Diamond hana washauri?

Diamond hana washauri?

Kama hujawahi kutelekezwa na mzazi huenda ukaona Diamond anamakosa. Lakini kwa waliowahi wanajua uchungu wake. Kuna wakati mtoto anakosa hata hela ya percetamol lakini utasikia baba anahama bar na kuoa kila siku. Hivi baba huyu nae utapewa lawama baadae?

Kwa bahati nzuri, mzazi ambaye hakukulea, hakukujali, alikukana, alikuacha bila kujua utaishije, Hawezi kukupa LAANA abadani. Na hapa ndio maajabu ya Mungu yanapojionyesha.

Lakini pia kuna wakati wazazi wa namna hii wakabaki kua kama somo kwa akina baba wengine.

You're very right... Aisee it's hard ukijiweka kwenye position kama hii.. Imagine mwanamke amehangaika toka akiwa mjamzito peke yake leo eti mtoto ame fanikiwa ndio awe wa maana!!!
 
kweli kabisa ilibidi amsamehe. kwani bila yeye diamond asingekuwepo. me naomba diamond amsamehe mshua. ampeleke hospital. mungu atamjalia zaidi na zaidi. rihanna nae alikuaga name bifu name baba yake ishu Kama hiyo lakini akamsamehe had I Leo mzee anakula bata maisha matamu

What if the child died? Mimi huwa naona kuwa muda mtu anapohitaji baba kuliko kipindi chochote kile ni wakati wa utoto.. Sasa kama hakumfaa utotoni Sasa kuna mantiki gani ya kuwa na baba?
 
mimi namchukulia huyu mondi kam wapenda sifa wengine waliopita...siku zote mzazi akosei...mondi kalewa misifa anayoipata kwenye mitandao ila akae akumbuke kuwa huwezi kuwa bingwa milele siku moja utashuka ili apande mwingine...mafanikio ni kama gari la abiria...kila mtu atapanda...wako wapi wakina mr.nice (mzee wa kuku kapanda basikel) yuko wapi tid (mzee wa zeze) wote walipanda gari la mafanikio wakalewa umaarufu wakafanya mambo ya kijinga mwisho waka zima kama taa...joks maana ya mond hayanihusu
 
What if the child died? Mimi huwa naona kuwa muda mtu anapohitaji baba kuliko kipindi chochote kile ni wakati wa utoto.. Sasa kama hakumfaa utotoni Sasa kuna mantiki gani ya kuwa na baba?
Wababa wa hivi wanatia hasira yeye anavomuhitaji diamond sahivi Ndivo hivo diamond alimuhitaji kipindi hicho hayupo.... Mzee atulie tu ndo kishalamba garasa
 
Je alizaliwa ndani ya ndoa au nje ya ndoa....!?? Alimuhudumia kipindi cha malezi....???
 
Kila mwanaume anatakiwa ajifunze ujifunze kupitia baba Diamond kuwa kutelekeza watoto hailipi hata siku moja. Wapendeni watoto wenu hata ama umeachana na mama yake but hakikisha kuwa unaelea watoto wako. Iko neno la Mungu linasema kuwa Jiwe walilolikataa Waashi litakuwa jiwe kuu la pembeni siku moja. Kwa misingi hii unamkataa mtoto halafu mama anateseka naye anakuwa na say kusoma au kufanikiwa katika maisha halafu unajitokeza. Kafie mbali kabisa.
 
Vipi Quran inasemaje kuhusu kumtelekeza mtoto?
 
Katika hili la mzazi wake wa kiume mimi binafsi limenigusa hasa kwa imani yangu ya dini. Siwezi kuhukumu moja kwa moja kwa maana sijui chanzo cha ugomvi wao wala status yao kwa sasa na pia MIMI SI HAKIMU, lakini nina haki ya kutoa maoni yangu hasa kumsaidia pia diamond ajitambue.

Katika hali ya kawaidia inatakiwa ingekuwa rahisi kama mzazi wako anapata msaada wako by then kila siku awe analalamika au tunamuona kwenye mitandao huo tayar ni udhaifu wako wewe mtoto kwa kuruhusu mzazi wako awe anakutia aibu wewe au familia yenu kwa ujumla. Kwa namna yoyote ni lazima suala la wazazi wako ukalipa umuhimu mkubwa sana katika maisha yako.

