Diamond Platnumz badili mwenendo before it’s too late!

Diamond Platnumz badili mwenendo before it’s too late!

Once unauza soul yako tegemea lolote, maana unauza will power yako, unabaki kuwa controlled tu, Ukiambiwa toboa pua unatoboa, vaa gauni unavaa, kula madawa kama ugali unakula, sababu huna nguvu ya kupinga, na ndicho anachotaka lucifer akutumie kisha akuteketeze milele.
 
Mbaya mbovu ya wasanii wengi kutumia vilevi ni vile wanataka ku maintain vibe wakiwa juu ya stage,pili watu maarufu wanakuwa na pirukushani nyingi kiasi kwamba hata muda wa kupumzika unakuwa finyu hivyo anajikuta anaingia kwenye vilevi kama sehemu ya kumpumzisha na kumuasha vibe ili pesa siku nyengine iingie!.

Refer msanii mkubwa kama Michael Jackson alishawahi sema kitu ambacho alikuwa hakipendi ni tour!!!, Na hizo ndizo zilikuwa zinamuingizia mshiko maana msanii bila show sawasawa na kazi bure!,Sasa kumaintain hiyo ili aendane na vibe la watu kama hatatumia midawa hapo itakuwaje!,mashabiki mtalalama mmetoa hela zenu halafu hamna kitu na mtu anatandika show ya masaa kadhaa..

Nafikiri ni muhimu wasanii wahaswe na wafatiliwe maana nje na kazi wanafamilia pia na watu wanaowategemea.
 
Tukubaliane kuwa yule mama yake naye ni tatizo kubwa, hivi halioni hilo kwa mwanae? Ameweza kucontrol mangapi ya Diamond hilo limshinde? Diamond ana access na wataalamu wa kila aina angetaka wamsaidie kuishinda addiction asingeshindwa.

Diamond wa kipindi cha wema alikuwa amekonda bado kapauka pauka kiasi, Diamond wa kipindi cha Zari alikuwa ana ka mwili, anavaa smart anapendeza, akivaa suti inakaa, huyu Diamondi wa Tanasha na wa Zuchu aisee pamoja na hela zote hatazamiki, kakondeana, ngozi imevutika, ana mirasta yaani haeleweki.

Anyways: It is never too late, kama ni addict kweli bado ana nafasi ya kupona, watu wake hawawezi kumwambia ukweli yamkini wanafaidia na yeye kuwa alivyo. Na pakisambaratika kila mtu atabeba mbao zake atasambaa!

Binafsi ntasikitika sana tukimpoteza huyu kijana wa Tandale aliyefanikiwa kufika mahali ambapo wasanii wetu hawakuweza kufika, “Super star”.
Bora wee uduguu umesemaa, kila siku najiuliza km mama ake anaweza kumu control, ndo ashindwe kwa hilii? Khaaah
 
Mbona kabinti kenyewe nacho tayari kameshaanza kulamba sema ndio kapo ktk early stage.

Ndio maana hakichagui cha kuimba, mara mibuno, mala sokomeza kavukavu, mara nailamba yote.

Ni athali za madawa hizo.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Lisemwalo lipo.

Kitu kinachofanya niamini haya ni namna alivyoshindwa kuitumia nafasi nzuri alipokuwa akivuma kila pande za Africa.

Diamond alikuwa na nafasi kubwa sana ya kufanya makubwa kwenye muziki wake, alikuwa na wakina Burna Boy, Wizkid, Davido ila sasa hivi siyo wenzake tena. Sasa hivi hata watoto wa juzi tu wakina Rema wanamkimbiza kwenye muziki.

Lazima kuna tatizo.
 
Wewe ni mpumbavu na isitoshe wewe ni teja mtumiaji.

Wewe unafikiri kwa nini serikali inapambana kudhibiti madawa ya kulevya kwa watu?

Kama mtu kutumia madawa ya kulevya ni "Maisha ya mtu" kwa nini serikali iingilie kati kupambana na wauzaji madawa ya kulevya?

