Diaspora Hawatoi connection?

Diaspora Hawatoi connection?

Kuna yeyote ana uzoefu wa life la Australia, huenda labda alienda kule kimasomo, au mpaka sasa yupo huko anasoma, au anafanya kazi, au aliwahi kwenda kwa sababu yoyote ile? Naomba mwenye experience ya huko anijuze shauku yangu nataka kuzamia huko kwa kupitia njia ya kwenda kusoma. Halafu ikiwezekana niunganishe mazima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Aussie the land of opportunities, pako vizuri....jiandae na safari ya masaa zaidi ya 20 , Dar-Dubai, Dubai-Perth/Sydney/Melbourne, ngozi nyeusi hawajawa wengi sana lakini huwezi kuwakosa wakenya na wanaija, waasia hasa wachina wapo wa kumwaga.
 
Wagumu toka sehemu mbalimbali na safari zao kuelekea Marekani ya Kaskazini

Ungana nasi kwa kutazama video hii kufuatilia mguu kwa mguu toka wakiwasili jijini Sao Paolo Brazil wakijifanya raia wa Angola ktk utalii Brazil kisha wanaanza safari kwenda Canada.

Safari hii ya Wakongomani toka Congo wanaoingia Brazil bila viza kisha wanakutana na wahamiaji wengine toka nchi za China, Morocco, Mali, Senegal, Somalia, Nepal, Nigeria and Bangladeshi kwa miezi mitano wanakatiza mito misitu na barabara ktk nchi kumi za bara la Marekani ya Kusini kabla ya kuingia Marekani nia ni kufika nchini Canada.

Safari hii ya kilometa 20,000 wanakutana wa wahamiaji wengine toka nchi za Caribbean na Latino America ambao pia lengo lao ni kufika Marekani na Canada. Wakongomani lengo ni kufika jimbo la Quebec Canada linalotumia lugha ya Kifaransa kama Congo.

Safari hii inajumuisha kutembea kwa miguu, kupanda basi, taxi, punda, boti , ngalawa na kushirikisha wenyeji wa nchi hizo za Latin America ktk kuonesha njia za vichochoro vijijini zisizo ktk ramani za GPS maana wahamiaji wanatumia simu janja smart phone kutafuta welekeo kupuguza malipo kwa wavushaji watu kwa magendo pale inapowezekana.

Njiani katika njia za panya zilizobatizwa "Njia ya Kuzimu" kukwepa askari wa uhamiaji, kunaonekana utelezi utokanao na mvua zisizokoma za misitu minene ya tropiki, matope yafikayo ugokoni, makaburi yasiyo na jina wala alama za imani zao kwani hao wahamiaji waliopoteza maisha na sasa wamelala udongoni hata kaburini utambulisho wao haujulikani.

Nchi nyingi kama Colombia, Ecuador na Panama wameongeza vikwazo ktk vituo vya mipaka rasmi kutokana na mbinyo toka serikali ya Marekani. Hivyo wahamiaji na watu wote wanaojihusisha na biashara ya kusafirisha watu hutumia njia za vichochoroni kukwepa askari hao.

Pamoja na hayo bado kuna ongozeko kubwa la wahamiaji wanaoelekea Marekani ya Kaskazini wakiwa na imani ya kutafuta fursa na maisha bora zaidi. Wenyeji wa vijiji vya ndani ndani Colombia na Ecuador wanashangazwa na ari bila kusahau hamasa ya kusonga mbele ya hawa wageni toka nchi za mbali.

Watu watajiuliza unawezaje kukatiza nchi zaidi ya 10 salama bila kudhuriwa na wenyeji au magenge ya kutorosha watu mipakani.

Sababu ni kuwa hii ni biashara kubwa inayoingiza kipato na makundi ya waliokuwa wanasafirisha madawa ya kulevya sasa wamejiingiza ktk biashara hii ya kusafirisha watu. Hivyo wakubwa wa magenge haya hawataki kusikia mtu kakabwa au kina mama kubaka n.k na kuwataka wote wanaojihusisha na biashara hii ya kuvusha watu kimagendo mipakani kuwalipa 'kodi' ma drug lords na pia kuhakikisha wageni hao wanamaliza safari salama ili njia zao ziendelee kuaminiwa na maelfu ya wageni hawa waendao Marekani ya Kaskazini. Yeyote atakaye mdhuru mgeni huadhibiwa kwa adhabu kali na wababe hawa wa biashara hii ya kusafirisha wageni.

