Mimi nashauri ukumbi wa Siasa ufungwe maana matusi na kashfa zimezidi
Niliomba kupewa tafsiri ya "kashfa", lilikuwa ni direct swali kwa SteveD, lkn haikuwa na maana kuwa wengine wasingeweza kuchangia! Vinginevyo tutakuwa tukijadili kitu tusichokijua.
Tanzania 1,
Samahani sikuweza kukujibu swali lako hapo awali. Kwa vile umetuuliza swali hapa lihusianalo na tafsiri ya neno, nitajitahidi tu kulijibu kwa uharaka haraka kama jinsi nionavyo miye. Naona kama ni kupata tafsiri fasaha kisheria kama ulivyo uliza, labda bora kulipeleka swali lako kwenye forum ya lugha, naamini kuna wataalam huko wanaweza lichambua ipasavyo..
'Kashfa' kama nilivyo iongelea mimi ni ile hali ya kuongelea kitu 'imani/dini' ya mwenzako kwa lengo mahiri kuwa unataka kumkosoa yeye, yakuwa anacho amini si halali na hakifai mbele ya macho yake na ya wengine, na jinsi unavyo ongelea swala hilo ni katika hali ya kudharau wala si kujenga hoja (logical reasoning) bali unafanya hivyo kwa msukumo wa imani yako, kitu ambacho nacho ni cha kuaminika tu pia.
Na imani kuwa kuna wengine wanaweza kulifafanua hili kwa undani na kwa kiswahili fasaha zaidi. Ahsante.
OOh, out of topic: Tanzania 1, avatar yako kiboko ndugu yangu.. nimeipenda sana tu..lol.
SteveD.
...'Kashfa' kama nilivyo iongelea mimi ni ile hali ya kuongelea kitu 'imani/dini' ya mwenzako kwa lengo mahiri kuwa unataka kumkosoa yeye, yakuwa anacho amini si halali na hakifai mbele ya macho yake na ya wengine, na jinsi unavyo ongelea swala hilo ni katika hali ya kudharau wala si kujenga hoja (logical reasoning) bali unafanya hivyo kwa msukumo wa imani yako, kitu ambacho nacho ni cha kuaminika tu pia.
Na imani kuwa kuna wengine wanaweza kulifafanua hili kwa undani na kwa kiswahili fasaha zaidi. Ahsante...
Kashfa maana yake ni ukweli uliofichwa, ukweli ambao ukitoka adharani utaondoa reputation ya mtu au jambo husika. Kasshfa ni sawasawa na neno la kiingrerza Scandal.
Mfano: Kama ueandika kitabu na watu wakagunduwa kuwa vile vilivyomo ndani ya kitabu hicho ni uwongo, that's Kashfa, kwa sababu watu wamegunduwa kuwa ulicho andika ni uwongo na hali ya kwamba wewe mwandishi au publisher umekusudia watu waamini kuwa kilichomo ndani ya kitabu chako ni kweli.
Kama mwandishi ameelezea jambo fulani ndani ya kitabu chake au amezungumzia machafu ya mtu fulani, na jambo hilo likaja kuonekana kuwa ni uwongo, hii Pia ni kashfa kwa mwandishi kwa mwandishi aliye andika na inapelekea kazi yake kuwa kwenye kundi la Libel. Yaani umesingizia.
Kwa upande wa dini kama jambo linaongelewa ni logical Reasoning, na likaonekana kuwa ni kweli, basi hiyo ni Kashfa kwa sababu umetoa kweli iliyofichwa dhidi ya kundi fulani.
Lakini maandishi yako na reasons zako zikithibitika kuwa ni uwongo tha's Libel dhidi ya mandishi yako.
Kwa ufupi neno KASHFA ni neno la kiarabu na maana yake ni kuelezea jambo la ukweli ambalo likitoka hadharani litaondoa reputation yako au kile unacho kiamini.
tupo hapa kutafuta solution ya ukumbi wa dini na wengine wameona huku huku walete hayo mambo yao ya kitoto.hivi unatuonesha nini? kwamba huwezi kujirekebisha au?.waswahili tuna tabu kweli kweli. haya lete kejeli nyengine.Dini muhimu ndugu zangu, lakini mbaya kukashifu madhehebu ya watu. Kwani dini nini? Wengi tunadhani dini ni madhehebu ya kiislamu, kikristo, kibudha nk. Dini kwa maoni yangu ni ile hisia ya kimaadili iliyoumbwa katika nyoyo za binadamu. Pahala fulani katika historia wakazuka watu au vikundi vya watu wakaamua kurasmisha mienendo ya watu wengine kufuata hayo maadili. Lakini wengi wa hawa watu walidandia migongoni mwa mawazo au mifano ya maisha ya watu wachache walioishi maisha ya mifano bora kimaadili kama kina Manueli au Yesu au Issa; au kina Muddy, samahani Muhammadi na wengineo. Kinachogomba sasa ni ushabiki wa wafuasi wa haya makundi, yaani madhehebu, SI DINI KWA MAANA YA DINI!
