Diamond Platinumz Fans' Special Thread: Njooni tukutane hapa


Duuuh!kwa style hii harufu ya nyama nyumbani kwa mcharo lzm iendelee kupeleka shida kwa majirani....hard work pays
 
Nna kila sababu ya kuamini rais wa nchi atamuita rais wa wasafi ili amsaidie kupunguza kelele za esikuro akaunti....
Maaaaana rais katupiamo 3D
 
Mtanisamehe tuuuu kwa gazeti ntakalopost lakini lina maana kubwa sana
 
Wow, worth sharing: HONGERA DIAMOND PLATNUMZ!

Ngoja niseme kidogo kitu nilichojifunza kwa huyu kijana.
Kuna wakati fulani Hezron Michael (Paul Mashauri) aliwahi kuandika kuhusu msanii wa muziki wa bongofleva Diamond akisifia bidii yake lakini sasa naelewa zaidi.

Diamond huyu alikuwa hana hela ya kwenda studio mara ya kwanza (mtaji wa biashara) lakini hii hai kuwa kizuizi kwake. Kwa kuwa alitaka kutoka moyoni aisee hela ilipatikana! Ilikuwaje? Mama yake alimpa mkufu akauze ili apate hela ya studio. Na alienda studio. The rest is history.
Sasa ili unielewe hapa naomba unisikilize kidogo.
Unamjua Joseph Kusaga? Labda humjui. Huyu ni mmiliki wa Clouds FM na Clouds TV. Niliwahi kumsikiliza LIVE akisema kuwa wakati alipopata wazo la kufungua kituo cha redio mtaji "uligomba". Kwa kuwa alitaka saana kufungua redio alimfata mzazi wake akaomba HATI YA NYUMBA ili akakope pesa benki! Can you imagine? Mzazi alimpa akijua hiyo dream ikifa nyumba hawana. Hela ilikopwa nyumba ikawekwa rehani and the rest is history!
Unamjua Jeff Bezoz? Kama humjui nisaidie tu kugoogle. Lol. Anyway. Huyu ni moja ya matajiri 20 wakubwa duniani. Hivi sasa akiwa No. 18 kwenye Forbes list utajiri wake ukiwa $32 billion! Lakini huyu bwana wakati anataka kuanzisha mtandao wake wa Amazon.com hakuwa na mtaji. Sasa huyu alichofanya aliwafata wazazi wake ambao walikuwa ndo wamestaafu. Akawaomba pensheni yao ili afungulie biashara. Can you imagine wazazi waliwaza nini? Wanamuuliza biashara gani anawambia ni mambo mapya ya internet nataka niuze vitabu kwa kutumia internet. Hawakuelewa lakini kwa vile alitaka wamkopeshe hiyo pensheni by hooks and crooks aisee walimpa! And the rest is history.
Hebu jiulize leo wazazi wake wanaishije?
Jiulize mzazi wa Jay Kusaga leo kama anashida ya nyumba (kama yupo hai.. Na kama yu hai aishi miaka mingi zaidi). Jiulize mama wa Diamond Platnumz leo anaishije. Kwanza tunavyoongea hayupo bongo yuko zake Sauzi na mwanaye! Yes. Jiulize kama ana shida ya hela ya kunulia mkufu tena.

Sasa wengi mna woga! Ndoto unayo lakini ukiulizwa kidogo tu: We Salome unaomba hela ya biashara ukishindwa hela yangu itakuwaje..? Au ukiambiwa elimu ulishindwa biashara utaweza? Unajiinamia kesho unaenda kwenye mkesha kuomba Mungu afungue njia nyingine! Pshuuu! Hivi humo kichwani kuna maji au? Afu ukisikia watu wanafanikiwa ooh Freemason ooh one day nitamiliki na kutawaka. Tawala kwanza fikra zako! Fursa zinazidi kuja na kukupita uko tu reception unapata laki tatu kwa mwezi na degree yako ya Mass Communication! Pshuuu.

