Diamond hawa ndio wabongo, chukua ushauri wangu

nikujibu, ni mwanamziki yupi wa kike ameshamfikia au kumpita jide??? kwa hizi tabia zenu za kiswazi ngoja atokee kama atapona??
 

Poor mind set inamalza watz weng sana , mimi hv vitu huwa vinanisikitisha sana kuona jinc watz weng walivojaa negative attitude, ss cjui ni hzo dv5 au ndo vp?????? Am speechless
 
Diamond kufika mbali kesha fika tatizo hao wapuuzi sijui babu tale angewapiga chini kwa level zake kuongozwa na watu kama hao guaranteed atapotea..ila.mimi najiuliza tu hivi ile nyumba yake haijaisha tu...daah...huyu Ali Kiba sasa hivi zimebaki stori tu jamaa hana jipya video hatoi show alizofanyanga miaka hiyoo ndo hizo hizo sasa hivi hana jipya...
 
Huyo Kiba hana jipya wimbo toka autoe hata video hamna. Hawezi kumfikia Daimond hata akeshe na akumbuke aliyepewa kapewa. Kwanza vipi kuhusu yule mamake wa BSS bado anamlea au.
 
Huyo Kiba hana jipya wimbo toka autoe hata video hamna. Hawezi kumfikia Daimond hata akeshe na akumbuke aliyepewa kapewa. Kwanza vipi kuhusu yule mamake wa BSS bado anamlea au.

Ukisikia kuweweseka ndio huku, Na tunamsubili Mbeya tumfunze adabu.
 
Hivi davido alipeform? Maana ulisema hataperfom na akitumbuiza damu ingemwagika
 

Very true. Diamond anapashwa aajiri afisa habari wake ambaye ata deal na media. Yeye ajikite kwenye kazi ya muziki tu. Washabiki wake walimpenda sana kwa sababu wengi wao ni watu masikini sana. Hivo kwao ilikuwa ni ushindi kuona mwenzao katoboa kifani na kimaisha pia. Sasa kosa lake kubwa ni kuwadharau watu ambao ki ukweli ndo mashabiki waliompandisha huko juu.
Kuna Fiesta ya 2014 nadhani Mwanza wakati anampandisha Linnah jukwaani. Alisema ni msaani anayependa kuupeleka muziki wetu nje ya mipaka ya nchi. Na ndo maana akawa tayari kummsaidia katika wimbo wake wa Kizai zai. Maneno hayo ameyarudia kwenye interview yake na XXL kuhusu kufanya collable na Ali Kiba. Kwamba yupo tayari kumsaidia. Nadhani dogo amelewa mafanikio mapema kabla hajafika peak.
Ajifunze kwa watu kama makocha wa timu kubwa zenye mafanikio makubwa. Wakiwa kwenye interview kamwe hawawezi kuidharau timu pinzani hata kama ukweli kuwa wao wapo juu. Kocha atasema tu, namheshimu huyu kocha mwenzangu najua ana timu nzuri sana na watatupa upinzani mkali nk. Hata kama moyoni anaamini wataenda kuifunga hiyo timu. Thats the spirit.
MWISHO: Waswahili wana misemo yao ambayo tumeirithi toka kwa babu zetu mfano aliye juu mgoje chini, mpanda ngazi hushuka.Maana yake ni kuwa waswahili hatupendi kuona mtu aliyee juu anadharau maskini ambaye hana kitu. Hivyo ikibidi watakushusha kwa njia yeyote iwayo ili watumie misemo yai hii. Watch out Diamond...
 
Tunduma kwenyewe mashabiki walikereka wakamwachia ukumbi peke yake baada ya kuingia ku perform sa kumi usiku
 

huyo kiba ushamsikia anajitangazza? bosi wako kutwaaa kuchaa na hawara yake kwenye magazeti!!
kidogi kashawafata global wamuandike
ishu sio kuzaa na wanawake wawili au watatu ishu anapaswa awe na privacy
sio kila kitu global mda wote yuko location
mfano monalisa kaolewa kanisani akazaa mtoto wakatengana akaolewa tena msiktini na slim akazaa na akaachika but we still respect her!
do you know why?!!!!!
mwingine jide aliolewa na mme wa mtu but people respect her...!!!unajua kwa nini?!!
anajiumiza mwenyewe huyo naseeeb kwani ye ndo wa kwanza kuhit tz kiivyo kutwa na mateam mavimavi tuuuuuu!!!
 
