Diamond Platnumz ang'ara kwenye jarida la Billboard kwa kufanya vizuri Youtube

Diamond Platnumz ang'ara kwenye jarida la Billboard kwa kufanya vizuri Youtube

Program Manager

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2018
Posts
2,763
Reaction score
3,955
Mtandao maarufu wa kupanga charts za muziki duniani wa Billboard umeachia makala wakielezea namna ya kupata mafanikio kimataifa kwa kutumia mtandao wa Youtube huku wakimtolea mfano star wa muziki wa Tanzania @Diamondplatnumz

Makala hiyo imeandikwa "Wanamuziki wa Marekani wanatafuta njia za kutoboa kwenye Youtube, Wanapaswa kusoma mikakati ya kufanya na kuachia video kutoka kwa wasanii wa Kiafrika."

Wasanii wa Magharibi wanaweza kujifunza kutoka kwa kile wanachokifanya wasanii wa Kiafrika , haswa wale ambao wamefanikiwa kimataifa," Amezungumza meneja wa 'Youtube Music Trends' Kevin Meenan, ambaye anasimamia ukusanyaji na uchambuzi wa data za chati za Muziki za YouTube. Ameelezea kuwa alivutiwa sana na mbinu pamoja na ubunifu ambao anautumia msanii wa bongo flava wa Tanzania Diamond Platnumz kwenye chaneli yake ya YouTube - sehemu moja tu ya mikakati ya ujasiriamali ambayo inajumuisha kituo cha redio ya FM na TV pamoja na usimamizi kamili wa huduma, kurekodi, kuchapisha na kampuni ya burudani, @WCB_Wasafi.

Kwenye Makala hiyo Kevin Meenan amesema Ukubwa wa diamond kwenye Youtube ni wakustaajabisha akiwa na Subscribers Millioni 3.6 na zaidi ya jumla ya views Millioni 980 huku 80% ya watamazaji wakiwa wanatokea nje ya Tanzania. Kwa kipimo cha kipindi cha kutoka Mei 1, 2019 hadi Mei 1, 2020 Meenan anasema kwamba, kimataifa Diamond alitazamwa zaidi na watu wa Nchini ya Kenya ikifuatiwa na Tanzania na Marekani.

Billboard wameeleza kuwa Msimamizi huyo wa Youtube Trending alishangazwa kukuta Diamond ameweka zaidi ya video 600 kwenye mtandao wa Youtube "Kwa kweli ilibidi nichunguze mara tatu ili kuhakikisha kuwa ilikuwa sawa," Alielezea. Wamesifia kuwa Diamond anaweza kuweka hadi video 20 akitangaza Official video moja tu huku wakitolea mfano wa wimbo wa Jeje ambapo ukiachana na Official video, kuna dance video, cartoon video, lyrics video pamoja na official audio.

Kwenye Makala hiyo Billboard wameelezea kuwa uchunguzi wao umegundua kuwa wasanii wengi ambao wamefanikiwa kufikisha subscribers zaidi ya Million 1 basi huwa wanatazamwa zaidi na watu wa nje ya nchi zao.

101370492_111740247067345_8725964267346259391_n.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtandao maarufu wa kupanga charts za muziki duniani wa Billboard umeachia makala wakielezea namna ya kupata mafanikio kimataifa kwa kutumia mtandao wa Youtube huku wakimtolea mfano star wa muziki wa Tanzania @Diamondplatnumz
.
Makala hiyo imeandikwa "Wanamuziki wa Marekani wanatafuta njia za kutoboa kwenye Youtube, Wanapaswa kusoma mikakati ya kufanya na kuachia video kutoka kwa wasanii wa Kiafrika."
.
Wasanii wa Magharibi wanaweza kujifunza kutoka kwa kile wanachokifanya wasanii wa Kiafrika , haswa wale ambao wamefanikiwa kimataifa," Amezungumza meneja wa 'Youtube Music Trends' Kevin Meenan, ambaye anasimamia ukusanyaji na uchambuzi wa data za chati za Muziki za YouTube. Ameelezea kuwa alivutiwa sana na mbinu pamoja na ubunifu ambao anautumia msanii wa bongo flava wa Tanzania Diamond Platnumz kwenye chaneli yake ya YouTube - sehemu moja tu ya mikakati ya ujasiriamali ambayo inajumuisha kituo cha redio ya FM na TV pamoja na usimamizi kamili wa huduma, kurekodi, kuchapisha na kampuni ya burudani, @WCB_Wasafi.
.
Kwenye Makala hiyo Kevin Meenan amesema Ukubwa wa diamond kwenye Youtube ni wakustaajabisha akiwa na Subscribers Millioni 3.6 na zaidi ya jumla ya views Millioni 980 huku 80% ya watamazaji wakiwa wanatokea nje ya Tanzania. Kwa kipimo cha kipindi cha kutoka Mei 1, 2019 hadi Mei 1, 2020 Meenan anasema kwamba, kimataifa Diamond alitazamwa zaidi na watu wa Nchini ya Kenya ikifuatiwa na Tanzania na Marekani.
.
Billboard wameeleza kuwa Msimamizi huyo wa Youtube Trending alishangazwa kukuta Diamond ameweka zaidi ya video 600 kwenye mtandao wa Youtube "Kwa kweli ilibidi nichunguze mara tatu ili kuhakikisha kuwa ilikuwa sawa," Alielezea. Wamesifia kuwa Diamond anaweza kuweka hadi video 20 akitangaza Official video moja tu huku wakitolea mfano wa wimbo wa Jeje ambapo ukiachana na Official video, kuna dance video, cartoon video, lyrics video pamoja na official audio.
.
Kwenye Makala hiyo Billboard wameelezea kuwa uchunguzi wao umegundua kuwa wasanii wengi ambao wamefanikiwa kufikisha subscribers zaidi ya Million 1 basi huwa wanatazamwa zaidi na watu wa nje ya nchi zao.

