Bongo kila kitu vice versa mbele msanii analipwa kwa nyimbo yake kupigwa kwenye redio, huku msanii halipwi na kwenye show lazima ufanye bure usipofanya nongwa mara utaambiwa unadharau, kiburi lkn hawaangalii msanii kawekeza kiasi gani ktk ile kazi.Alafu ile movement iliyo anzishwaga na wasanii, kulipwa baada kazi zao kupigwa redioni sijui imeishia wapi au sijui ndio uoga wao kwa hizi media mpaka wana sahau haki zao muhimu.
Mimi Diamond namsikilizaga sana, hana matatizo ila watu wanamuona ana matatizo sababu anataka win win yaani kila upande unufaike na hapo ndipo unapogombana na washika dau (media) .Wakati wenzetu wa ulaya wanaamini nyimbo ni kivutio kinachowavutia wasikilizaji wasikilize redio zao na ndio maana kwa kujua umuhimu wa wasanii wanawalipa.
Kwanza kwa dunia ya sasa hata ukisoma baadhi ya tafiti, social media zimepunguza namba za wasikilizaji redio na watizamaji TV na ndio maana kila redio sasa hivi nazo zinatumia hizi social media platform ili kutafuta wasilikilizaji (insta, fb, YouTube) , so nikimuona msanii analia eti apewi promo na mshangaa wakati Kuna platform kibao za kupromoti kazi yako na ukaingiza hela, wakati kwenye redio hela huingizi na kwenye show unapiga bure.
Hizi media zijifunze kuheshim kazi za watu na mziki sio kazi ya milele unapokuwa wa moto ndio mda wa kupiga hela, ukishapita muda wako ndio basi, unabaki kuwa mtu wa lawama na kulialia kama Q chief na TID na wengineo.
Mimi nina mwaka wa pili nikifungua redio na sikiliza mpira TBC basi, ila TV vipindi vyangu ni habari Star TV, ITV, BBC swahili , Kipindi cha mahojiano EATV saa moja jioni baada ya hapo Trace Muziki, MTV base , NGE W (documentary za wanyama).Habari nyingine nitazisoma kupitia kwenye simu na PC yangu.
Mziki wa bongo nikimtoa Jide, Fa, AY, Nature, Prof Jay na Sugu hawa kidogo wapo vizuri, lkn hao wengine wana maisha mabovu, ninaowafaham mm Inspector, PNC na Big black (solid ground family wazee wa Bush party, yupo Tbt karibia St Mary College kwa mama yake hali yake ni mbaya) , sijui Blue maana nyumba yake ya Tabata mvua ikinyesha mnatega kambale ndani.