Diamond Platnumz apewe shahada ya falsafa ya heshima

Diamond Platnumz apewe shahada ya falsafa ya heshima

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Mwanamuziki nguli anayetamba duniani kwa kazi zake na ukwasi mkubwa Naseeb Abdul Juma Issack almaarufu kama Diamond Platnumz anastahili kupewa tuzo ya heshima ya udaktari wa falsafa na vyuo maarufu duniani kwa jinsi ya mchango wake kwa mtu mmoja mmoja, jamii kwa upana wake, taifa/serikali (kupitia kodi anazolipa).

Ukimya wa taasisi za elimu ya juu duniani zikiwemo za ndani ya Tz unatia shaka kubwa kwasababu Bingwa huyu ame-reform wanamuziki wenzake na kutransform maisha ya vijana duniani kwamba alistahili hata nishani ya rais kama siyo tuzo ya Grammy. Uwezo wa Diamond haulingani na wa Khadija Kopa, Cpt. Komba na Mzee Nnauye ambao hawa wamefanywa/walifanywa Makada nguli wa chama tawala.

Matokeo ya kazi za Diamond katika tasnia ya muziki ni makubwa kuliko matokeo ya kazi za Maprofesa ambao hata wao wamestaafu bila hata single wakati ni wataalam wa muziki kwa ngazi ya uweledi wa uzamivu (PhD). Ziko wapi UDSM, OUT, SAUT, TUDARCO nk? Tunasubiri Mungu ampandishe cheo kwenda kwake ndiyo tumpe tuzo ambayo hatoiona kwa macho yake?

Tz tumpaishe Diamond wetu ili ulimwengu wa nje nao ujumuike nasi katika kumpaisha. Tuzo ya Muziki ya Grammy ndiyo inayoongoza dunia tangu karne ya 20 na ukiipata ile utakuwa na ela ya kuweza kufadhili bajeti ya serikali na kazi zako hazitakwama sokoni hata siku moja.

US ilimpaisha Jacko (Michael Jackson) hadi akaongoza dunia kwa kupata tuzo 100 hadi anafariki, katika hizo, ni Grammy Music Award ndiyo ilimpa kitita kilichomfanya billionaire. Sasa hapa kwetu CCM inamtumia Diamond kwa viwango vya chini mno ambavyo siyo hadhi yake. Siasa ni sumu.

Nadhani dunia imtendee Mondi haki anayostahili. Bila wivu kwa Diamond, Konde Boy hasingefanya bidii na kufanya vizuri kama anavyofanya hivyo Mondi amemtengeneza indirectly. Karibuni tujadili.

1639235155358.png

Taswira kwa hisani ya google.
 
Heshima ipi? Kazi kuleta mapambio tu jibwa we
 
Jamaa anafanya kazi kubwa kaaajiri watu wengi ikiwamo madancer, IT na watu wenye taaluma tofauti imesaidia kupanua fursa ya kupunguza tatizo la ajira nchini lakini pia kampuni yake ya Wasafi inachangia kiasi kubwa kwenye kulipa Serikali kodi
 
Jamaa anafanya kazi kubwa kaaajiri watu wengi ikiwamo madancer, IT na watu wenye taaluma tofauti imesaidia kupanua fursa ya kupunguza tatizo la ajira nchini lakini pia kampuni yake ya Wasafi inachangia kiasi kubwa kwenye kulipa Serikali kodi
Bora umeona hiyo, wengine wanachangia kwa ushabiki wa Yanga na Simba bila kujuwa Mondi anafahamika hadi Hollywood, wakati wao hata Manzese hawajulikani.
 
Ndio ni kweli lakini hebu neileze hii tuzo ya "Granny" unayosema hapa ni wapi waandaji wake? samahani kwa usumbufu
 
Ndio ni kweli lakini hebu neileze hii tuzo ya "Granny" unayosema hapa ni wapi waandaji wake? samahani kwa usumbufu
Wala hakuna usumbufu mkuu,

Sorry! spellcheck ni Grammy NOT Granny.

 
Wala hakuna usumbufu mkuu,

Sorry! spellcheck ni Grammy NOT Granny.

yap! nimekupata shukrani
 
Jamaa anafanya kazi kubwa kaaajiri watu wengi ikiwamo madancer, IT na watu wenye taaluma tofauti imesaidia kupanua fursa ya kupunguza tatizo la ajira nchini lakini pia kampuni yake ya Wasafi inachangia kiasi kubwa kwenye kulipa Serikali kodi
Kina Rostam, Mo, Bakheresa etc nao wapewe nini? Hiyo wasafi sidhani wanafika watu 200 hao niliowata ukijumlisha ajira rasmi na zisizo rasmi ni maelfu ya watu.
 
Tuweke chuki
ushabiki
wivu
utimu
ushirikina

pembeni mondi kawatoa sana vijana huyu jamaa kaupandisha sana mziki wa bongo flavour na swala la grammy anastahili kuchukua huyu mwamba (simba) kama uamini sikiliza namna uimbaji wa harmonize na wengineo wanavoimba vitu ving wamegain kwa mondi

jamaa ni international anyway tutafute pesa kwa nguvu na si majungu
 
Kina Rostam, Mo, Bakheresa etc nao wapewe nini? Hiyo wasafi sidhani wanafika watu 200 hao niliowata ukijumlisha ajira rasmi na zisizo rasmi ni maelfu ya watu.
Mzee baba mtoa mada anazungumzia kiwanda ambacho Serikali haikipi uzito lakini kupitia hicho kiwanda yaani mziki kimemtoa mtu ( Diamond ) ambaye amekuja kuleta mchango mkubwa Sana kwa vijana wengi
 
Aende akahiji huyu kijana, life is too short. Haya yoote ayafanyayo hayana manufaa yoyote kwake.
 
Tuweke chuki
ushabiki
wivu
utimu
ushirikina

pembeni mondi kawatoa sana vijana huyu jamaa kaupandisha sana mziki wa bongo flavour na swala la grammy anastahili kuchukua huyu mwamba (simba) kama uamini sikiliza namna uimbaji wa harmonize na wengineo wanavoimba vitu ving wamegain kwa mondi

jamaa ni international anyway tutafute pesa kwa nguvu na si majungu
Mkuu,
Umeitendea haki mada. Nafikiri Mondi atakutumia hundi.
 
Aende akahiji huyu kijana, life is too short. Haya yoote ayafanyayo hayana manufaa yoyote kwake.
Kuna school of thought kwamba kazi za Mondi zimeajiri vijana wengi kwenye vibanda vya kuuza kazi zake, Ma-DJ wenye vyombo vya muziki nk. Eti mapato ya makundi haya toka kwa baadhi yao ndiyo matoleo kwenye majumba wakfu (nyumba za ibada). Kumbe basi karama ya Mondi imetambuka hadi kwenye ibada licha ya kwamba huenda haendi hija.
 
Back
Top Bottom