Diamond alipouza mkufu hela nyingine alipeleka studio kurekodi nyingine akaenda British Council kusoma English! Mambo ya "Good morning" mambo ya "let me read the contact once again.." nini. Huyu ni mtu anayeona mbali. Wasanii Wangapi walikuwa maarufu kabla yake but hawakuwaza kama yeye. Niwataje? Halafu haohao wanamsengenya na kumponda.
Hivi wasomi wangapi wanajua lugha zaidi ya Kiswahili. Honestly. Hivi nitajie wasomi wangapi wameitangaza nchi hii kimataifa kama Diamond Platnumz. Kila siku wasomi tunapost picha za graduation. "Thank God I have made it. Xoxo". You have made what? Joho au? Joho hata wanafunzi wa Nursery School wanavaa mbona. Ilipotokea uvumi kuwa anapewa degree ya heshima kila mtu alisema ooh sijui nini.. Umeitangaza nchi wewe?!!

Diamond anasomesha watoto watatu IST. Unajua ada ya IST lakini? Au unadhani naongelea gari IST. Naongelea International School of Tanganyika ambao watoto wa mabalozi wa nchi za nje ndo wanasomeshwa na nchi zao! Huyo ni Diamond Platnumz! Wewe umesomesha wangapi hata shule ya Kata na una Masters ya UDSM sijui ya Mzumbe sijui ya Edinburgh, nk.
Mentality is everything. Sasa Mungu akubariki wewe au yeye?

Kila siku uko kwenye maombi ya kufunguliwa na kuinuliwa unarudi nyumbani saa tano usiku Diamond anatoka studio saa saba za usiku. Who is hard working? Siku ya mwisho walokole tutaabishwa na watu tunaowaona "namna gani vipi". Mungu atupe ujasiri wa kufanya makuu!

Mentality ya utajiri haiangalii elimu. Shigongo na wewe nani kasoma zaidi. Nani tajiri? Nani anaweza kuitwa na rais awambie vijana kwenye TV kuhusu biashara Shigongo au wewe mwenye Degree ya biashara kutoka CBE?
Jiulize maswali magumu. Usijipe FALSE HOPES. Ati hata nikikosa hela mbinguni naenda. Sikia wewe, kuna watu hawakwendaga mbinguni kwa sababu tu hawakumvisha mtu aliyekuwa na uhitaji wa Nguo. "Nalikuwa uchi...." Hilo tu. Nilikuwa namchekesha cousin wangu Haruni Leonard kuwa unaweza kwenda mbinguni ukamkuta BOB MARLEY na huku wewe ulikuwa unaimba gospel.

Kama unataka kufanikiwa hebu acha excuses. Sina mtaji. Sina muda. Kwani kuna mwenye kiwanda cha kuzalisha muda? Muda wa Escrow uliupata. Muda wa kukaa kubadilishana mawazo na watu upate mtazamo mpya huna eti. We kaa hapo? December ndo hiyo imefika!

Diamond akirudi hukawii kusikia kaenda ikulu. We roho inakuuma hata kazini kwako tu hutambuliki. Hukawii kusikia kaenda Marekani kufanya shoo. We mwisho wako Tabata Bima Buguruni Posta hata huko hawakujui.

Success has nothing to do with your religion but your MENTALITY.
 
Wajameni musikwazike na gazeti hilo wala lisiwachoshe,nilitaka tu mtambue kuwa kijana wetu ni kioo kwa sasa kwa vijana wote wenye ndoto na UTHUBUTU na KUJITUMA.
 
Wajameni musikwazike na gazeti hilo wala lisiwachoshe,nilitaka tu mtambue kuwa kijana wetu ni kioo kwa sasa kwa vijana wote wenye ndoto na UTHUBUTU na KUJITUMA.

kuna kitu nimekipata japo sio kikubwa sana na wala sio kidogo ila nitakifanyia kazi
 
Hilo bandiko LA Innocizy la maana sana....ila ntarudi kuchangia keshooo....now ubongo umevurugikaaa.....
 