Canada has become the new El Dorado for many African migrants, who have seen Europe and the United States close their borders.

But they face a dangerous journey across South and North America. Every year, some of them die on their way to a better life, amid widespread indifference to their plight.

For five months, our reporters followed Rosette and her family from DR Congo on this long, dangerous odyssey across ten countries. In the space of five months, Rosette and her family have travelled more than 20,000 kilometres – risking their lives......

Endelea kusoma:

Source: France 24
 
Mkuu kwa mfano mimi nakualika wewe kama nani yangu au kwenye function gani?

Nadhani wengi mnadhani mualiko wowote tu unatosha kupewa visa ila hamjui ni lazima muwe na ukaribu na huyo mtu na wewe as a visitor uonyeshe upo well established nyumbani na utarudi ili upewe visa kigezo ambacho vijana wengi hawana maana ndo wanatafuta maisha. Kama haupo vizuri bongo kwa maana ya a stable job, assets, ndoa, watoto, na hela visa ya kutembea kwa mualiko ni mtihani.

Niseme tu diapora wanatumia internet hii hii kutafuta hizo internships na kazi mnazotaka wawajulishe sio kwamba wanaenda kwenye hizo organizations in person. Wewe muhitaji ni bora kuwekeza nguvu nyingi kuzitafuta hizo nafasi, ukikpata ndo mshauriane na mtu wako wa karibu aliyeko huko. Hao diaspora wana majukumu mengine hawawezi kuacha majukumu yao na kushinda online siku nzima kukutafutia internships na kazi. Tujiongeze hapa tuache uzembe na lawama za reja reja.

Hakuna mtu anaogopa kuwapa muongozo ila you're asking way too much hata kwa mambo yaliyo ndani ya uwezo wenu. Mimi sina muda wa kumtafutia mtu chuo, passport au internship huo muda sina kabisa Ila akipata nitamsaidia all the way through ndo maana nilisema lazima ucheze part yako as well hakuna mtu ataacha majukumu yake kukusaidia wewe kila kitu.
asante sana nilitegemea jibu kama ili kutoka kwako mimi nimechangia mada tu kuhusu msaada sitegemei mtu yeyote hapa sky is the limit brother.
 
asante sana nilitegemea jibu kama ili kutoka kwako mimi nimechangia mada tu kuhusu msaada sitegemei mtu yeyote hapa sky is the limit brother.

That's the mentality. Ukijisaidia at least halfway watu watakusaidia be it wabongo wenyewe au watu baki. Nimesaidiana na watu baki kabisa ambao leo tumegeuka ndugu wengine wapo kutoka jukwaa hili hili la JF. Binafsi hiyo roho mbaya au kusema wabongo hawashirikiani naonaga ni story tu. Kama wao walifika basi inawezekana.
 
Acha uongo .tena ww uliyeandika huu Uzi ndo ulikuwa wa kwanza kunikatisha tamaa na ukaniambia niwe SHOGA ili nitimize ndogo zangu alfu Leo hii unaandika uongo ili kuonesha jamii kuwa ww ni kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu.mkuu acha kujitetea na kumbuka MTU mwenye sifa ya kusaidia MTU hajali kuwa anayetaka kusaidiwa ana kitu au hana ,kutoa ni moyo mkuu
Weka picha tuamini
 
That's the mentality. Ukijisaidia at least halfway watu watakusaidia be it wabongo wenyewe au watu baki. Nimesaidiana na watu baki kabisa ambao leo tumegeuka ndugu wengine wapo kutoka jukwaa hili hili la JF. Binafsi hiyo roho mbaya au kusema wabongo hawashirikiani naonaga ni story tu. Kama wao walifika basi inawezekana.
Asante kwa kuchangia mawazo brother.
 
Asante, hivyo vyuo vinavyotoa hizi post graduate mpaka ufike ndio navihitaji binafsi nimefuatilia poland gharama zao ziko reasonable bank statement ndio kipengele.
Vipi mawakala wa kazi huko na gharama zao!?
Bank statement unaweza tafuta ya mtu unaemfaham awe na mpunga kdgo, along with barua kusema atalipia/gharamia shule na pesa za matumizi yako ya kila mwez..
 
