Aussie the land of opportunities, pako vizuri....jiandae na safari ya masaa zaidi ya 20 , Dar-Dubai, Dubai-Perth/Sydney/Melbourne, ngozi nyeusi hawajawa wengi sana lakini huwezi kuwakosa wakenya na wanaija, waasia hasa wachina wapo wa kumwaga.Kuna yeyote ana uzoefu wa life la Australia, huenda labda alienda kule kimasomo, au mpaka sasa yupo huko anasoma, au anafanya kazi, au aliwahi kwenda kwa sababu yoyote ile? Naomba mwenye experience ya huko anijuze shauku yangu nataka kuzamia huko kwa kupitia njia ya kwenda kusoma. Halafu ikiwezekana niunganishe mazima.
Sent using Jamii Forums mobile app
Canada has become the new El Dorado for many African migrants, who have seen Europe and the United States close their borders.
But they face a dangerous journey across South and North America. Every year, some of them die on their way to a better life, amid widespread indifference to their plight.
For five months, our reporters followed Rosette and her family from DR Congo on this long, dangerous odyssey across ten countries. In the space of five months, Rosette and her family have travelled more than 20,000 kilometres – risking their lives......
asante sana nilitegemea jibu kama ili kutoka kwako mimi nimechangia mada tu kuhusu msaada sitegemei mtu yeyote hapa sky is the limit brother.Mkuu kwa mfano mimi nakualika wewe kama nani yangu au kwenye function gani?
Nadhani wengi mnadhani mualiko wowote tu unatosha kupewa visa ila hamjui ni lazima muwe na ukaribu na huyo mtu na wewe as a visitor uonyeshe upo well established nyumbani na utarudi ili upewe visa kigezo ambacho vijana wengi hawana maana ndo wanatafuta maisha. Kama haupo vizuri bongo kwa maana ya a stable job, assets, ndoa, watoto, na hela visa ya kutembea kwa mualiko ni mtihani.
Niseme tu diapora wanatumia internet hii hii kutafuta hizo internships na kazi mnazotaka wawajulishe sio kwamba wanaenda kwenye hizo organizations in person. Wewe muhitaji ni bora kuwekeza nguvu nyingi kuzitafuta hizo nafasi, ukikpata ndo mshauriane na mtu wako wa karibu aliyeko huko. Hao diaspora wana majukumu mengine hawawezi kuacha majukumu yao na kushinda online siku nzima kukutafutia internships na kazi. Tujiongeze hapa tuache uzembe na lawama za reja reja.
Hakuna mtu anaogopa kuwapa muongozo ila you're asking way too much hata kwa mambo yaliyo ndani ya uwezo wenu. Mimi sina muda wa kumtafutia mtu chuo, passport au internship huo muda sina kabisa Ila akipata nitamsaidia all the way through ndo maana nilisema lazima ucheze part yako as well hakuna mtu ataacha majukumu yake kukusaidia wewe kila kitu.
asante sana nilitegemea jibu kama ili kutoka kwako mimi nimechangia mada tu kuhusu msaada sitegemei mtu yeyote hapa sky is the limit brother.
Ndio maana tumejazana hapa Tz hatutokiWabongo wengi wavivu na hawajui kujiongeza zaidi ya lawama tu
Weka picha tuaminiAcha uongo .tena ww uliyeandika huu Uzi ndo ulikuwa wa kwanza kunikatisha tamaa na ukaniambia niwe SHOGA ili nitimize ndogo zangu alfu Leo hii unaandika uongo ili kuonesha jamii kuwa ww ni kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu.mkuu acha kujitetea na kumbuka MTU mwenye sifa ya kusaidia MTU hajali kuwa anayetaka kusaidiwa ana kitu au hana ,kutoa ni moyo mkuu
Asante kwa kuchangia mawazo brother.That's the mentality. Ukijisaidia at least halfway watu watakusaidia be it wabongo wenyewe au watu baki. Nimesaidiana na watu baki kabisa ambao leo tumegeuka ndugu wengine wapo kutoka jukwaa hili hili la JF. Binafsi hiyo roho mbaya au kusema wabongo hawashirikiani naonaga ni story tu. Kama wao walifika basi inawezekana.
