Diwani Athumani Msuya atenguliwa Ikulu

Diwani Athumani Msuya atenguliwa Ikulu

Mimi si mdau wa hiz mambo lakini huyo D-1 aelewe fika kwamba kuwa na siri za nchi si sababu ya kuwa na jeuri.Yeye hatakua DGIS mstaafu wa kwanza kustaafishwa pumzi zake.Anajua fika yaliyompata yule Lt.Gen kule Arusha mwaka 96.

Msimchonganishe na serikali na chama kwa vi thread vyenu hapa jukwaan kila uchwao aonekane hatii mamlaka za uteuzi
 
Tatizo nyinyi mmejiaminisha matatizo ya watu kutekwa na kupotea yameanzia kwenye utawala wa Magufuli na Diwani, mambo ya Watu kupotea au kufa yapo tokea enzi za Nyerere tena enzi za nyerere hata mitandao vyombo vya habari,hakukuwepo kama Sasahivi, hivyo walifanya walivyotaka enzi hizo tunasikiliza redio Tanzania (tbc)hata mtu wako akipotezwa hauwezi fungua mdomo kusema, Hata Sasahivi bado watu wanapotea tu sema bado mna mahaba na mama, kwenye utawala kuko hivyo kuna watu lazima waminywe ndipo unaweza kuendesha mchi maana wengine wako kwa ajili ya vurugu tu.



Hapana tumekataa utetezi huo wa kidhalimu.

Akipatikana mwenye kuleta fujo apelekwe kushtakiwa kwenye vyombo vya sheria na sio kumteka na kumpoteza au kumfanyia mateso,

Na hizi vurugu sheria iweke kipimo cha kujua kuwa ukifanyika hivi ni vurugu Au ni haki ya mwananchi.

Hata swala la uchochezi sheria iweke kipimo na isiwe ni mtazamo wa mtu Au kikundi cha watu fulani.

Usituambie Eti serikalini zote Duniani zinatesa na kuua watu , hapana unless iwe wamejiwekea kwenye sheria zao,

Kuua , kutesa ni kinyume na haki za kibinadamu,

Nchi yetu ni miongoni mwa nchi zilizo ridhia kuingia kwenye mikataba ya UN kuhusu kutunza na kuzingatia haki za binadamu.

Kwa hiyo usipotoshe kutaka ku-justify matendo maovu ya Viongozi wenye dhamana husika.
 
Mfano;

Katiba imetuhusu maandamo ya amani wazi kabisa,
Lakini ni ajabu kabisa tunapataga Viongozi ambao hawataki kusikia wala kuona jambo hilo,

Na cha ajabu wana apa kwa vitabu vitakatifu mbele za Mwenyezi Mungu na watu kuwa wataifuata Katiba ya JMT lakini kisha wanaenda kinyume?!

Imeandikwa; “Mwenyezi Mungu hadhihakiwi “

Tumuogope Mungu sana !
 
Tunataka uongozi wenye misingi ya sheria na Haki.

Actually ndio maana ya uongozi bora!

Kinyume chake ni uongozi dhaifu na dhalimu.
 
Mamba anatisha akiwa ndani ya maji, nje ya maji màmba ni sawa na mjusi tu.

Saa hizi ukimkuta Diwani Athman hata ukimtemea mate anaweza kukuomba wewe msamaha.

Mtoa mada umem over estimate Diwani bila sababu, I assure you he is nobody in this country.
Are you sure with this nonsence?

Diwani Sasa hivi aitishe press conference unazani Nini kitatokea? Dont undermine that man.

Hata uchaguzi wa 2025 akiamua asimame upande wa mpanzani wa CCM na aongea any shit Raia wataamini tu.

Once a TISS is always a TISS.
 
Ewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa taifa la Israel, Basi nikikwambia mlinde mtu huyu, na yule mtu akapotea nawe usijue alikokwenda, roho yako itakuwa mahali pa roho yake
 
Kombe hakufikia cheo cha Lt General, wacha kudanganya watu hapa!
Screenshot_20230107_075441_Chrome.jpg
 
Watu wenye mamlaka wanachukia sana vitu viwili, usaliti na dharau. Hivyo vitu viwili sio rahisi kusamehewa.
Mie nafikiri fikiri labda mkurugenzi alikuwa kemp iliyokuwa haimtaki Bi Mkora maana tunaona mshikaki kama vile bado upo jikoni?
 
Ameukataa uteuzi na siyo kutenguliwa, niliandika hapa juzi! Iweje Mkurugenzi TISS kupelekwa Ikulu?

Diwani ni mwenye kujitambua, ameukataa uteuzi ule. Diwani ana uzoefu na serikali zaidi ya nne za CCM.

Diwani ni afisa aliehudumu idara mchanganyiko za nchi hii kwa kiwango cha juu. Diwani anaijua michezo yote ya CCM na magenge yake. Diwani sio Kabudi au Lukuvi!

Diwani ndiye afisa mwenye siri nzito za kilichojiri kati ya serikali hizi mbili. Serikali ya Magufuli na hii ya Samia!

