Sema aina ya muziki aliouchagua Dizasta, kwa bongo una wafuasi wachache sana.
Hata kazi zake ukiangalia kwenye digital platforms nyingi number hazisomi vizuri na kwenye show ni ngumu kusikia jina lake.
GK alikuwa super star wa daraja la juu linaloelekeana na wasanii kama Prof Jay au Afande huku akilibeba kundi zima la East Coast kwa kutoa ngoma zinazobamba masikioni mwa wengi.
Binafsi nazielewa kazi kadhaa za D ila ameshindwa kuifikia hadhira kubwa.
Hitimisho, mshaurini D aboreshe sanaa yake iendane na mahitaji ya walaji walio wengi kuliko kuibakiza sanaa yake mafichoni.
Kwa hatua aliyonayo ni ndogo sana kiasi cha kumkosea heshima GK kwa kufananishwa na wachanga wanaotafuta kutoboa bila mafanikio licha ya kuwepo kwenye game kwa miaka kadhaa sasa.