Bank statement unaweza tafuta ya mtu unaemfaham awe na mpunga kdgo, along with barua kusema atalipia/gharamia shule na pesa za matumizi yako ya kila mwez..Asante, hivyo vyuo vinavyotoa hizi post graduate mpaka ufike ndio navihitaji binafsi nimefuatilia poland gharama zao ziko reasonable bank statement ndio kipengele.
Vipi mawakala wa kazi huko na gharama zao!?
Nyumbani kumenogaa 🤣🤣🤣🤣🤣Mimi kinacho nifurahisha ni kuona kua zile thd za kuponda wabeba box hapa JF hazipo tena,badala yake hata wale wapondaji nao wanataka connection,
Nakomaa na box,nitarudi kusoma povu.
😀😀😀😀
Watu wanapenda kulipwa kwa dolari hata kama ni dola 2😂Mimi kinacho nifurahisha ni kuona kua zile thd za kuponda wabeba box hapa JF hazipo tena,badala yake hata wale wapondaji nao wanataka connection,
Nakomaa na box,nitarudi kusoma povu.
😀😀😀😀
Nikiendelea kujifariji we unapungukiwa na nin kwenye maisha yakoEndelea kujifariji kama inakupa nafuu.
Today, more than 10 million Filipinos—or about 10 percent of the population—are working and/or living abroad ........... When the Philippines launched an overseas employment program in the 1970s, the thrust was finding labor markets: The state not only promoted Filipino workers to the oil-rich but labor-short Gulf Cooperation Council (GCC) countries, it also sold these uncharted Middle East destinations to Filipinos. By the latter half of the 1970s, as deployment and competition with other origin countries increased, surfacing labor migration problems (including poor working conditions and abuse by employers) prompted the government to address migrant welfare and protection. As destinations diversified and women joined the labor migration flows, the protection aspect assumed more importance........ The Philippines: Beyond Labor Migration, Toward Development and (Possibly) Return
🤣🤣🤣 dah kwanini Ulete😆Aah mwalimu mpwayungu village naona leo umetema point. Vipi na wewe ulijaribu kupaa mbele ukaletewa figisu sio.
Mimi nlidhani ungeishia pale Lyandembela au Kivalali, au ukienda mbali saana basi Ulete (kidding)
Haaahaha safari kama hizi kizazi cha sasa cha wabongo hawawezi ndio maana hata ma shoga wameongezeka. Kizazi cha zamani watu walikua wanatambaa toka Pakistan wanakatisha Balkan hadi wanaingia ulaya, chakula ni mkate na maji. Hawa ma yoyoo wa sasa wanataka connection halafu na kuhifadhiwa juu na kazi uwatafutie. Hizi ni trip za wacongo, wakenya, wanaija, waghana na mataifa wengine wagumu wa africa sio hawa wa kubana pua eti wahifadhiwe. 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣Wagumu toka sehemu mbalimbali na safari zao kuelekea Marekani ya Kaskazini
Ungana nasi kwa kutazama video hii kufuatilia mguu kwa mguu toka wakiwasili jijini Sao Paolo Brazil wakijifanya raia wa Angola ktk utalii Brazil kisha wanaanza safari kwenda Canada.
Safari hii ya Wakongomani toka Congo wanaoingia Brazil bila viza kisha wanakutana na wahamiaji wengine toka nchi za China, Morocco, Mali, Senegal, Somalia, Nepal, Nigeria and Bangladeshi kwa miezi mitano wanakatiza mito misitu na barabara ktk nchi kumi za bara la Marekani ya Kusini kabla ya kuingia Marekani nia ni kufika nchini Canada.
Safari hii ya kilometa 20,000 wanakutana wa wahamiaji wengine toka nchi za Caribbean na Latino America ambao pia lengo lao ni kufika Marekani na Canada. Wakongomani lengo ni kufika jimbo la Quebec Canada linalotumia lugha ya Kifaransa kama Congo.
Safari hii inajumuisha kutembea kwa miguu, kupanda basi, taxi, punda, boti , ngalawa na kushirikisha wenyeji wa nchi hizo za Latin America ktk kuonesha njia za vichochoro vijijini zisizo ktk ramani za GPS maana wahamiaji wanatumia simu janja smart phone kutafuta welekeo kupuguza malipo kwa wavushaji watu kwa magendo pale inapowezekana.