Pia ieleweke yeye ndiye alikuwa madarakani wakati JPM anafariki Dunia. Yote yaliyojiri katikati hapo, ni Diwani ndiye anaeyajua!

Diwani sio wa kubezwa! Diwani anastahili kupewa ulinzi kwa usalama wake! Kitendo cha kuikataa safe house, ina maana amekataa ku surrender mawasiliano yake yote ili kuanza kutumia mapya ya Safe House!

Na mengi bado yanakuja, maana kadri inavyonyesha ndio matobo yanavyozidi kuonekana.

"Rais Samia atengua uteuzi wa Diwani Athumani"

Mwananchinewspaper
Alhamisi, 05/01/2023.

Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Ikulu, Kamishna Diwani Athumani uliodumu kwa siku mbili baada ya kuteuliwa akitokea Idara ya Usalama TISS.

Kamishna Diwani aliteuliwa Januari 3, 2023 kuwa Katibu Mkuu wa Ikulu, akitokea katika wadhifa wa Mkurungezi Mkuu wa TISS, nafasi aliyohudumu kwa siku 1,210 tangu alipoteuliwa na Rais wa awamu ya tano, Hayati John Magufuli.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Januari 5, 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus, imeeleza kuwa nafasi ya Diwani imechukuliwa na Mululi Mahendeka aliyekuwa ofisa mwandimizi wa Ofisi ya Rais, Ikulu.

Alamsikhi
10101.
Imrani Kombe RIP
 
Hata mkurugenzi wa TISS, IGP na CDF wanafanyiwa ujasusi pia ili kuwa na uhakika kuwa wakati wote wapo kwenye mstari.
Lakini si watajua tu kuwa wanachunguzwa, sababu hao wakurugenzi wa hizo Idara au taasisi nao si wamewaweka watu wao binafsi au wasaidizi wao kufuatilia nani anaewafuatilia!!


Huyu bila shaka kuna makosa amefanya, akashushwa na kupelekwa karibu ili achunguzwe zaidi mienendo yake. Huenda ndani ya muda mfupi wa uteuzi kuna taarifa mbaya zaidi zimemfikia mkuu wa nchi kiasi cha kuonekana kuwa hafai hata kwa nafasi hiyo au pengine anafikiriwa kwa nafasi tofauti na hiyo.
Kwani kukataa uteuzi ni lazima iwe expressly? Si inawezekana kabisa mtu kukataa impliedly kwa kufanya jambo la kukera au la ovyo ili aliyekuteua akutengue. Yeye aone amekufukuza na kumbe amefanya kile ulichotaka akifanye. Chukulia hii, kwamba kuna uwezekano kweli alifanya makosa akiwa Mkuu wa TISS akaondolewa hapo kama adhabu ila hajakubaliana na adhabu kaamua kuikataa kwa kufanya jambo lingine bovu ili aondokane na fedheha ya kukaa ikulu.
 
Nafikiri kitendo cha kulazimisha iwe awamu ya sita na sio ya tano kikatiba ndio kitaisumbua nchi sana mpaka kufika 2025
Mkuu, Katiba ya JMT haina mambo ya awamu. Hakuna awamu ya 1 au ya 6 kikatiba. Mambo ya awamu ni ya mazoea tu, sio ya kisheria (kikatiba)

Mkuu, Urais ni taasisi flaan kuuuuuubwa mno. Anaekaa kwenye kiti cha Urais hajiongozi mwenyewe katika maamuzi!
Siku ya kwanza, SSH kuwa 'Rais' alitangaza maombolezo ya siku 14 badala ya 21. Hii inatosha kukuaminisha kuwa ama Rais anajiongoza mwenyewe ama hiyo taasis flaani kuubwa inafanya makosa tu sababu ina binadamu na sio miungu. Kama inafanya makosa, kuna uwezekano wakawa hawajafikiri yote kama ulivyomuuliza mleta mada. Ni binadamu tu kama walivyo wengine
 
Hahahaha, Gereza la Ukerewe. Hivi unajuwa nini kilimleta mle Gerezani? Alikuja kiwatoa wale walioshikwa na dhahabu. Polisi hawakujua kuwa ni mchongo wake na Kagame wakawakamata. Ila wajinga wanasema Magufuli alikuwa mzalendo, nawadharau sana
Hivi mkuu Stuxnet baada ya kumjibu jiwe kuwa amekuinua siku ile pale butimba, alikupeleka wapi? maana sijakuona tena.
 
Nao unakua wewe. Eti umtemee mate.! Akili za vijana wa bavicha hizi
Fasihi haiko wazi kwa wote, mpaka uwe na akili ndiyo utaelewa sarcasm au satire iliyotumika kwenye "kutema mate". Nendeni shule UVCCM mtanishukuru baadaye
 
naamini hakuna baya litakalotokea, TZ kanyaga twende. kwani tangu uhuru hakuna mwenye cheo kama chake aliwahi kuondolewa?!?,kama yupo au wapo nini kilitokea?!?. KANYAGA TWENDE MAMA
 
Back
Top Bottom