MY TAKE: Inabidi Watanzania hasa wapenda burudani na wasanii wengine, waone na kukubali kujifunza kupitia huyu jamaa... HE IS THE REAL DEFINITION OF A FIGHTER AND THE GAME CHANGER

View attachment 1466162

View attachment 1466163
 
Wasanii wa wanaochipukia/wa kiafrika wajifunze kutoka kwake sio akina Chriss brown, Ed sheeran, Justin Bieber coz video moja ya kati ya watu nliowataja hapo views wake ni sawa or zaidi ya video zoooote za YouTube za Diamond.

All in all jamaa anafanya vzuri amebakiza step moja tu nayo ni kuingia rasmi kwenye market ya Marekan
 
Wasanii wa wanaochipukia/wa kiafrika wajifunze kutoka kwake sio akina Chriss brown, Ed sheeran, Justin Bieber coz video moja ya kati ya watu nliowataja hapo views wake ni sawa or zaidi ya video zoooote za YouTube za Diamond
All in all jamaa anafanya vzuri amebakiza step moja tu nayo ni kuingia rasmi kwenye market ya Marekan
Kwa Africa diamond anakimbiza.
Sasa hivi tunataka tuone angalau kuna goma lake lumefikia level ya Gold kama ndugu David Adeleke alivyofanya.
.
Tutatamba hadi muhame hii nchi
 
Wasanii wa wanaochipukia/wa kiafrika wajifunze kutoka kwake sio akina Chriss brown, Ed sheeran, Justin Bieber coz video moja ya kati ya watu nliowataja hapo views wake ni sawa or zaidi ya video zoooote za YouTube za Diamond
All in all jamaa anafanya vzuri amebakiza step moja tu nayo ni kuingia rasmi kwenye market ya Marekan
Kuingia kwenye market ya Marekani sio kitu rahisi maana kule kuna wasanii wengine kushinda hata hii Nijai tunayo shindana nayo wale kila siku watu ni wapya na wao wanataka kutoboa

Afrika yenye waliopo kwenye ramani kidogo huko Marekani ni hawa wakina Burnaboy, Wizkid, Davido,Nasty C unaona kabisa jamaa wanapambana kukaa kwenye ramani ya Marekani na wao.
 
Heaters mwaka huu mnatakufwa kwa kihoro!!

sie tupo na baba laooo.
 
maisha hayajawahi kua sawa, kiba na beki3 wake robidinyo wakihangaika kupost ujio wa kingoma chao kipya huku mwenzao anatolewa mfano na BILLBOARD, dah! sina chakuwaambia kiba & bek3 wako robidinyo isipokua kuwapa pole kwa maumivu mnayougulia mda huu
 
maisha hayajawahi kua sawa, kiba na beki3 wake robidinyo wakihangaika kupost ujio wa kingoma chao kipya huku mwenzao anatolewa mfano na BILLBOARD, dah! sina chakuwaambia kiba & bek3 wako robidinyo isipokua kuwapa pole kwa maumivu mnayougulia mda huu
 
Pia naamini Wanaijeria wapo wengi sana Marekani na nchi za Magharibi ndio maana ni rahisi kutoboa kwa wakina Wiz, Burna na Davido ukilinganisha na sisi watz. Sisi hata Kenya hatumpati kwakuwa na raia abroad.

All in all, Big up Diamond.
Kuingia kwenye market ya Marekani sio kitu rahisi maana kule kuna wasanii wengine kushinda hata hii Nijai tunayo shindana nayo wale kila siku watu ni wapya na wao wanataka kutoboa

Afrika yenye waliopo kwenye ramani kidogo huko Marekani ni hawa wakina Burnaboy, Wizkid, Davido,Nasty C unaona kabisa jamaa wanapambana kukaa kwenye ramani ya Marekani na wao.
 
Back
Top Bottom