Njiani katika njia za panya zilizobatizwa "Njia ya Kuzimu" kukwepa askari wa uhamiaji, kunaonekana utelezi utokanao na mvua zisizokoma za misitu minene ya tropiki, matope yafikayo ugokoni, makaburi yasiyo na jina wala alama za imani zao kwani hao wahamiaji waliopoteza maisha na sasa wamelala udongoni hata kaburini utambulisho wao haujulikani.
Nchi nyingi kama Colombia, Ecuador na Panama wameongeza vikwazo ktk vituo vya mipaka rasmi kutokana na mbinyo toka serikali ya Marekani. Hivyo wahamiaji na watu wote wanaojihusisha na biashara ya kusafirisha watu hutumia njia za vichochoroni kukwepa askari hao.
Pamoja na hayo bado kuna ongozeko kubwa la wahamiaji wanaoelekea Marekani ya Kaskazini wakiwa na imani ya kutafuta fursa na maisha bora zaidi. Wenyeji wa vijiji vya ndani ndani Colombia na Ecuador wanashangazwa na ari bila kusahau hamasa ya kusonga mbele ya hawa wageni toka nchi za mbali.
Watu watajiuliza unawezaje kukatiza nchi zaidi ya 10 salama bila kudhuriwa na wenyeji au magenge ya kutorosha watu mipakani.
Sababu ni kuwa hii ni biashara kubwa inayoingiza kipato na makundi ya waliokuwa wanasafirisha madawa ya kulevya sasa wamejiingiza ktk biashara hii ya kusafirisha watu. Hivyo wakubwa wa magenge haya hawataki kusikia mtu kakabwa au kina mama kubaka n.k na kuwataka wote wanaojihusisha na biashara hii ya kuvusha watu kimagendo mipakani kuwalipa 'kodi' ma drug lords na pia kuhakikisha wageni hao wanamaliza safari salama ili njia zao ziendelee kuaminiwa na maelfu ya wageni hawa waendao Marekani ya Kaskazini. Yeyote atakaye mdhuru mgeni huadhibiwa kwa adhabu kali na wababe hawa wa biashara hii ya kusafirisha wageni.
Endelea kusoma:
Source: France 24
Wahamiaji: Safari toka Congo kupitia Brazil mpaka Canada kwa miguu
Ungana nasi kwa kutazama video hii kufuatilia mguu kwa mguu toka wakiwasili jijini Sao Paolo Brazil wakijifanya raia wa Angola ktk utalii Brazil kisha wanaanza safari kwenda Canada. Safari hii ya 'Wakongomani' toka Congo na nchi za Maziwa Makuu pia Afrika ya Mashariki wanaoingia Brazil bila...www.jamiiforums.com
wabongo kwenye kusaidiana bado sana mfano mtu ana kila kitu passport,nauli na hela ya kujikimu akiwa mfano marekani kupata mchongo wa kwenda mbele inakua mziki wakati kuna mwaliko tena mtu anaweza kukulipa kidogo kufidia muda wako,kuna internship tunaweza kuonganishiana ata kwa malipo siyo mbaya au kusaidiana link ya vyuo vya bei nafuu kabisa ila kwa mbongo hapo kipengele kukupa mwongozo tuna ogopana sana..
Povu langu wewe si Mbongo piaHaaahaha safari kama hizi kizazi cha sasa cha wabongo hawawezi ndio maana hata ma shoga wameongezeka. Kizazi cha zamani watu walikua wanatambaa toka Pakistan wanakatisha Balkan hadi wanaingia ulaya, chakula ni mkate na maji. Hawa ma yoyoo wa sasa wanataka connection halafu na kuhifadhiwa juu na kazi uwatafutie. Hizi ni trip za wacongo, wakenya, wanaija, waghana na mataifa wengine wagumu wa africa sio hawa wa kubana pua eti wahifadhiwe. 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
POVU RUKHSA!
kaka komaa mwenyewe ukitegemea mtu muda utakuacha bure hakuna atayekupa msaada hapa.Hapo kwenye internship zipo, ila kuzipata ni issue
Diaspora mtusaidie kama mna njia rahisi
Hapo kwenye internship zipo, ila kuzipata ni issue
Diaspora mtusaidie kama mna njia rahisi
Hapo kwenye internship zipo, ila kuzipata ni issue
Diaspora mtusaidie kama mna njia rahisi