27 March 2023
Balozi Tom Amolo azungumzia nafasi za zilizopo za kuingia Germany kufanya kazi mbalimbali pia fursa za elimu ktk nchi hiyo ya ulaya. Balozi amefanya mahojiano ktk video hii kwa lugha sanifu ya kiswahili


Source : Nation

N.B
SERIKALI INA RASILIMALI ZA KUTOSHA KURASIMISHA RAIA KWENDA KUCHUKUA FURSA KIHALALI NJE YA NCHI

Ni mfano mzuri wa serikali kushiriki ktk kuwatafutia raia wake fursa, kuweka makubaliano ya visa, kazi za muda mfupi na mrefu masuala ya wananchi kupata pasipoti, masomo ya lugha za kigeni kuongeza uwezekano wa kupata kazi za aina zote n.k

Nchi kama nchi ya the Philippines 🇵🇭 kwa mfano inatoa uzito unaofaa kwa mafunzo ya somo la ziada kuhusu lugha na tamaduni za nje kupitia vyuo kibao vya kama Ras Simba zinavyoratibiwa kwa karibu ubora wake na serikali ili raia wake wapate ufahamu, connections, network na wepesi wakihitimu vyuo vya VETA, UBAHARIA, UUGUZI n.k moja kwa moja wanakwenda nchi za Ulaya, Canada, Mashariki ya Kati na Australia kufanya kazi .
Today, more than 10 million Filipinos—or about 10 percent of the population—are working and/or living abroad ........... When the Philippines launched an overseas employment program in the 1970s, the thrust was finding labor markets: The state not only promoted Filipino workers to the oil-rich but labor-short Gulf Cooperation Council (GCC) countries, it also sold these uncharted Middle East destinations to Filipinos. By the latter half of the 1970s, as deployment and competition with other origin countries increased, surfacing labor migration problems (including poor working conditions and abuse by employers) prompted the government to address migrant welfare and protection. As destinations diversified and women joined the labor migration flows, the protection aspect assumed more importance........ The Philippines: Beyond Labor Migration, Toward Development and (Possibly) Return

Hili suala la huku Tanzania mtu mmoja mmoja ktk diaspora kubebeshwa zigo la lawama wakati ilitakiwa serikali ya Tanzania iwe mstari wa mbele kuweka mazingira mazuri mikataba mizuri baina ya nchi na vyuo vyote kuwekewa
mtaala wa somo la lugha za kigeni na tamaduni za nje ili wahitimu wa Welding, makenika useremala udereva VETA, MUCHAS, UDSM, SAUT n.k wawe tayari kutimkia ngambo wakiwa wanajiamini kunyakua fursa.
 
Wagumu toka sehemu mbalimbali na safari zao kuelekea Marekani ya Kaskazini

Ungana nasi kwa kutazama video hii kufuatilia mguu kwa mguu toka wakiwasili jijini Sao Paolo Brazil wakijifanya raia wa Angola ktk utalii Brazil kisha wanaanza safari kwenda Canada.

Safari hii ya Wakongomani toka Congo wanaoingia Brazil bila viza kisha wanakutana na wahamiaji wengine toka nchi za China, Morocco, Mali, Senegal, Somalia, Nepal, Nigeria and Bangladeshi kwa miezi mitano wanakatiza mito misitu na barabara ktk nchi kumi za bara la Marekani ya Kusini kabla ya kuingia Marekani nia ni kufika nchini Canada.

Safari hii ya kilometa 20,000 wanakutana wa wahamiaji wengine toka nchi za Caribbean na Latino America ambao pia lengo lao ni kufika Marekani na Canada. Wakongomani lengo ni kufika jimbo la Quebec Canada linalotumia lugha ya Kifaransa kama Congo.

Safari hii inajumuisha kutembea kwa miguu, kupanda basi, taxi, punda, boti , ngalawa na kushirikisha wenyeji wa nchi hizo za Latin America ktk kuonesha njia za vichochoro vijijini zisizo ktk ramani za GPS maana wahamiaji wanatumia simu janja smart phone kutafuta welekeo kupuguza malipo kwa wavushaji watu kwa magendo pale inapowezekana.

