Diamond Platnumz hili la kumfananisha demu (msichana) wako na Yesu (Mungu) utuombe radhi wakristo na utubu au wimbo wake ufungiwe na BASATA

Diamond Platnumz hili la kumfananisha demu (msichana) wako na Yesu (Mungu) utuombe radhi wakristo na utubu au wimbo wake ufungiwe na BASATA

Nimeusikiliza wimbo mpya wa Diamond Platnumz uitwao ongeza kiukweli anatakiwa atafute mhariri wa mashairi na mistari yake. Kwenye ngoma ya ongeza anasema "we ndo wangu yesu mkombozi sa mbona unaniacha mwenyewe" anamuongelea mwanamke/ msichana/demu wake.

Kwa hili Diamond hapana umeenda mbali mno na umetukosea Wakristo. Hivi mkristo aimbe wimbo amljnganishe demu wake na Mtume Mohammad au Allah atakuwa sawa?

Kwetu Wakristo Yesu ni Mungu kweli, mtu kweli Yohana Mtakatifu 1:1-10. Yesu ni Mungu mwana katika nafsi tatu za Mungu zinazofanya Utatu Mtakatifu.

Yesu aliacha kiti chake cha nzi kule mbinguni akauvaa mwili akashuka duniani ili atufie na kutukomboa sisi na dhambi zetu. Alisulubiwa akafa, akazikwa siku ya tatu akafufuka na sasa ameketi mkono wa kuume wa Mungu Baba na hapa tulipo tunasubiri arudi aje awahukumu walio hai na wafu. Maana ameahidi anakwenda kwa Baba kutuandalia makao na atakuja kutuchukua ili alipo nasi tuwepo. Je ni Yesu huyu wa kumlinganisha na demu wake kweli Diamond Platnumz?

Yesu huyu ambaye alikuwepo kabla ya ulimwengu kuumbwa ambaye maandiko yanasema vitu vyote viliumbwa kwa jina lake na pasipo yeye hakuna kilichoumbwa? Huyu ndiyo wa kumlinganisha na demu.


Ni kweli sanaa inahitaji ubunifu lakini siyo kwa kiwango hiki Diamond aombe radhi kwa kweli au wimbo wake ufungiwe na BASATA.
Sawaaaa...lakini

Hivi kweli Mungu anasifa ya kufa...tena siku tatu jamani jamani duuuh
 
Shida ya kuanzisha na kuchangia uzi kwa kukurupuka ndio hizi na wachangiaji wengi naona mmesapoti bila kufuatilia. Diamond amesema

" .... wewe ndio wangu yesu mkombozi sa mbona petro unaniacha mwenyewe..."

Naona umetoa neno petro ili kuhalalisha ulivyo elewa wewe. Hapo kalinganisha kitendo cha yeye kuachwa sawa na petro alivyo muacha yesu. Sijaona kosa mimi hapo zaidi tu niseme kwamba jamaa ni mbunifu.
Kwenye Ukristo hakuna binadami mwenye hadhi sawa na Yesu, mwambieni amfananishe demu wake na mtume wake.
 
Tumpende tu kwani wangekuwa wenzetu wangemkata kichwa.
Tujitofautishe na hao wanyama
 
Ni makufuru kumlinganisha Yesu na girl friend wake, lakini pia ni makufuru kumwita Yesu Mungu Muumba wa mbingu na dunia.

Soma Mathayo 16:16,17 Simoni Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”17 Yesu akamwambia: “Mwenye furaha ni wewe, Simoni mwana wa Yona, kwa sababu mwili na damu havikukufunulia hilo, bali Baba yangu aliye mbinguni ndiye aliyekufunulia.

Yohana 14; 28 Mlisikia nikiwaambia, ‘Ninaenda, nami nitakuja tena kwenu.’ Kama mngenipenda, mngeshangilia kwamba ninaenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.
Hoja umenielewa? Jikite kwenye hoja, achana na hayo marufuku ya mapepo
 
Yohana 1:1

“Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.”

Yohana 17:3

Uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na yule uliyemtuma, Yesu Kristo.

Yohana 20:17

Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania, kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu, nawe uwaambie, ‘Ninapanda kwenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.

Bottomline: Kuna Mungu na mungu.

Ikiwa Yesu anamwabudu Mungu Yehova kwanini wewe umwabudu mungu Yesu?
Anzisha mada mkuu, inaonekana unatumiwa vema na mapepo. Fungua thread tukuchomoe hayo majini
 
Kama hupendi usisikilize na usinunue muziki wake.

Kwa watu wengine Yesu ni Mwanafalsafa tu.
Hao ni wengine kama ulivyosema, hapa hoja haihusu watu wengine, vinginevyo Domo angehesabiwa kuwa yuko sawa. Ukiwa mtu mwingine usiingie kwenye huu uzi
 
Ingekuwa upande wa pili Fatwa ingemhusu.

