Didier Drogba ashindwa Urais wa Shirikisho la Soka la Ivory Coast

Didier Drogba ashindwa Urais wa Shirikisho la Soka la Ivory Coast

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Mshambulizi wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, aliangushwa katika raundi ya kwanza ya upigaji kura wa Urais wa Shirikisho la Soka la nchini Ivory Coast ( FIF) kwa kupata kura 21 huku mahasimu wake Diallo (kura 59) na Diabaté (kura 50)

Katika raundi ya pili, Idriss Diallo, mfanyabiashara na mjumbe mkuu wa sasa wa FIF, aliibuka mshindi kwa kumuondoa aliyekuwa makamu wa Rais wa FIF Sory Diabaté kwa kura 63 dhidi ya 61

Uchaguzi wa Jumamosi katika mji mkuu wa kisiasa wa Yamoussoukro uliahirishwa mara kadhaa tangu 2020, hasa kutokana na masuala ya kuhusu kustahiki kwa baadhi ya wagombea, huku Drogba akiwa miongoni mwao.

Chanzo: BBC
 
Rafu za soka ni kali mno. Sidhani kama kuna taasi yenye hujuma na umafia kuliko hii ya soka.
Akajipange upya, kushindwa si mwisho wa pambano. Bado nafasi ya kupambana anayo huko mbeleni.
 
Rafu za soka ni kali mno. Sidhani kama kuna taasi yenye hujuma na umafia kuliko hii ya soka.
Akajipange upya, kushindwa si mwisho wa pambano. Bado nafasi ya kupambana anayo huko mbeleni.
Wajumbe tu alikosa sijajua rafu gani zilikuwepo ila Drogba naamini hana uwezo wa kuongoza soka uko kwao. Kucheza mpira na kuongoza mpira ni vitu viwili tofauti
 
Baada ya kuwajengea hospitali ya rufaa na kuwanunulia ma CT scanners na MRI scanners hii ndiyo asante wanauompa.

Anajipanga kupata Urais huu ili baadae agombee Urais wa nchi. Kuikosa hii nafasi ni pigo kubwa kwake.
 
Baada ya kuwajengea hospitali ya rufaa na kuwanunulia ma CT scanners na MRI scanners hii ndiyo asante wanauompa.

Anajipanga kupata Urais huu ili baadae agombee Urais wa nchi. Kuikosa hii nafasi ni pigo kubwa kwake.
Kuongoza mpira sio kwa sababu ya asante. Kujenga hospitali na kununua CT scanners ndio kunaleta uwezo wa kuongoza mpira? Kwani walikubaliana ajenge hospitali ili apewe urais, hiyo rushwa italipwa kwa njia gani. Waafrika tuna matatizo sana, kwahiyo kule Marekani kina John Hopkins walitakiwa wagombee urais
 
Rafu za soka ni kali mno. Sidhani kama kuna taasi yenye hujuma na umafia kuliko hii ya soka.
Akajipange upya, kushindwa si mwisho wa pambano. Bado nafasi ya kupambana anayo huko mbeleni.
Huku kwetu Msomali alipita bila kupingwa
 
Mnajuaje hana uwezo wa kuongoza wakati hajawahi kupewa nafasi akaharibu ?
Nafasi hapewi mtu kwa umaarufu kama ni hivyo wasingefanya uchaguzi wangemteua ambaye probability imemuangukia. Kuwa mchezaji mzuri na kuongoza chama cha soka havina uhusiano sana.

Efforts za Drogba hazipo kwenye mpira ndio maana mpenda ujenzi kasema Drogba anatafuta urais wa nchi. Mpira sio uchochoro wa kupanda ngazi nyingine. Tofauti na Etoo ambaye kwao ana mwamko wa soka waziwazi, Drogba hana motives za soka directly. Mashabiki wa soka kwao wanalijua hili. Hata hivyo kuna figisu ila hata tukija kwenye neutral ground sishawishiki kwamba ataleta mageuzi kulingana na mwenendo wake.

Mbona George Weah ni Rais wa Liberia na hana maajabu kafanya kulinganisha na mtangulizi wake mwanamama Ellen Johnson
 
Mshambulizi wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, aliangushwa katika raundi ya kwanza ya upigaji kura wa Urais wa Shirikisho la Soka la nchini Ivory Coast ( FIF) kwa kupata kura 21 huku mahasimu wake Diallo (kura 59) na Diabaté (kura 50)

Katika raundi ya pili, Idriss Diallo, mfanyabiashara na mjumbe mkuu wa sasa wa FIF, aliibuka mshindi kwa kumuondoa aliyekuwa makamu wa Rais wa FIF Sory Diabaté kwa kura 63 dhidi ya 61

Uchaguzi wa Jumamosi katika mji mkuu wa kisiasa wa Yamoussoukro uliahirishwa mara kadhaa tangu 2020, hasa kutokana na masuala ya kuhusu kustahiki kwa baadhi ya wagombea, huku Drogba akiwa miongoni mwao.

Chanzo: BBC
Tatizo laki walishasema wa ivory coast kuwa jamaa mbaili sanaaaa🤣🤣🤣🤣

Wenzie wanarudiki makwao kujenga hospitals mashule na academy ila yeye anaishi ufaransa alafu anataka urais huku kwenye mechi za ndani ya nchi huonekani
 
Nafasi hapewi mtu kwa umaarufu kama ni hivyo wasingefanya uchaguzi wangemteua ambaye probability imemuangukia. Kuwa mchezaji mzuri na kuongoza chama cha soka havina uhusiano sana.

Efforts za Drogba hazipo kwenye mpira ndio maana mpenda ujenzi kasema Drogba anatafuta urais wa nchi. Mpira sio uchochoro wa kupanda ngazi nyingine. Tofauti na Etoo ambaye kwao ana mwamko wa soka waziwazi, Drogba hana motives za soka directly. Mashabiki wa soka kwao wanalijua hili. Hata hivyo kuna figisu ila hata tukija kwenye neutral ground sishawishiki kwamba ataleta mageuzi kulingana na mwenendo wake.

Mbona George Weah ni Rais wa Liberia na hana maajabu kafanya kulinganisha na mtangulizi wake mwanamama Ellen Johnson
Huyu kwanza zakora alisema hafai kuwa rais wa shirikisho na ukumbuke wamecheza pamoja kwenye timu ya taifa.
 
Baada ya kuwajengea hospitali ya rufaa na kuwanunulia ma CT scanners na MRI scanners hii ndiyo asante wanauompa.

Anajipanga kupata Urais huu ili baadae agombee Urais wa nchi. Kuikosa hii nafasi ni pigo kubwa kwake.
Duh Tanzania kila jambo lina mjuaji hahaaaa
 
Huyu kwanza zakora alisema hafai kuwa rais wa shirikisho na ukumbuke wamecheza pamoja kwenye timu ya taifa.
Mtu kakulia Ulaya uko muda wenyewe wa kuishi nchini kwake sio mwingi mara nyingi yuko nje kwenye mishe zake. Mpira ndio hivyo hana mwamko nao, hana mahusiano na wadau wa soka sasa ataongoza na nani kama sio migogoro tu, wadhamini alikosa maana wadau wa soka wanajua hamna kitu. Then wabongo wanataka awe rais kisa alikuwa mchezaji mzuri
 
Back
Top Bottom