Njiani katika njia za panya zilizobatizwa "Njia ya Kuzimu" kukwepa askari wa uhamiaji, kunaonekana utelezi utokanao na mvua zisizokoma za misitu minene ya tropiki, matope yafikayo ugokoni, makaburi yasiyo na jina wala alama za imani zao kwani hao wahamiaji waliopoteza maisha na sasa wamelala udongoni hata kaburini utambulisho wao haujulikani.

Nchi nyingi kama Colombia, Ecuador na Panama wameongeza vikwazo ktk vituo vya mipaka rasmi kutokana na mbinyo toka serikali ya Marekani. Hivyo wahamiaji na watu wote wanaojihusisha na biashara ya kusafirisha watu hutumia njia za vichochoroni kukwepa askari hao.

Pamoja na hayo bado kuna ongozeko kubwa la wahamiaji wanaoelekea Marekani ya Kaskazini wakiwa na imani ya kutafuta fursa na maisha bora zaidi. Wenyeji wa vijiji vya ndani ndani Colombia na Ecuador wanashangazwa na ari bila kusahau hamasa ya kusonga mbele ya hawa wageni toka nchi za mbali.

Watu watajiuliza unawezaje kukatiza nchi zaidi ya 10 salama bila kudhuriwa na wenyeji au magenge ya kutorosha watu mipakani.

Sababu ni kuwa hii ni biashara kubwa inayoingiza kipato na makundi ya waliokuwa wanasafirisha madawa ya kulevya sasa wamejiingiza ktk biashara hii ya kusafirisha watu. Hivyo wakubwa wa magenge haya hawataki kusikia mtu kakabwa au kina mama kubaka n.k na kuwataka wote wanaojihusisha na biashara hii ya kuvusha watu kimagendo mipakani kuwalipa 'kodi' ma drug lords na pia kuhakikisha wageni hao wanamaliza safari salama ili njia zao ziendelee kuaminiwa na maelfu ya wageni hawa waendao Marekani ya Kaskazini. Yeyote atakaye mdhuru mgeni huadhibiwa kwa adhabu kali na wababe hawa wa biashara hii ya kusafirisha wageni.



Endelea kusoma:

Source: France 24
Haaahaha safari kama hizi kizazi cha sasa cha wabongo hawawezi ndio maana hata ma shoga wameongezeka. Kizazi cha zamani watu walikua wanatambaa toka Pakistan wanakatisha Balkan hadi wanaingia ulaya, chakula ni mkate na maji. Hawa ma yoyoo wa sasa wanataka connection halafu na kuhifadhiwa juu na kazi uwatafutie. Hizi ni trip za wacongo, wakenya, wanaija, waghana na mataifa wengine wagumu wa africa sio hawa wa kubana pua eti wahifadhiwe. 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
POVU RUKHSA!
 
Hapo kwenye internship zipo, ila kuzipata ni issue
Diaspora mtusaidie kama mna njia rahisi
wabongo kwenye kusaidiana bado sana mfano mtu ana kila kitu passport,nauli na hela ya kujikimu akiwa mfano marekani kupata mchongo wa kwenda mbele inakua mziki wakati kuna mwaliko tena mtu anaweza kukulipa kidogo kufidia muda wako,kuna internship tunaweza kuonganishiana ata kwa malipo siyo mbaya au kusaidiana link ya vyuo vya bei nafuu kabisa ila kwa mbongo hapo kipengele kukupa mwongozo tuna ogopana sana..
 
Haaahaha safari kama hizi kizazi cha sasa cha wabongo hawawezi ndio maana hata ma shoga wameongezeka. Kizazi cha zamani watu walikua wanatambaa toka Pakistan wanakatisha Balkan hadi wanaingia ulaya, chakula ni mkate na maji. Hawa ma yoyoo wa sasa wanataka connection halafu na kuhifadhiwa juu na kazi uwatafutie. Hizi ni trip za wacongo, wakenya, wanaija, waghana na mataifa wengine wagumu wa africa sio hawa wa kubana pua eti wahifadhiwe. 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
POVU RUKHSA!
Povu langu wewe si Mbongo pia
 
Back
Top Bottom