Diaspora Wetu Wanafanya Nini cha Kuonekanika Huko Ughaibuni?. Diaspora Mliofanikiwa, Onekanikeni Kupitia TAK na Rudisheni Tanzania Japo Kidogo!

Diaspora Wetu Wanafanya Nini cha Kuonekanika Huko Ughaibuni?. Diaspora Mliofanikiwa, Onekanikeni Kupitia TAK na Rudisheni Tanzania Japo Kidogo!

Sijalisoma andiko lote lakini kwa ufupi, sidhani kama kuna diaspora ambae ana akili za kujionesha Tanzania, ili iweje?
Lengo la TAK, sio kujionesha kwa show off, bali ni the visibility of Tanzanians Diaspora success stories, angalia wenzetu Wakenya mbona wana cha kuonyesha

Sifahamu kama kuna diaspora ambae anaishi vizuri kisheria hajafanya kitu nyumbani.
Hapa sichunguzi diaspora wamefanya nini nyumbani, no, TAK inaangazia diaspora wetu wanafanya nini visible, ili na sisi tuwe na visibility
Kuna diaspora wengi sana, tena sana, ambao wamejiamulia huko nje walipo ndiyo kwao. Tanzania patabaki kuwa asili yake.
Naunga mkono uamuzi wao, na hawa hatuwagusi wala kuwatafuta.
Sheria za Tanzania za kuzuwia uraia pacha zimewafanya diaspora wengi wadhulumiwe na ndugu, jamaa na marafiki mpaka ikawakatisha tamaa kufanya lolote la maana Tanzania.
Hili linakwenda kuisha, dadio anatoa uraia pacha.
Kwa wengi, sisemi wote, kama mwenyewe haupo Tanzania, kuwekeza Tanzania imefikia kuwa kama mtu kuchukuwa pesa kuzimwaga shimo la choo.
Sad!
P
 
Mimi niliishia level ya kubeba box, sikufanikiwa kutusua, hivyo nikajirudia zangu Bongo. Hapa nawazungumzia diaspora wa Tanzania walotusua Marekani, wana vuta ma G -Wagon na ma Tesla, huku vijijini kwao walikotoka, kina mama wanajifungulia chini wanafunzi wanakaa chini kwa kukosa deski!.
Is this fair?.
P
Ila Paskali unatafuta lawama tu kwa waja.
 
Mwanangu umeamua kuwa chawa? Kwenda nje kwenyewe mbinde. Wakishafika huko, manawaita wasaliti. Mmewanyima uraia pacha. Angalia wenzenu Kenya wanavyovuna. Nashauri wanadiaspora wa Tanzania wekezeni nchi jiarani zinazoruhusu uraia pacha badala ya Tanzania. Mijitu maskini na ina roho mbaya hakuna. Mnapenda pesa zao lakini siyo wao. Msiwekeze huko. Mijitu mingi ni mijizi na ina roho mbaya hakuna.
 
Onyesheni mfano ili serikali ijione ilikosea! Hata wenzenu Kenya walianza kwanza kwa kutuma kidogo kidogo mpaka ikaona kumbe kuna fursa! Sasa nyie wa kwetu kulilia michango ya kusafirisha maiti tu! Mzikane huko huko msitusumbue sisi!

Unajua Kenya walikua wanatuma shingapi before and after dual citizenship?

Unajua sasa diaspora wa TZ wanatuma shingapi?
 
Kosa kubwa wanalifanya diaspora na kuwafanya wapate ugumu wa uraia pacha ni Kama anavyofanya huyo mdada kudai hawezi kuwekeza huku Hadi uraia pacha uruhusiwe.
Kama wangewekeza nyumbani kwa maswala ya afya, elimu, viwanda, kilimo wangetengeneza ushawishi mkubwa kuanzia kwa wananchi wa kawaida mpaka wanasiasa kupitishwa Sheria ya uraia pacha. Lakini wamewekeza ugenini huku kwao wameacha kwa kisingizio Cha kusubiri Mambo ya uraia pacha. Matokeo ukimwuliza mwananchi wa kawaida faida ya uraia pacha haioni.

Mwananchi wa kawaida hana sababu ya kujua umuhimu wa uraia pacha na diaspora hawaoni ulazima wa kuwekeza TZ au kurudi huko. Huko ni makaburini watarudi kuzikwa (kama wasipo amua kuzikwa walipo currently), viongozi wenyewe wanafia nje na kurudi kuzikwa tu TZ.
 
Wa Tanzania ni njaa kali maana wanaenda ughaibuni huku hawana elimu!

Kama mnajua hilo mnawatafuta wa nini? Kwanini ndugu Mayalla anatafuta watu njaa kali?

Kwanini serikali ya TZ inaweka lengo la kuongeza remittances za diaspora wakati wanajua hawana kitu?

Mnataka hela zao hapo hapo mnasema njaa kali. Tena hapo hapo mnawaomba connection kwenda huko 🤣
 
Kama mnajua hilo mnawatafuta wa nini? Kwanini ndugu Mayalla anatafuta watu njaa kali?

Kwanini serikali ya TZ inaweka lengo la kuongeza remittances za diaspora wakati wanajua hawana kitu?

Mnataka hela zao hapo hapo mnasema njaa kali. Tena hapo hapo mnawaomba connection kwenda huko 🤣
Jinsi mlivyo njaa kali, mnasuburi mfe ili mtuombe michango! Msitusumbue sisi!
 
Jinsi mlivyo njaa kali, mnasuburi mfe ili mtuombe michango! Msitusumbue sisi!

🤣 🤣

Usiwachangie mkuu acha wazikwe huko huko tuwakomoe.

Tusiwape uraia pacha ila pia tusiwasumbue na hizi media tour au kuwaomba hela.
 
Mtafuta Christina lasway ndio.raisi wa dicota mtu.wa.maana kabisa akili kubwa sana mchaga huyu. Mgoogle utapata contact.zake.

Usiogope akikukwepa maana watu.wanaangalia what.in.it.for em ndio wafunguke kwenye bongo media
 
Back
Top Bottom