Kwa hiyo dini kwa maana ya masuala ya maadili ya kijamii, kiroho nk ni muhimu kujadiliwa kwa minajili ya kuongozana au hata kuongoana; tuachie tufwaidi hizo nondo kama kweli nondo zenyewe zina uzito na dawa mujarab kwa maisha yetu!
Dini muhimu ndugu zangu, lakini mbaya kukashifu madhehebu ya watu. Kwani dini nini? Wengi tunadhani dini ni madhehebu ya kiislamu, kikristo, kibudha nk. Dini kwa maoni yangu ni ile hisia ya kimaadili iliyoumbwa katika nyoyo za binadamu. Pahala fulani katika historia wakazuka watu au vikundi vya watu wakaamua kurasmisha mienendo ya watu wengine kufuata hayo maadili. Lakini wengi wa hawa watu walidandia migongoni mwa mawazo au mifano ya maisha ya watu wachache walioishi maisha ya mifano bora kimaadili kama kina Manueli au Yesu au Issa; au kina Muddy, samahani Muhammadi na wengineo. Kinachogomba sasa ni ushabiki wa wafuasi wa haya makundi, yaani madhehebu, SI DINI KWA MAANA YA DINI!
Kwa hiyo dini kwa maana ya masuala ya maadili ya kijamii, kiroho nk ni muhimu kujadiliwa kwa minajili ya kuongozana au hata kuongoana; tuachie tufwaidi hizo nondo kama kweli nondo zenyewe zina uzito na dawa mujarab kwa maisha yetu!
Huyo niliyemnukuu hapo juu nadhani ni mtu mzima, ila sidhani km anaelewe kinachojadiliwa hapa, and his mental health is questionable. Kutokana na hilo, naomba admin. im-ban at least ktk mjadala huu, o/wise hakukuwa na haja ya kuuanzisha mjadala huu, na k/hiyo hakuna haja ya kuuendeleza. THIS IS RIDICULOUS!!Kwa wote mliochangia mpaka hivi sasa;
Nashukuru sana kwa maoni yenu. Mwangaza nilioupata ni mkubwa kuhusiana na jinsi tunavyo ona majadiliano yahusuyo imani/dini yanavyo jiendesha hapa jamvini.
Kutokana na yale niliyoyasoma, miye pia naona ni bora jamvi la dini/imani libakie. Ila kimoja ni kuwa labda ni kumshauri ndugu Admin aongeze sana moderation/uhakiki katika hili jamvi bila kukwaza maoni ya watu. Ila nasi kama wachangiaji ni muhimu kuzingatia yale mengi wengi wetu tumeyasema kwenye thread hii, ya kuwa; Imani/dini ni kitu sensitive sana, na kwa wengine imani/dini inashika umbele kuliko hata wazazi, hivyo tupunguze maoni yanayoonekana ni kashfa zidi ya wengine katika hili. Pia kama tuna kitu tunakiona ni cha kukosoa/kuuliza kihusinacho na imani ya mwingine, basi tukiulizie/tukijadili katika hali ya ustaarab. Ni hayo tu kwasasa. Ahsanteni.
Kwa kweli bias ni mbaya! Nilipotumia majina ya aina zote kwa Issa haikuonekana mbaya, lakini kwa Muhammad ikawa noma!!! Poleni, nimeshakujueni. Kama admini watanifungia safi tu!!! Kwani wataninyima ugali??Tuvumiliane.
Kwa kweli bias ni mbaya! Nilipotumia majina ya aina zote kwa Issa haikuonekana mbaya, lakini kwa Muhammad ikawa noma!!! Poleni, nimeshakujueni. Kama admini watanifungia safi tu!!! Kwani wataninyima ugali??Tuvumiliane.
kina Muddy, samahani Muhammadi
Mkuu nakuunga mkono kabisa.Suala la imani ni la ajabu sana,wapo wachangiaji hapa JF katika mada zingine utasema hivi ni vichwa kwelikweli lakini akija huku kwenye imani utashangaa jinsi munkari unavyompanda hata anapoteza staha yake ile tunayoifahamu.Steve D,
Mimi ukiniuliza nasema ifungwe tu.. maana ni kutukanana kila kukicha unajua watu wanaochangia kule wanatetea Imani zao zaidi ya kujibu hoja!
Ndo maana neno kama Mpumbavu!!!! kutumiwa na watu huona ni poa...sasa watu wengine wanaokuja hapa jamvini wanajifunza nini!
Ifungwe kwa say 2 weeks hadi wachangiaji wajirekebishe kwanza!