Diamond: Nipo tayari kubadili jina

Diamond: Nipo tayari kubadili jina

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Dar es Salaam. Msanii wa muziki wa bongofleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz amesema endapo sheria itamtaka kubadilisha ubini wake anaotumia sasa atafanya hivyo

Ameyasema hayo ikiwa ni siku chache baada ya Sanura Kassim maarufu mama Dangote ambaye ni mama mzazi wa msanii huyo, kusema baba halisi wa mwanaye ni Salum Iddi Nyange na si Abdul Juma ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifahamika kama baba yake.

Baada ya mama yake mzazi kusema hayo Abdul Juma ambaye alikuwa akijulikana kama baba mzazi wa mkali huyo wa bongo flava alimtaka kuacha kutumia jina lake kama ubini.

Akizungumza leo katika mahojiano kupitia kipindi cha The Switch kinachorushwa na Wasafi Fm, Diamond Platnumz amesema suala la kubadilisha jina limekaa kisheria zaidi.

“Nafikiri ni la kiserikali zaidi na wanasheria wanaweza kulizungumzia suala hili mimi sina tatizo, wakisisitiza hili kisheria sina tatizo kabisa,” amesema Diamond

“Lakini siku zote nitaendelea kumuheshimu kama mzee wangu, kumpenda kama mzee wangu na kumsaidia atakapohitaji msaada kwani hata baada ya kupata taharuki sikuachaga hizi huduma kila niposikia kuna hili na hili natakiwa kufanya,”

Amesema hata alipojua kuwa mzee Abdul siyo baba yake miaka mingi nyuma hakubadilisha wala kumfanya amchukie kwa sababu ni suala la kawaida.

“Kitu ambacho kipo ni mimi na yeye hatukupata ukaribu sana,”

Alipoulizwa kwanini hajabadilisha hadi sasa alijibu kuwa hakutaka kuleta taharuki ya kubadili jina kwa haraka kwa sababu tangu amezaliwa amekuwa akitumia jina hilo.

“Hili ni jina (Naseeb Abdul) ambalo tangu nimezaliwa nimekua nalo sikutaka kuleta tena mambo ya haraka ni kama ushamba,” amesem.

Chanzo: Mwana halisi
 
Hahahaaa inanikumbusha Sanford and Son season 3 episode 14.

Mama's Baby, Papa's Maybe​

1612029336197.png

1612029378764.png
 
Akijiroga kubadilisha jina tu...basi na huo ndio utakuwa mwisho wa umaarufu wake kimziki. Jina linabeba uhalisia wa maisha yetu katika ulimwengu wa roho
Nafikiri ilikuwa afike hapo hili aingie kwenye destination yake.Mwisho wa binadamu yoyote yule huwa na Sababu iwe kifo au uchumi.
 
Akijiroga kubadilisha jina tu...basi na huo ndio utakuwa mwisho wa umaarufu wake kimziki. Jina linabeba uhalisia wa maisha yetu katika ulimwengu wa roho
Jina la muziki ni diamond sio nasibu Abdul
 
Unakuta hukua unalala usiku,kisa mtoto mara anaumwa,unamsaidia mama mtu kumpeleka hospitali.
Mara unahangaika huku na kule kutafuta mahitaji ya mama na mwanae,hadi inafikia kipindi unahatarisha maisha yako kwaajili YAO ili upate ridhiki upeleke WAKALE.
Mwisho wa siku unaambiwa SI MWANAO.
Inauma kufichwa muda wote huo,baadae ndiyo unakuja kuambiwa,inauma sana.
 
Dar es Salaam. Msanii wa muziki wa bongofleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz amesema endapo sheria itamtaka kubadilisha ubini wake anaotumia sasa atafanya hivyo

Ameyasema hayo ikiwa ni siku chache baada ya Sanura Kassim maarufu mama Dangote ambaye ni mama mzazi wa msanii huyo, kusema baba halisi wa mwanaye ni Salum Iddi Nyange na si Abdul Juma ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifahamika kama baba yake.

Baada ya mama yake mzazi kusema hayo Abdul Juma ambaye alikuwa akijulikana kama baba mzazi wa mkali huyo wa bongo flava alimtaka kuacha kutumia jina lake kama ubini.

Akizungumza leo katika mahojiano kupitia kipindi cha The Switch kinachorushwa na Wasafi Fm, Diamond Platnumz amesema suala la kubadilisha jina limekaa kisheria zaidi.

“Nafikiri ni la kiserikali zaidi na wanasheria wanaweza kulizungumzia suala hili mimi sina tatizo, wakisisitiza hili kisheria sina tatizo kabisa,” amesema Diamond

“Lakini siku zote nitaendelea kumuheshimu kama mzee wangu, kumpenda kama mzee wangu na kumsaidia atakapohitaji msaada kwani hata baada ya kupata taharuki sikuachaga hizi huduma kila niposikia kuna hili na hili natakiwa kufanya,”

Amesema hata alipojua kuwa mzee Abdul siyo baba yake miaka mingi nyuma hakubadilisha wala kumfanya amchukie kwa sababu ni suala la kawaida.

“Kitu ambacho kipo ni mimi na yeye hatukupata ukaribu sana,”

Alipoulizwa kwanini hajabadilisha hadi sasa alijibu kuwa hakutaka kuleta taharuki ya kubadili jina kwa haraka kwa sababu tangu amezaliwa amekuwa akitumia jina hilo.

“Hili ni jina (Naseeb Abdul) ambalo tangu nimezaliwa nimekua nalo sikutaka kuleta tena mambo ya haraka ni kama ushamba,” amesem.

Chanzo: Mwana halisi
Upumbavu tu. Mama yako kashindwa kukupa jina la Baba yako for 30 yrs, hujiulizi kwanini? leo out of blue, ubadilishe jina na kujiita jina la mtu ambae wakati wa uhai wake hukuitwa jina lake, leo hayupo duniani ndio uitwe jina lake. hapa tatizo ni Mama na sio Diamond.
 
Inabidi awe makini, maana jina huwa linamaana kubwa katika maisha ya binadamu na mafanikio yake.
 
Back
Top Bottom