Huyo Kiba hana jipya wimbo toka autoe hata video hamna. Hawezi kumfikia Daimond hata akeshe na akumbuke aliyepewa kapewa. Kwanza vipi kuhusu yule mamake wa BSS bado anamlea au.

Hoja umeishiwa??kwann usiulize Diamond na Chief kiumbe wanaendeleaje??
 
Huyo Kiba hana jipya wimbo toka autoe hata video hamna. Hawezi kumfikia Daimond hata akeshe na akumbuke aliyepewa kapewa. Kwanza vipi kuhusu yule mamake wa BSS bado anamlea au.

Humjui mpaka utake video??
 

daimond anajiandika mwenyewe??? au huwa anaenda kwa shigongo kumuomba amwandike???
si ni mapaparazi wake kutwa kucha kumfuatilia kila aendapo na kila alifanyalo??? kwa kuamini kumuandika daimond kila siku ndio atauza???

yanayomchafua daimond ni magazeti, au mlishamuona ameitisha press comference na kuomba magazeti wamchapishe kila siku??
hapo nyuma kidogo kuna gazeti lilimtoa kiba amepozi na mdada wakaandika kiba aamua kumuanika mpenzi wake mpya,ilikuawaje hata akampublish huyo mpenzi wake?? kama sio mtu wa show off?? sema haikuvuma sana kwa sababu kiba mwenyewe wakati huo alikuwa havumi.
ndio maana nasemaaaaa, kwa mtu yeyote kuwa na scandal au kutokuwa nazo ni uamuzi wa shigongo, na hizi blogs shigongo akiamua kugeuzia camera zake kwa kiba akapokezana na hizi blogs, huyu akacopy huku akapaste kule kiba ataomba pooo.
kama hauamini, give your self time, si ndio mpo kwenye kampeni ya kumpaisha kiba, ngoja afike pale shigongo anapopataka, ndio utakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kumjudge daimond.
nikukumbushe kidogo, kuna mtu Tanzania hii alishawahi kuandikwa kama SINTAH??? enzi za juma nature?? mpaka akapewa tunzo ya kuandikwa sana kwenye KLM awards? mpaka aliatemty suicide nakumbuka, what happen baada ya kuachana na juma nature??? shigongo katurn off his camera on her.
so please try to think again unavyomjudge mtu kwa habari ulioisoma kwenye gazeti.
 
Mti wenye matunda ndio upigwao mawe, ukiona watu wana chuki sana ,wivu sana,wanakuongelea sana,ujue kuna kitu umewazidi mbali mnoooooo

Kaka comedy stars ni tofauti sana na music stars
Music inagusa maisha ya watu wengi na ina watu wengi wanaoifanya ....
Hata MASANJA angekua musician yangekua kama ya diamond tu
 

maelezo meengi
instagram nakooo?!!!
wanahack account?
tetea tu show off hizi nyie mngeenda kumshangilia pale juzi msilalamike sana!!!!
km kweli mnampenda mngeenda maana wanaompenda kiba walienda so dont blame anyonr here
yaleyale mt hapigi kura halafu analalamika mbunge wenyewe hafai!
 
Bahadhi ya wabongo,sijui hizi roho za kishetani wanatoa wap?full ujuma,usuuda,uongo na umbeya ukifanikiwa tuuuh.

*Bahadhi - Baadhi
*Ujuma - Hujuma
*Usuuda - Husda

Ova
 
nikujibu, ni mwanamziki yupi wa kike ameshamfikia au kumpita jide??? kwa hizi tabia zenu za kiswazi ngoja atokee kama atapona??

Kipindi ray c anakuja kwa kasi walianza kumponda sana komando...mara mbaya mara hajui kukata mara vile...matokeo yake wamebaki na aibu komando bado yupo palepale
 

tuombe uzima mamii, ndio kwanza kumekucha tutayaona mengi tuu.
 
Matumbo chukua.like zangu 1000. Watu ni wivu tu unawasumbua..,
 
Watanzania siku zote wana wivu wa ajabu mtu ukipata mafanikio kwa muda mfupi majungu yataanza,walianza kumuita Freemason wameona imeshindikana sasa hivi wanatafuta kila njia.

Kitu ambacho nawambia mafanikio hayaji kwa urahis Diamond kapiga sana kuwa hapo alipo.

Wabongo mshaanza na kumsema Masanja mara kumuita Tapeli na Freemason mshindwe nendeni mbarali muone kijana anavyolima mpunga.

Wivu si kitu kizuri,wivu mzuri ni wa kutaka uwe kama yeye si kupiga majungu ashuke
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…