Kwa nini isi ingilie walevi wanywa pombe?
Boss una proof jamaa anatumia madawa?
 
Lisemwalo lipo.

Kitu kinachofanya niamini haya ni namna alivyoshindwa kuitumia nafasi nzuri alipokuwa akivuma kila pande za Africa.

Diamond alikuwa na nafasi kubwa sana ya kufanya makubwa kwenye muziki wake, alikuwa na wakina Burna Boy, Wizkid, Davido ila sasa hivi siyo wenzake tena. Sasa hivi hata watoto wa juzi tu wakina Rema wanamkimbiza kwenye muziki.

Lazima kuna tatizo.

Tajir unataka Mondi awe kama Burna boy au wizkid ... Jamaa amepambana na bado anaendelea kupambana kwa nafasi yake so you have to respect that
 
Mama yake anachojali ni kijana wake awe single ili awe na uhakika wa kuzitumbua mali za mwanae. Akioa au kuwa kwenye mahusiano hatakua na nguvu kwenye mali za mwanae. Hivyo nguvu nyingi anawekeza kuvunja mahusiano yoyote serious ya jaba
Unajua shida ya familia zetu mtu akishakuwa ana pesa na nguvu ya pesa hata kusemwa au kushauriwa inakuwa shida….
Kuna wazazi wengi huwaogopa watoto wao kwakuwa wanazo pesa..hilo ni shida
Na muda mwingine wazazi wanaweza kuwa hawajui lakini watu wengine wakajua…..
 
Tangu tumpoteze Cowbama Ngwair


Tangu tumpoteze Whitney Houston


Tangu tumpoteze DMX


Tangu tumpoteze Maradona


Wote hao Kwa visa mbalbali vya madawa ya kulevya Sina hamu na madawa ya kulevya!


Wote Hawa tuliowapoteza zilianza kama tetesi na mwisho wake Kila mtu anajua kilichowakuta!


Hata hapa tanzania waathirika wote wa madawa ya kulevya ilianza kama tetesi

Ray C
Lord Eyez
Chid Benz
Langa
Pauline Zongo

Wote Hawa ilikuwa tetesi



Diamond Platinum kama ni kweli unatumia acha haya makitu unaenda kujizika. Kama hutumii endelea kutushushia Magoma makaleeeeeeeee ...


"We Zombieeeee"



Nimeandika Hii comment Leo tarehe 28.10.2023 kama sehemu ya ushauri.
 
Tajir unataka Mondi awe kama Burna boy au wizkid ... Jamaa amepambana na bado anaendelea kupambana kwa nafasi yake so you have to respect that
Anastahali pongezi kwa alipofika ila ukitoa mafanikio yake kifedha kwenye muziki wake alifikia hatua ambayo angeweza kufanya makubwa zaidi ila ni kama akapotea kwa kufanya muziki wa nyumbani zaidi.

Mwaka 2014 Diamond anatoa Remix ya Number One na kushirikisha Davido kama msanii anayefanya vizuri East Africa na akaweza kupata collabo kutoka Nigeria. Burna Boy alikuwa anafanya collabo na wakina AKA kwenye All Eyes On Me.

Ukiangalia safari ya muziki kwa Burna Boy miaka ya 2016 anatoa Pree Me kama msanii wa kawaida tu pale Nigeria wakati huo Diamond ndiyo anatamba na kufanya collabo na AKA, Akothee. Mpaka 2017 anatoa wimbo na Ne-Yo.

Mpaka 2019 Harmonize akaweza kufanya kazi na Burna Boy, hapo ndiyo Burna akatoa Album ya African Giant iliyomtambulisha Duniani. Yani wakati Diamond anatoa A Boy from Tandale 2018, Burna Boy alikuwa bado anajitafuta.

Sasa hivi Burna Boy yupo kwenye level nyingine kabisa ambayo Diamond angeweza kuifikia ila sijui nini kilimkwamisha.
 
Back
Top Bottom