Diamond Platinumz mtafutie shughuli nyingine Queen Darleen, amekuwa kituko na mchekeshaji, muziki hauwezi kabisa

Mkuu hili ni jukwaa maalum kwaajili ya kuwaongelea hao..................
 
Wakati ana tuzo kabisa aliiipata 2008 au 2009 kwa nyimbo yake inaitwa maneno kama sikosei
 
Ndio dish limeyumba Na Yale maji yenu nimeyanywa sana na mengine nimeyaoga Na yaliyobakia nimemwagilia ule mmea wenu. Una la nyongeza?
teh teh
 
Mbona huyo dada alishakua maarufu tu kabla diamond kujulikana single yake ya kwanza alimshirikisha ali kiba inaitwa wajua wanipenda ma ilipata umaarufu tu
Ila mtoa mada huijui game b.flavor
 
Mbona huyo dada alishakua maarufu tu kabla diamond kujulikana single yake ya kwanza alimshirikisha ali kiba inaitwa wajua wanipenda ma ilipata umaarufu tu
Ila mtoa mada huijui game b.flavor

Achana nae mzushi huyo.. kabla hata hiyo unanianda ambayo ndio imemtoa kiba huyo ndio mdada wa mwanzo mwanzo kbs kuimba chorus za wasanii w bongo fleva!!.. achana na zile salome za dully, hata ule uliowahi kuwa wimbo wa taifa GETI KALI huyo dada anasikika na ile sauti yake ya "inspekta sema basi unataka nini" ni dada aliyetoka mbali sana na bongo fleva..hata hao kina diamond wamethubutu kujaribu kuimba kwasababu ya kupata hamasa toka kwa huyo dada!! diamond ana kila sababu ya kumshikilia dada yake anajua alimtoa wapi na alimshawishi vipi hadi nae akathubutu kuimba.!! Mtu anaposema ampige chini dadaake kisa pale WCB kuna wamakonde flani wanajiita sijui hamo nini sijui malombo nini.. ni upuuzi uliopitiliza
 
Babu Tale pale ni kibarua tu, kazi yake ni kubeba mabegi ya Diamond. Kwahiyo hawezi kuongea chochote kuhusu msanii
 
Babu Tale pale ni kibarua tu, kazi yake ni kubeba mabegi ya Diamond. Kwahiyo hawezi kuongea chochote kuhusu msanii
Na yule mzee wa matunguli je?
 

sikuungi mkono hoja. Sikiliza Touch na ntakufilisi. Dada anajua sana. ana bidi atafutiwe collabo za kina Yemi allade.
 
Queen Darleen wazamani sana enzi za New Jack Family, Enzi za kina Taqwa-kifo cha mpenzi, Mad Max - Vitu Adim late 90's na early 00's era......Hapo hakuna kiba wala Diamond.
 
Queen Darleen wazamani sana enzi za New Jack Family, Enzi za kina Taqwa-kifo cha mpenzi, Mad Max - Vitu Adim late 90's na early 00's era......Hapo hakuna kiba wala Diamond.
Hivi si aliwahi kuwa Dar Skendo huyu, ama ni Dorleen mwingine?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…