Tanzania 1,
Samahani sikuweza kukujibu swali lako hapo awali. Kwa vile umetuuliza swali hapa lihusianalo na tafsiri ya neno, nitajitahidi tu kulijibu kwa uharaka haraka kama jinsi nionavyo miye. Naona kama ni kupata tafsiri fasaha kisheria kama ulivyo uliza, labda bora kulipeleka swali lako kwenye forum ya lugha, naamini kuna wataalam huko wanaweza lichambua ipasavyo..
'Kashfa' kama nilivyo iongelea mimi ni ile hali ya kuongelea kitu 'imani/dini' ya mwenzako kwa lengo mahiri kuwa unataka kumkosoa yeye, yakuwa anacho amini si halali na hakifai mbele ya macho yake na ya wengine, na jinsi unavyo ongelea swala hilo ni katika hali ya kudharau wala si kujenga hoja (logical reasoning) bali unafanya hivyo kwa msukumo wa imani yako, kitu ambacho nacho ni cha kuaminika tu pia.
Na imani kuwa kuna wengine wanaweza kulifafanua hili kwa undani na kwa kiswahili fasaha zaidi. Ahsante.
OOh, out of topic: Tanzania 1, avatar yako kiboko ndugu yangu.. nimeipenda sana tu..lol.
SteveD.