Katika mafundisho ya dini yanatufunza nini kuhusu wazazi?

Hakika ametakasika yule ambaye amewajibisha na kuamrisha wema na kutimiza haqqi na kuiegemeza kwa kila anaestahiki na akawajibisha haki kwa wazazi wawili, na ikawa ni amri iliyoenea kwa walimwengu wote. Hakika ameamrisha ALLAH tabaaraka wata’la katika aya nyingi kuwafanyia wema na ihsani wazazi wawili.
Mfano wa kauli yake aliposema:

{وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلاَهُمَا فَلاَ تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلاً كَرِيماً* وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيراً}
Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.


Akaamrisha ALLAH tabaaraka wata’la ihsani kwa wazazi wawili katika namna zote za wema, nao ni katika kauli [unapozungumza nao] pale aliposema [basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima]. Vivyo hivyo kuwafanyia wema katika matendo; kimwili na kimali kwa kauli yake aliposema: (Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma).
Na akanyanyua ubora wanapofika katika hali ya uzee, kisha akakataza kuwavunjia adabu na kuwatusi, achilia mbali kuwaacha wakiteseka.

UWAJIBU WA KUWAFANYIA WEMA WAZAZI WAWILI:

Hakika ameamrisha Allah tabaaraka wata’la, na akawajibisha kwa njia ya wasia kuwafanyia wema wazazi wawili katika aya nyingi za qur’an. Pale ilipokuja amri ya wazi juu ya kuwatii, aliposema:
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَاناً
Na tumemuusia mwanadamu awatendee wema wazazi wake wawili[1]


Ikaonesha wazi kuwa kuwafanyia wema wazazi wawili ni jambo la wajibu kwa kuwa ni wasia wa Allah kwetu. Bali akaliambatanisha jambo hilo la kuwafanyia wema wazazi wawili na twaa’ yake Allah tabaaraka wata’la pale aliposema:

وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً
Na mola wako mlezi ameamrisha kuwa msimuabudie yeyote isipokuwa yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema.[2]


Na kauli yake aliposema:
وَاعْبُدُواْ اللّهَ وَلاَ تُشْرِكُواْ بِهِ شَيْئاً وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً
Na mwabudieni Allah wala msimshirikishe na chochote, na muwafanyie wema wazazi wawili.[3]


Zikakusanya aya mbili hizi kuwa kufanyiwa wema wazazi wawili ni haqqi yao, bali akaifafanya haki hiyo kuwa ni ya pili baada ya tawheed yake Allah tabaaraka wata’la akionesha ukubwa wa jambo hilo [la kuwafanyia wema].

Amesema Al qurtwubiy [Allah amrehemu], kauli ya Allah “Na wazazi wawili kuwafanyia wema [ihsani]” maana yake ni:
برهما وحفظهما وصيانتهما وامتثال أوامرهما

Kuwafanyia wema na kuwahifadhi, kuwatunza na kutekeleza amri zao.


Katika kulisisitiza hilo, mpaka ikawa [wema kwa wazazi wawili] ni wenye kutangulizwa mbele hata kabla ya Sunnah za kujitolea kama vile Sunnah za kabla ya swala nk. Na kwa hili akaweka imamu muslim [Allah amrehemu] mlango katika swahih yake akiuita:
باب تقديم بر الوالدين على التطوع بالصلاة وغيرها

By the way mimi nimekubusha tu. Kama ni kweli mzazi hapati msaada basi ajitahidi kumsamehe, kama anapata msaada ila ndio umaarufu basi Diamond anisemehe maana binadamu tumeumbwa kukOsea. Na huu ni mwezi wa toba hakika atakuwa amenisamehe.