Kama Mark Basseley Youseff wa Innocence of Muslims au kilichowapata akina Charlie Hebdo.
Sema ingekuwa upande wake "domo mwenyewe." Hii sio bahati mbaya, ni kusudi kabisa
 
Hao ni wengine kama ulivyosema, hapa hoja haihusu watu wengine, vinginevyo Domo angehesabiwa kuwa yuko sawa. Ukiwa mtu mwingine usiingie kwenye huu uzi
Unaingilia uhuru wa kikatiba wa watu kujieleza.

Ukishaweka uzi JF, mwanachama yeyote anaweza kuchangia.

Hivyo usiniwekee mipaka kwenye kuchangia.

Zaidi, mipaka yako ni ya kijinga.Kwa sababu huna uwezo wa kunizuia kuchangia. Unaweka sheria ya kijinga usiyoweza kui enforce.

Ujinga juu ya ujinga!

Kama unataka mazungumzo ya faragha, nisichangue, tuma PM kwa rafiki zako unaotaka kujadikiana nao.

Inaonekana huelewi hata maana ya Public Forum na Freedom of Speech.

Ndiyo maana huwezi kunielewa nikikwambia Domo ametumia haki yake ya kikatiba tu.

Kama hupendi alivyofanya unaruhusiwa kususia kusikiliza nyimbo zake.

Hiyo pia ni haki yako ya kikatiba.
 
Amtumumie Mwanafalsafa wa dini yake.
Inawezekana katika dini yake Yesu ni Mwanafalsafa.

Sasa usimzuie kumtumia mwanafalsafa wa dini yake.

Yesu ana maana tofauti kwa watu tofauti.

Wengine wanamuona Masiha mwana wa Mungu.

Wayahudi wenyewe waliomuona tangu anazaliwa wamemkataa, wamesema huyu si Masiha. Ni Rabbi tu, Mwalimu tu wa kawaida. Si mwana wa Mungu.

Wewe Mndengereko umemjua jana Yesu, kwa kuletewa dini na wakoloni, waliokuja kukunyanyasa na kukufanya mtumwa, unataka kujifanya unamjua Yesu kuliko wenyewe Wayahudi?

Wengine wanamuona mtume.

Wengine wanamuona mwanafalsafa.

Wengine wanamuona tapeli.

Wengine wanamuona kichaa.

Sasa, usilazimishe unavyomuona wewe, kika mtu amuone hivyo.

Na mimi sitaki kulazimisha ninavyomuona mimi umuone wewe.
 
Unaingilia uhuru wa kikatiba wa watu kujieleza.

Ukishaweka uzi JF, mwanachama yeyote anaweza kuchangia.

Hivyo usiniwekee mipaka kwenye kuchangia.

Zaidi, mipaka yako ni ya kijinga.Kwa sababu huna uwezo wa kunizuia kuchangia. Unaweka sheria ya kijinga usiyoweza kui enforce.

Ujinga juu ya ujinga!

Kama unataka mazungumzo ya faragha, nisichangue, tuma PM kwa rafiki zako unaotaka kujadikiana nao.

Inaonekana huelewi hata maana ya Public Forum na Freedom of Speech.

Ndiyo maana huwezi kunielewa nikikwambia Domo ametumia haki yake ya kikatiba tu.

Kama hupendi alivyofanya unaruhusiwa kususia kusikiliza nyimbo zake.

Hiyo pia ni haki yako ya kikatiba.
Povu la nini? Imesema mwenyewe WATU WENGINE waanaamini hicho ukitakacho. Sasa huu uzi haujagusia watu wengine, umeongelea kuhusu wenye imani ya Mungu wa kweli. Kumbe kuja humu na hoja za watu wengine ni kudhihirisha ujinga wako, bali mimi sina uwezo wa kukuzuia usichangie mada. Waweza changia vyovyote vile utakavyo, lakini yatakuwa mawazo ya WATU WENGINE!!
 
Inawezekana katika dini yake Yesu ni Mwanafalsafa.

Sasa usimzuie kumtumia mwanafalsafa wa dini yake.

Yesu ana maana tofauti kwa watu tofauti.

Wengine wanamuona Masiha mwana wa Mungu.

Wayahudi wenyewe waliomuona tangu anazaliwa wamemkataa, wamesema huyu si Masiha. Ni Rabbi tu, Mwalimu tu wa kawaida. Si mwana wa Mungu.

Wewe Mndengereko umemjua jana Yesu, kwa kuletewa dini na wakoloni, waliokuja kukunyanyasa na kukufanya mtumwa, unataka kujifanya unamjua Yesu kuliko wenyewe Wayahudi?

Wengine wanamuona mtume.

Wengine wanamuona mwanafalsafa.

Wengine wanamuona tapeli.

Wengine wanamuona kichaa.

Sasa, usilazimishe unavyomuona wewe, kika mtu amuone hivyo.

Na mimi sitaki kulazimisha ninavyomuona mimi umuone wewe.
Kwani Yesu Kristo alikuja kwa ajili ya kila mtu?
 
Kwann asingeimba mtume muhammad bu anawajua Muslims hawapend ujinga ila wakrsto wastaarabu maskini ya Mungu
 
Waweza kuta mleta mada ni babu tale kakaa pembini anaaNgalia mnavyohangaika na dini vs diamond...
 
Back
Top Bottom