio wakanunua (hizi ni estimation za chini kabisa pia tumeignore ambao sio mashabiki na wale ambao hawako kwenye mitandao) kwahiyo angalau kwa siku akawa anauza bottles 180,000 kwa hao watu 180,000 kwa shilling 500/- ina maana kwa siku atatengeneza kiasi cha shilling 90,000,000/-.. Hiyo Turnover ya million 90 kwa siku kwa profit margin ya 10% (mostly common to many fast moving products) itamletea faida ya 9,000,000/- kila siku.. Yaani kila mwezi anakuwa na uhakika wa faida ya Million 270.
Hizo perfume hao 20% wakinunua wanaweza kutumia hata mwaka mzima.. Yaani mtu anapulizia akiwa ana special event/occasion ya kuattend na si kupulizia kila siku akiwa kwenye mizunguko ya kawaida.. Unaweza kuta kwa mwaka faida ya hizo perfumes pamoja na bei kuwa kubwa wala isizidi Million 100 wakati akiweka cheap product ambayo kila shabiki ataafford kama mfano wangu hapo juu anatengeneza Million 270 kwa mwezi mmoja tu..