Asante.
Mm huwa najiuliza hivi bahati mbaya huyu baba yake anafariki (Mungu aepushie mbali) HIVI HUYU KIJANA DIAMOND ATAKWENDA MSIBANI???? Hivi huwa hajiulizi? ?? Atakua lini???
NA ASIPOKWENDA ATAJENGA LEGACY GANI KWA KAZI ZAKE???? Yani ndo maana watu husema pesa ni kama mvua inayo nyesha popote hata kwny kinyesi....huyu KIJANA kutembea kwake na pesa alizonazo hazijamsaidia lolote kukua kiakili...na kama mama yake ndo anamsonga hivyo achunguze sana huo msimamo...napita tu
 
Ivi huyo Mzee ana Mtoto Mmoja tu? Kwanini anae pewa lawama ni 'Dimond' tu?
Kabla ya kupost jiulize kwanza kisha upost, usikurupuke hao ndugu zake umewahi kuwasikia?na je hali zao kimaisha zikoje? Usiteteee ujinga hivi anwezaje kutoa m3 kwenye birthday ya rafiki akashindwa kutoa laki mbili Kwa ajili ya matibabu ya baba take ambaye alikatika mpaka akatokea yeye?
" Baba na mama ni Mungu wako wa hapana duniani"
 
Nawe ungeamua kufikiri basi ungeiona mantiki ya muuliza swali! Je, mtoto ni Diamond peke yake? Jibu HAPANA... mwingine anayefahamika ni Queen Darleen! Je; Queen Darleen anamsaidia baba ake? Kama ndiyo ni kwanini hatumuoni Mzee Abdul akitumia magazeti ya udaku kama kawaida yake akionesha kumshukuru mwanae?! Au nae hamsaidii?! Kama nae hamsaidii ni kwanini hatuoni magazeti ya Shigongo yakiandika habari za Queen Darleen kutomsaidia baba ake?!

One more thing! Hivi ni kwanini issue zote zihusishe magazeti ya udaku? Unataka kusema celebrities wote wa Kibongo wanawajali wazazi wao? Mbona hatuwaoni hao wazee wakilalamika kwenye magazeti ya udaku?

February mwaka huu, magazeti hayo hayo ya Shigongo yaliandika habari za Mzee Abdul kwenda studio ya Diamond!
View attachment 359277
View attachment 359278
View attachment 359279

Haya sasa nisaidie wewe! Global Publishers walijuaje kwamba Mzee Abdul alitaka kwenda Studio kwa Diamond hadi wakafanikiwa kupiga picha zote hizo not mentioning vile walivyofahamu kwamba anaenda hospital hadi wakafanikiwa kuwahi na kupiga picha akiwa bado mapokezi!!!

Ukiamua kufikiri hutachelewa kuona kwamba huyu Mzee anatumika na Shigongo kuuza magazeti yake ndio maana Diamond ana-keep distance na huyu mzee! Ingawaje mimi co Mungu but trust me; Diamond akishajiweka close na huyu mzee atakuja kujuta!
Nipe tano
 
mtoa mada mbona ameandika wajibu wa mtoto kwa baba pekee yake, alitakiwa aandike pia wajibu wa mzazi kwa mtoto ili kubalance story, na kukote vifungu vya aya

Umenena sawa kabisa, vifungu vyote alivyoandika ni vya wajibu wa mtoto kwa wazazi lakini hakuna kifungu cha wajibu wa wazazi kwa mtoto.

Kwa asilimia kubwa ikiwa wazazi watakushughulikia ipasavyo na wewe mtoto unapata upendo wa kuwashughulia vyema uzeeni kwao.

Mibaba mingine ikishazalisha haijui hata kumsalimia mtoto na unakuta ni mama ndiyo anahangaika peke yake, lakini mtoto akishapata kazi nzuri ndiyo bingwa wa kulaumu hashughulikiwi.
 
Wababa wa hivi wanatia hasira yeye anavomuhitaji diamond sahivi Ndivo hivo diamond alimuhitaji kipindi hicho hayupo.... Mzee atulie tu ndo kishalamba garasa
Atulie dawa imuingiee....kumbe aliuza nyumba kariakoo hela akakatia viuno leo anataka msaada kupitia waandishi makanjanja......aende kwa aliokula nao maisha wamsitiri
 
Back
Top Bottom