Last edited by a moderator:
Mie pia napenda kazi zake na anavyojituma, kama alivyosema mdau hapo juu ni kweli anatakiwa kuwa na msemaji na sio kila kitu anachoulizwa na media ni lazima atoe majibu, mengine ayapotezee, haswa kuhusu private life yake

#mama yake p. Mwenyewe anapenda private zake ziwe kwenye media wewe uko chumbani na mpenzi wako unasambasa picha kam si ulimbukeni nini anatumia nguvu nyingi sana kuonyesha private zake kwa watu
 
nmependa maneno yako

Domo kwangu ni zaidi ya msanii....kwangu ni alama ya hustling....2009 to 2014 ni miaka 5 mtu anakua amefika mbali si jambo Dogo....wachawi wana haki ya kumchukia aseeee
 
#mama yake p. Mwenyewe anapenda private zake ziwe kwenye media wewe uko chumbani na mpenzi wako unasambasa picha kam si ulimbukeni nini anatumia nguvu nyingi sana kuonyesha private zake kwa watu

Hata akiweka picha ya bendera ya taifa bado atafuatwa tuu....huo ndo mzigo wa kuwa staaa then unauzika gazetini
 
Sote tumeangalia majuzi wakati Diamond akiwa ni mmoja wa wa wanamuziki wachache Afrika walijinyakulia tuzo nyingi kule SA kwenye TV ya Channel O. Ni mwanamuziki wa kwanza kutoka Tanzania, sijui katika nchi za jirani, kujizolea tuzo tatu nje ya nyumbani kwao kwa mpigo katika event moja. Anatakiwa kupongezwa sana na watanzania wote hata wanaomchukia kwa sababu binafsi: ni lazima tujifunze kutenganisha maji na mafuta.

Tuzo hizo alizopata zimemuinua na kumpa power fulani katika jamii hii. Ni muhimu kuangalia tena kuwa Diamond ana sifa nyingi sana nzuri na vile vile sifa nyingi sana mbaya kwa jamii, mbaya zikiwa zinatokana zaidi na utoto. Kwa vile power huja na responsibility, ninawaomba washauri wa karibu na Diamond wamfundishe aweze kuchangia kama role model katika jamii hii ambayo imaevurugwa sana na wanasiasa wetu wenye ubinafsi. Role model siyo kutoa michango na misaada tu kama ambavyo wasanii wengi hufanya; ni pamoja na kufanya kazi zao ziwe za kufundisha jamii hata kama hazilipi sana- ni swala la kuchanganya tu. Vile vile ni kuhakikisha kuwa matendo yao binafsi yale wanayofanya hayatakuwa na madhara kwa wale watakaowaiga. Mwisho zaidi ni kujifu\za kuwa-accomodate watu wa namna nyingi hata wale wanaopingana nao; after all ukishafika juu huna haja ya kushindana na aliye chini yako.

Just my few words to our Diamond's success
 
Hivi huyu bwana mdogo ana vitega uchumi vyovyote...

Nakumbuka kuna wakati alikuwa anajigamba kuwa na pesa nyingi kiasi cha kufikia bilioni moja...

Sasa kwa nchi yetu hii muziki si ajira rasmi na mara nyingi huwa mashabiki wake wana kasumba ya kumpenda msanii mmoja kwa muda fulani baada ya hapo wanahamia kwa mwingine mpya...

Hivyo ni vyema kutazama vyanzo vingine vya mapato sasa kwa kufungua vitega uchumi, na kwa kuwa ana jina kubwa ni rahisi kufanikiwa upande huo pia...
 
Wajameni musikwazike na gazeti hilo wala lisiwachoshe,nilitaka tu mtambue kuwa kijana wetu ni kioo kwa sasa kwa vijana wote wenye ndoto na UTHUBUTU na KUJITUMA.

Na ndio anachofanya 3D anathubutu kwa lugha nyngine ni risk taker.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…